November 29, 2011

HATIMAYE MUSWADA MABADIRIKO YA KATIBA WAWA SHERIA!





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Novemba 29, 2011, ametia saini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011.

Hatua hiyo ya Mheshimiwa Rais kutia saini Muswada huo inakamilisha safari ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge kuwa limepitisha Muswada huo uliowasilishwa na Serikali katika kikao kilichopita cha Bunge.

Aidha, kutiwa saini kwa Muswada huo ili uwe Sheria ni hatua kubwa na muhimu katika safari ya kutungwa kwa Katiba mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais Kikwete katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Desemba 31, mwaka jana, 2010.

Pamoja na kutiwa saini hiyo bado Serikali itaendelea kusikiliza maoni na mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.

Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yoyote mwenye maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

KATIBA MPYA - CHADEMA NA RAIS WAKUBALIANA



MAKUBALIANO YA RAIS NA CHADEMA YALIVYOLIPOTIWA:

HABARI LEO: JK, CHADEMA MWAFAKA.
MUSWADAwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 uliopitishwa na Bunge hivi
karibuni utasainiwa na Rais Jakaya Kikwete kama ilivyopangwa.

Hali hiyo inatokana na makubaliano yaliyofikiwa jana kati ya Rais na Kamati ndogo ya Chadema iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe.

Juzi na jana, pande hizo mbili zilikuwa na mazungumzo kuhusu Muswada huo ambao ulipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila ushiriki wa wabunge wa Chadema na wa NCCR-Mageuzi ambao walisusia.

Kususia mjadala wa Muswada huo kwa wabunge hao wa vyama hivyo, ulitokana na madai yao ya kutaka Muswada huo usomwe mara ya kwanza bungeni wakidai haukuwa umesomwa na wananchi na kuuelewa, hivyo kukosa kuuchangia, lakini walikataliwa na Spika Anne Makinda.

Kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa jana Ikulu Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi na Kaimu Katibu Mkuu Chadema, John Mnyika, kutakuwa na haja ya sheria hiyo baada ya kusainiwa kuendelea kuboreshwa, ili ikidhi mahitaji ya kujenga na kuaminiana na mwafaka wa kitaifa.

Pia kutakuwa na mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha mwafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba mpya.

Awali ilielezwa kuwa mazungumzo hayo yalifanyika katika mazingira ya uelewano ambapo Rais Kikwete aliwahakikishia Chadema kuwa yeye na Serikali yake wana dhamira ya kuhakikisha Tanzania inapata Katiba mpya.

Kulingana na hatua iliyofikiwa jana, Rais atasaini Muswada huo kuwa sheria ambayo inatarajia kuanza kutumika Desemba mosi, lakini wakati ikiendelea kutumika, kutakuwa na fursa ya kuifanyia marekebisho endapo haja itajitokeza.

Hili si jambo jipya kwa masuala ya uandishi wa Katiba mpya, kwani hata ya Kenya ilipitishwa na mpaka sasa zipo taarifa kuwa imeshafanyiwa marekebisho mara 11 kutokana na mahitaji yanayoibuka kwa kuzingatia mazingira na muktadha.

Makubaliano ya jana, yanamaliza sintofahamu iliyokuwa imeanza kuibuka kwa Chadema na makundi mengine kutaka kufanya maandamano nchi nzima, kupinga Muswada huo kusainiwa na kushinikiza urejeshwe bungeni kusomwa kwa mara ya kwanza.

Lakini pia kunatoa fursa pana kwa wawakilishi na wabunge kurudi kwa wananchi kuwahimiza kujitokeza kutoa maoni na mawazo yao kuhusu aina ya Katiba inayotakiwa na Watanzania wote.



MWANANCHI - JK, CHADEMA WAKUBALIANA KUBORESHA MUAFAKA.
RAIS Jakaya Kikwete na viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe wamekubaliana kwamba ipo haja ya kuendelea kuuboresha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 ili ukidhi mahitaji ya kuaminiana na mwafaka wa kitaifa.Pia, wamekubaliana yawepo mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha mwafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba Mpya.

 Makubaliano hayo yamefikiwa jana na kusainiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi baada ya kumalizika kwa mkutano wa siku mbili baina ya pande hizo mbili kuhusu muswada huo.

 Katika kikao cha jana Mbowe aliongozana na wajumbe wa kamati hiyo Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara) Said Arfi na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) Said Issa Mohamed, Mshauri wa Masuala ya Siasa wa chama hicho, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Tundu Lissu na John Mrema.

 Katibu Mkuu Dk Willibrod Slaa ambaye ni mjumbe hakuwapo katika kikao cha juzi na cha jana na taarifa zilizopatikana baadaye na kuthibitishwa na yeye mwenyewe ni kwamba alikuwa safarini kwenda kuhudhuria kesi yake mahakamani Arusha jana.

 Kabrasha lililokabidhiwa na ujumbe wa Chadema kwa Rais Kikwete lilikuwa lina waraka uliotoa mapendekezo mbalimbali ya kurekebisha muswada huo huku wakitaka sheria iweke wazi kwamba Rais hana mamlaka yoyote juu ya Bunge Maalum la Katiba zaidi ya mamlaka ya kuliitisha kwa mara ya kwanza na kwamba mamlaka ya Bunge hilo yataisha mara baada ya kupitishwa kwa Katiba Mpya katika Bunge Maalum la Katiba.

 Wametaka ifanyike hivyo kwa kuwa sheria hiyo inampa Rais mamlaka juu ya Bunge Maalum la Katiba wakati Bunge hilo linatakiwa kuwa chombo huru na chenye mamlaka ya juu kuliko mamlaka nyingine zozote katika nchi.

 Katika waraka wao, Chadema wameeleza kutaka vifungu vyote vinavyokiuka haki za kimsingi za kikatiba vifutwe na kuwapo na uhuru kamili wa kujadili, kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi juu ya utungaji wa Katiba Mpya hata kama itakuwa kinyume na matakwa ya Tume ya Katiba na masharti ya Sheria hiyo.

Katika ukusanyaji na uratibu wa maoni ya wananchi juu ya Katiba Mpya na masuala ya muungano wametaka ziundwe tume mbili za katiba, moja itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya kwa ajili ya masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanganyika na ya pili itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi juu ya masuala ya Muungano.

THE CITIZEN – JK, CHADEMA Talks:  The Way forward
The government and the opposition Chadema party have agreed in principle that the newly passed Constitutional review Act 2011 bill needs major amendments.

A joint statement issued yesterday by the two sides at the end of two days  of consultations, said that the bill should be improved so as to bring  it to the requirements of building a national consensus as well as cohesion. The one page statement signed by the minister for Information, Youth, Culture and Sports, Dr Emmanuel Nchimbi, on behalf of the government and Chadema Director for Foreign Affairs and International relations, Mr John Mnyika, notes also that the talks were conducted in a cordial atmosphere.


The two sides also agreed in the closed door talks that there was a need  for the government and other stakeholders to hold constant  meetings and consultations, for the purpose of building and strengthening national consensus during the process of crafting a new Constitution.

The agreement has brought the two sides at the middle ground. The Chadema team, which was led by its national chairman, Mr Freeman Mbowe, went into the talks with  a strong proposal that President Kikwete should not sign the new Bill into law.

On the other hand, the government believed that the bill was perfect and President Kikwete indicated that he would  endorse it despite sentiments from Chadema and a number of activists under the banner of Tanzania Constitution Forum (TCF).

President Kikwete, his government and the Parliament, insisted that the Bill has no flaws as it followed all legal  processes and procedures during its processing before it was passed by the Parliament more than a week ago.

Chadema MPs boycotted the debate on the Bill in Parliament in protest over claims that the authorities did not give common Tanzanians an  opportunity to widely discuss one of “the most important pieces of legislation to have been drafted in the last 50 years.”

And the thrust of  the Chadema message to President Kikwete and his team during the talks centred on rejecting the Bill, asking that it should not be assented, and its processing start afresh.

In their letter to the President, a copy of which was seen by The Citizen, the opposition party pleaded with  the Head of State not to assent the Bill so as to give time for wananchi to air their views on it. They also argued that there is a need for wananchi to be educated about the Bill as experience has shown that most people believe that what was passed was a new Constitution. Chadema said there was a need to first amend the current constitution in order to align it with prevailing conditions, in order to have a level playing field between the two sides of the Union during the writing of a new Constitution.


DAILY NEWS - Kikwete, Chadema reach consensus
PRESIDENT Jakaya Kikwete will soon sign into law the Constitutional Review Bill following a two-day meeting with a delegation from the opposition Chadema that apparently held different views.

 This means that the review process will start anytime from now, putting to an end heated debate and forums on the same that recently dominated the country’s political scene.

 A press statement signed by the Minister for Information, Culture and Youth, Mr Emmanuel Nchimbi, and Chadema Acting Secretary General John Mnyika reiterated that the meeting was conducted in a friendly atmosphere.

 The five-hour long meeting that started from 10am at the State House in Dar es Salaam on Monday, concluded that despite the Bill being passed by Parliament, it would be amended if and when necessary for it to win public trust and national consensus.

 The two parties also underscored the need for frequent communications and cooperation between the government and other stakeholders on improving the law to maintain national consensus during the constitutional review process.

 The CHADEMA delegation was led by the party’s National Chairman, Mr Freeman Mbowe. On Sunday, President Kikwete received recommendations on constitution review from CHADEMA. Both parties agreed that the process should adhere to the interest of the nation much as it should also refrain from dividing the public according to their religion, tribe and region.
 Last week, CHADEMA sought the president’s audience over the constitutional review Bill after their bid to stop a second tabling of the constitutional review Bill in parliament by staging a walk-out failed.

 Demonstrations planned by activists scheduled for Saturday to press President Kikwete not to sign into law the constitutional review Act were banned by police for fear that they would escalate into chaos. 

My take: 
Hizo YELLOW, sijaelewa sawasawa, labda wataalamu wanaweza kunisaidia, mnisamehe kwa kutokuelewa kwangu muafaka huu hasa kutokana na nukuu hizo. 

November 28, 2011

Movie debut: How Canon's C300 camera was created - British Journal of Photography

Movie debut: How Canon's C300 camera was created - British Journal of Photography:



When Canon announced that it was developing a new concept digital SLR with 4K video recording capabilities, photographers wondered whether the new model would be the long-awaited EOS 5D Mark III.


And while the new concept camera has so far remained unnamed, Mike Owen, Canon's European professional communication manager, in an interview with BJP's news and online editor Olivier Laurent at the Cinema EOS launch event in Berlin, confirmed that the camera [pictured above] will not be part of the firm's EOS range of still cameras.

"The Cinema EOS system is a system," he tells BJP. "It will have multiple products as the EOS product line has, and the thing that will tie all of this together will be the lens mount, because we feel that our lenses are one of our key assets. But when it comes to the concept camera, that will be part of the Cinema system, and the still EOS range will continue to develop as it has been over the past few years."

The confirmation comes as Canon is heavily promoting its Cinema EOS C300 camera to the European market, which, despite its fragmentation, is home to the world's largest filmmaking community. "It's always difficult to address a fragmented market when launching a new product," says Owen, "but it's the same with every single product we launch. We always try to have, as much as possible, a unified European approach to launching products. But, in terms of the implementation of the message, it can very complicated. One message, for example, that might work in the UK might not work in the Middle East."

"KUPANDISHA POSHO ZA WABUNGE 154% NI UKICHAA"


Nimeshtushwa sana na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa Wabunge. Nimeshtushwa zaidi kwamba Posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua maana maslahi yote ya Wabunge huamuliwa na Rais Baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge.


Wabunge wote watambue kwamba kuamua kujipandishia posho zao bila kuzingatia Hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano. Mbunge yeyote ambaye anabariki Jambo hili au anaishi hewani haoni tabunza wananchi au ni mwizi tu na anaona Ubunge ni Kama nafasi ya kujitajirisha binafsi.


Kwa Wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni uamuzi wa chama na ni uamuzi wa kisera. Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi. Nimemwomba Katibu Mkuu wa chama kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hili.


Toka tarehe 8 juni mwaka 2011 nilikataa kupokea posho za vikao. Popote ninapohudhuria vikao huomba Risiti ya fedha ninazokataa. Baadhi ya Wabunge Kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho.


 Nampongeza kijana mwenzangu kwa uzalendo huu. Nawataka wabunge wengine wenye Moyo wa dhati kukataa sio tu ongezeko hili la posho Bali posho yote ya vikao. Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa?

Tazama nchi hii, juzi serikali ilipokea Msaada wa tshs 20bn kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa 28bn Kama posho za kukaa tu.

Tanzania inaagiza gesi ya matumizi ya nyumbani kutoka nje kwa kutumia mamilioni ya dola za kimarekani. Kuwanda cha kutengeneza LPG kinagharimu tshs 35bn tu, Wabunge peek Yao kwa mwaka wanatumia 28bn kwa posho za kukaa tu achilia mbali mishahara na marupurupu mengine.

Ipo siku Watanzania watatupiga mawe kwa usaliti huu dhidi yao.

Zitto Kabwe(MB)
Kigoma Kaskazini -Chadema

PRESS RELEASE - IKULU


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wa Serikali yake leo, Jumapili, Novemba 27, 2011, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

 Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, yamefanyika katika mazingira ya urafiki na ujumbe wa CHADEMA umewasilisha mapendekezo yake kuhusu mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya Tanzania. Serikali imepokea mapendekezo hayo.

 Hata hivyo, pande zote mbili zimekubaliana kukutana tena asubuhi ya kesho, Jumatatu, Novemba 28, 2011, ili kuipa nafasi Serikali iweze kutafakari mapendekezo hayo.
 

Lakini pande hizo mbili zimekubaliana kuwa Katiba ya sasa ni Katiba nzuri iliyolilea Taifa kwa miaka 50 iliyopita kwa sababu ni Katiba ya sasa iliyoliwezesha Taifa la Tanzania kuwa na amani, utulivu na kupata maendeleo makubwa ambayo nchi yetu imepata mpaka sasa.

 Pia pande zote mbili zimekubaliana kuhusu umuhimu wa kutunga Katibu Mpya kama Mheshimiwa Rais Kikwete alivyoliahidi taifa wakati wa salamu zake za mwaka mpya Desemba 31, mwaka jana, 2010, Katiba ambayo italiongoza Taifa la Tanzania kwa miaka mingine 50 ijayo.

 Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Rais aliwahakikishia wajumbe hao wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Mheshimiwa Freeman Mbowe kuwa ni dhamira yake na ya Serikali yake kuhakikisha kuwa Tanzania inapata Katiba mpya.

 Katika mkutano huo, pande zote mbili zimekubaliana kuwa ni jambo muhimu sana kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba Mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na umoja wa kitaifa.

 Aidha, pande zote mbili zimekubaliana kuwa mchakato huo uendeshwe kwa kuzingatia misingi ya mambo mengine muhimu kwa taifa la Tanzania kama vile kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, kuligawa Taifa kwa misingi ya udini na ukabila ama kutugawa kwa misingi ya maeneo.

 IMETOLEWA NA: KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU NOVEMBA 27, 2011
 DAR ES SALAAM

November 27, 2011

JK akutana na CHADEMA IKULU

 Rais Jakaya Kikwete akimkaribisha Ikulu Mwenyekiti wa CHADEMA na Kiongozi wa upinzania bungeni Freeman Mbowe na ujumbe wake kwa mazungumzo.
Rais Jakaya Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa CHADEMA, pamoja na baadhi ya mawaziri na maafisa wa Ikulu muda mfupi kabla ya kuanza kwa kikao chao.
Picha na K-VIS blog.

November 25, 2011

TAKO LA SIMENTI!!!!! KINA DADA MWAPATA SOMO GANI HAPO

Dada mmoja huko Miami  Marekani aliyekuwa akitaka kwenda kufanya kazi ya uchangudoa katika klabu za usiku amejikuta akiweza simenti katika makalio yake katika kutafuta gharama nafuu za kukuza makalio ili avutie wateja, ifuatilie zaidi hapo chini, 
Oneal Ron Morris

A woman who wanted to work at a nightclub started searching for someone who could perform plastic surgery at a cheap price to give her a curvier body. Police say what she found was a woman posing as a doctor who filled her buttocks with cement, mineral oil and flat-tire sealant.

The suspect -- who police say was born a man and identifies as a woman -- apparently performed the surgery on herself, and investigators say she may have victimized others. Oneal Ron Morris, 30, was arrested
 Friday after a year on the lam and has been charged with practicing medicine without a license with serious bodily injury.

Police photos show Morris as a small-framed woman with bee-stung pouty lips, arched eyebrows, oversized hoop earrings -- and a large backside. She was released from jail on bond. A phone listing for Morris could not be found, and it's unclear if she has an attorney.

Miami Gardens Police Sgt. Bill Bamford said Sunday that Morris bounced from house to house for a year, driving a black Mercedes and staying out of investigators' sight "like a ghost." An officer drove by one of those possible houses nearly every day on his way to work and saw the car outside on Friday, and he arrested Morris soon after.

The victim, who is not being named due to medical privacy laws, paid $700 for a series of injections in May 2010. She was referred to Morris by a friend.

Morris injected some type of tube in several sites around her bottom, pumping it full of a toxic concoction. Morris reassured the woman when the pain became too intense, police said.

Bamford said Morris told the woman, "`Oh don't worry, you'll be fine. We just keep injecting you with the stuff and it all works itself out."'

Bamford said the victim was reluctant to come forward. She quickly went to two South Florida hospitals due to severe abdominal pain and infected sores on her buttocks accompanied by flu-like symptoms. But she left each time, too embarrassed to tell doctors what she'd done.

Her mother eventually took her to a hospital on Florida's west coast, where alarmed doctors pressed her for information. They alerted the Department of Health.

"The doctors knew no licensed physician in his right mind would ever do this," Bamford said.
The victim is still recovering from the surgery and says it's too painful to work. She also has racked up numerous medical bills.

Authorities believe there are other victims who may be too embarrassed to come forward.
"(Morris) was readily introduced to our victim as someone who could help improve her shape, so we believe (she's) done this to other people," Bamford said.

  Source: Fox News.com 

Mvua zaleta maafa!



WATU wawili wamekufa na wengine watatu kunusurika baada ya lori walilokuwa wakisafiria kusombwa na maji katika daraja la Mto Loobuko kati ya Makuyuni na Mto wa Mbu wilayani Monduli.


Ajali hiyo ilitokea jana saa 12 alfajiri wakati lori hilo namba T190 AKW likiwa limebeba mitambo ya kutengeneza barabara likitoka Engaruka kwenda Arusha, kukumbwa na dhahama hiyo.

Maafa hayo yametokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika milima ya Monduli.

Mfanyakazi wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), Augustino Masige, akiendesha gari namba T573 AHW, akitoka Arusha kwenda Musoma ni miongoni mwa watu walionusurika katika maafa hayo baada ya gari lake aina ya Toyota kusombwa na maji eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Jowika Kasunga, aliwataja watu waliokufa kuwa ni dereva wa lori hilo aliyetambuliwa kwa jina moja tu la Shekman (38) na msaidizi wa mitambo ya kutengeza barabara, Samwel Julius (28).

Kasunga alisema watu hao walisombwa na maji umbali wa kilometa moja huku msaidizi wa opareta wa mitambo, alikutwa amenasa kwenye miti huku amekufa.

Dereva alikutwa amekufa umbali wa kilometa moja baada ya kugunduliwa na wanafunzi wa shule za msingi waliokuwa wakirejea nyumbani kutoka shuleni.


Kwa hisani ya Father Kidevu blog

MAFURIKO YA SENENE


Wakti mikoa mingine ni mafuriko na hata kufikia watu kupoteza maisha na miundombinu kuharibiwa, mkoani Kagera ni tofauti, wao ni mafuriko ya senene, kitoweo wakipendacho ata kusema kuwa ni tamu kuliko nyama.  tembelea hapa kwa picha zaidi.

GAMBA LAWA LA KOBE!


Nipashe: LOWASSA AJIELEZA NEC
Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imemaliza kikao chake jana huku aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, akisimama na kutoa dukuduku lake kuhusiana na tuhuma za ufisadi dhidi yake.

Kikao hicho cha siku mbili kilichoketi chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete, ambacho kilimalizika jana saa 11:30 jioni, mtoa habari wetu alikuwa ndani ya kikao hicho alisema Lowassa, alisimama na kueleza masikitiko yake juu dhana ya kujivua gamba ilivyoendeshwa wakati kikao hicho kikijadili hali ya siasa nchini.
Chanzo chetu kilimkariri Lowassa akisema kama ni suala la kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, alitaka kuuvunja mkataba kati ya kampuni hiyo na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) mapema, lakini Rais Kikwete aliyekuwa nje ya nchi alikataa kufanya hivyo na badala yake alimwambia kuwa anasubiri ushauri wa makatibu wakuu wa wizara.

Alisema aliamua kujiuzulu nafasi zake katika serikali ili kulinda heshima ya serikali na chama chake, lakini anashangazwa na hatua ya wanaCCM wenzake na si wapinzani kuzunguka mikoani kumchafua wakidai kuwa yeye ni fisadi.

Lowassa alimkumbusha Mwenyekiti kuwa kumekuwa na utamaduni wa kupikiana majungu ndani ya chama na kukumbushia tukio la yeye (Kikwete) kuzushiwa mengi na Daud Mwakawago wakati wa harakati za kuusaka urais kabla ya 2005.

“Mwenyekiti wewe unakumbuka wakati Mwakawago alipokuja na rundo la tuhuma za hisia, isingekuwa busara za Rais Mkapa (Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa), wewe usingekuwa hapo ulipo,” chanzo hicho kilimkariri Lowassa akisema.




Daily News: NO EXPULSIONS NEC WINDS UP MEETING 
THE National Executive Committee of the Ruling Party, Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM), on Thursday ended its two-day meeting without expelling or stripping some prominent cadres of their posts as speculated earlier.

However, the Dar es Salaam Regional Party Secretary, Kilumbe Ng'enda, was relieved of his duties.

The party's Ideology and Publicity Secretary, Mr Nape Nnauye, promised reporters here on Thursday that he would address a press conference on Friday.

Sources from the meeting however told the 'Daily News' that the meeting resolved to forward the 'cleansing and skin shedding' business to the Ethics and Security Committee, and the Central Committee (CC-CCM).

"The meeting decided that any CCM member who has evidence of wrong-doing by the cadres should submit it to the two committees for appropriate action," revealed the source.

Another high-profile NEC member said the meeting resolved to 'cleanse' the party without breaking it up.

"NEC members debated the philosophy, it was decided it should be conducted with sobriety and with evidences," revealed another NEC member.




 Mwananchi: LOWASSA, SUMAYE WABWATUKA NEC
MAWAZIRI Wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, jana walishambulia kwa maneno makali wajumbe wawili wa Sekretarieti ya CCM kwamba wamekuwa wakikivuruga chama na kusababisha mgawanyiko uliopo.Lowassa aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu, kutokana na kashfa ya Richmond ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzungumzia suala hilo wakati wa mjadala wa hali ya siasa, katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kilichomazika jana mjini Dodoma.

Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zinasema Lowassa alianza kubwaga moyo wake baada ya NEC kuridhia ombi la Kamati Kuu ya chama hicho (CC) kwamba suala la mageuzi ndani ya CCM maarufu kama kujivua gamba lirejeshwe katika kamati hiyo ili lifanyiwe kazi kwa taratibu za kawaida za kinidhamu baada ya wahusika kukataa kuachia nafasi zao.

“Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama wakinitukana, hivi hatukujua kwamba kuna kamati hizo za maadili,”Lowassa alinukuliwa akihoji.

Lowassa alinukuliwa akiwataja Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, John Chiligati kwamba wamekuwa wakitukana watu ovyo kwa fedha wanazopewa na CCM.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Lowassa alitumia dakika saba kumshambulia Nape kwamba amekuwa akifanya mambo nje ya utaratibu na kwamba mwenendo huo umekuwa ukikibomoa chama badala ya kukijenga.

Baada ya maneno ya Lowassa, Waziri Mkuu mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Sumaye alisimama na kuhoji sababu za chama hicho kunyamazia ukiukwaji wa taratibu ambao umekuwa ukifanywa na watendaji hao.

“Mwenyekiti huyu bwana (Lowassa) amesema kwamba amechafuliwa kwa miezi saba, sasa kama leo tunasema kwamba tunarudi kwenye utaratibu wa kamati za maadili, hao waliomchafua watafanywaje?”Sumaye alinukuliwa akihoji.
Hata hivyo, taarifa za ndani ya kikao hicho zilimnukuu Kikwete akisema kwamba viongozi hao watakuchukuliwa hatua za kinidhamu kama watakuwa wamefanya hivyo.
Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete aliwasihi wajumbe kuachana na suala hilo na badala yake kuchangia maeneo mengine ya taarifa hiyo ya hali ya siasa iliyowasilishwa na Katibu wa Siasa na Mambo ya Nje ya CCM, January Makamba.

November 24, 2011

GAMBA LAGOMA


UTEKELEZAJI wa mpango wa CCM uliolenga kuwashinikiza watuhumiwa wa ufisadi kuachia nafasi zao za uongozi ndani ya chama hicho, umechukua sura mpya na sasa Kamati Kuu (CC) inaomba ipewe kibali cha kuwachukulia hatua zaidi wale ambao wamegoma kujiuzulu.Juzi, katika kikao chake mjini hapa, CC iliazimia kuomba idhini ya Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM ili ifanye kazi hiyo baada ya kuwepo ukimya ambao unaashiria kutokuwepo viongozi na makada ambao wako tayari kujiuzulu nyadhifa zao kwa hiari.

Tangu kupitishwa kwa mpango huo maarufu kwa jina la kujivua gamba katika kikao cha NEC kilichopita cha Aprili mwaka huu, ni kada mmoja tu, Rostam Aziz aliyechukua hatua za kujiuzulu ubunge wa Jimbo la Igunga na ujumbe wa NEC, lakini wengine wamekuwa kimya hadi sasa.

Katika kikao cha Aprili NEC hiyo ya CCM ilipitisha maazimio 26 lakini kubwa ni lile lililokuwa likihimiza vita dhidi ya ufisadi kuendelea na kutoa mwito kwa watu wanaotajwa na jamii kuhusika na ufisadi ambao wako ndani ya chama kujitathmini kisha kuchukua hatua za kuachia madaraka waliyo nayo.

Sehemu ya mwisho ya azimio hilo inasomeka: “Wasipoachia madaraka chama kiwachukulie hatua mara moja.”

Mmoja wa wajumbe wa CC ambaye ameomba jina lake kuhifadhiwa alisema: “Tunawaomba NEC waturuhusu jambo hili tulifanyie kazi sisi (CC) na litafanyiwa kazi kupitia taratibu za kawaida za chama kwa kuzingatia kanuni na taratibu za maadili za chama hicho.”

Kubadilika kwa utaratibu wa kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi, kulipokewa kwa shangwe na wafuasi wa watuhumiwa hao ambao wanasema kulikuwa na ajenda ya siri, kubwa likiwa ni vita ya urais wa 2015.

Hata hivyo, kada mwingine ambaye yuko karibu wa vigogo wa chama hicho alisema: “Hivi sasa hali itakuwa mbaya zaidi kwa watuhumiwa, tunakokwenda si hiari tena itakuwa ni lazima ikiwa chama kitawapata na hatia.”

“Ujue azimio la kwanza lilikuwa na pande mbili, kwanza ni watuhumiwa hao kujipima wenyewe kisha kuchukua hatua, lakini pili ni upande wa chama, sasa ukomo wa upande wa kwanza ambao ni kuchukua hatua wenyewe umekwisha, sasa ni zamu ya upande wa pili ambao ni wa chama,” alisema kada huyo ambaye pia ni mshiriki wa vikao vya uamuzi ndani ya CCM.

SOURCE: Mwananchi

November 22, 2011

TAQWA ACCIDENT UPDATES: Picha za wanafunzi 6 wa UDSM waliofariki

Kassim Dadi - Tanzania

Josephine Kaleso  - Malawi 

Nshaija Muganyizi - Tanzania

Mubiru Patrick  - Uganda

Chimuka Hamajata  - Zambia

Chikondi Chasowa - Malawi

WANAFUNZI sita waliokuwa wakisoma Shahada ya Uzamili, Hisabati katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni miongoni mwa watu 18 waliokufa Jumamosi katika ajali ya basi la Taqwa lililogongana na lori mkoani Kagera.

 Kwa mujibu wa Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala, marehemu hao ni miongoni mwa wanafunzi 10 wa UDSM waliokuwa wakienda Kigali nchini Rwanda kwa ajili ya ziara ya kimasomo katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Kigali.

 Kwa mujibu wa taarifa ya Profesa Mukandala kwa vyombo vya habari, wanafunzi waliokuwa katika safari hiyo ni wa kimataifa waliokuwa wakisoma shahada ya uzamili kupitia Programu ya Hisabati katika Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki.
 Miongoni mwa waliokufa katika ajali hiyo, wawili ni raia wa Malawi, Watanzania wawili, Mganda na Mzambia.
 Watanzania waliokufa ni Nshaija Muganyizi, na Kassim Dadi, Wamalawi ni Chikondi Chasowa na Josephine Kaleso, Mganda ni Mubiru Patrick na Mzambia ni Chimuka Hamajata.
 

 Basi la Taqwa lenye namba za usajili T 635 ABC aina ya Nissan Diesel lililokuwa likitoka Dar es Salaam kwenda Bujumbura Burundi liligongana na lori la Kampuni ya Bakhresa lenye namba za usajili RAB 255ACT lililokuwa likitoka Ngara kwenda Dar es Salaam.

 Magari hayo yaligongana Jumamosi saa nne asubuhi katika eneo la Lusahunga wilayani Biharamulo.

Tutarajie nini toka WHITE HOUSE Dodoma?????

 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete wa pili kutoka kushoto akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM leo Novemba 21, 2-011 ukumbi wa 'White House' wa makao makuu ya chama hicho tawala mjini Dodoma. kulia katika picha na Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama na kutoka kushoto ni Rais Mstaafu William Benjamin Mkapa, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Rais Mstaafu wa Zanziba Aman Abeid Karume

Vikao vya juu vya Chama Cha Mapinduzi, CC na NEC vinaendelea mjini Dodoma china ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete, ambapo wengi wanatarajia uenda maaumuzi magumu na hasa ya kujivua gamba ama kuvuliwa Gamba yatatolewa.



Wakati akihahirisha NEC mwezi wa Aprili mwaka huu Rais Jakaya kikwete aliongea na vyombo vya habari na kunukuliwa akitoa kauli hii 

" Tumekubaliana hatua zetu mbili, ya kwanza kuwabana wa..wa.. waji..wawaamue kuwajibika, lakini wanapokataa tusicheleee kuwawajibisha" JK.


Haikuleza ni kina nani na wanapaswa kuwajibikaje, tusubiri tuone labda sasa tutawajua hao WANAOPASWA KUWAJIBIKA/KUWAJIBISHWA. 

November 21, 2011

MEJE 30, MRITHI WA TSHALA MUANA ALIYEAMUA KUPANDA JUKWAANI MTUPU!



 
Nilipoiona kwa mara ya kwanza picha ya mdada huyu akiwa mtupu jukwaani akikatika nilistuka kidogo, nikajiuluza inawezekanaje mtu apande kwenye stegi akitegemea umati wa watu utakuwepo asivae ile nguo ndogo na kisha afanye kusudi ili watu wajue kwamba hakuvaa chu**?

 Akili ya kwanza iliyonijia ni kuwa hii itakuwa vijiukumbi vyetu vya uswazi, kama uwanja wa fisi vile maana huko yanafanyika mengi kuliko ya kupanda stejini kuwaburudisha wanywaji wa Komoni, Wanzuki, Kimpumu nk, kuangalia vyema nikaona hapana, sivyo, hili gauni la bei kidogo, wale wa uswazi si rahisi kutinga hili, wenyewe wanaliita evening dress, ikabidi nitafiti zaidi.

 Niliweka post hapa kuoji inakuwaje wadada siku hizi wameamua kujidhalilisha hivi? ni maslahi au ni kitu gani? je wamelazimishwa na wamiliki wa bendi kwamba lazima mpande hivi ili kuvutia wateja? nikaoji tena kutakakumfahamu je huyu ni nani?

 Jibu la swali hilo ndilo lililoniacha kinywa wazi, ati huyu ni Mtarajiwa mrithi wa Miondoko ya Mutwashi toka kwa Tshala Muana! kweli huyu ndio anatarajiwa kuchukua mikoba ya Tshala Muana? sikuelewa haraka, nikaamua kufanya kautafiti kidogo.

 Nikaingia mitandaoni, nikakuta ni kweli, anajiita MEJE30, nikakuta naye ana album kadhaa mitandaoni, tena ni muimbaji mzuri tu, tena picha hili ilipigwa akiwa katika show Kampala 2009, sasa kwanini aliamua kuanika kitumbua chake hadharani akijua kuwa kuna kamera ambazo haziongopi? Je ni mbinu mpya aliyobuni ya kuvutia wateja? ili siku nyingine akija watu wajue wanapa mbili kwa moja? au pengine ilikuwa ni biashara ndani ya biashara?  

 Hiyo kama haitoshi nikakutana na kioja kingine, eti ametafuta mwanasheria na ata wafungulia mashtaka wapiga picha kwa kumvua Ch**, sasa hapa ikabidi niziangalia vyema picha zote kutoka katika show ile ambazo zimejaa mitandaoni, kwa utaalamu wangu wa kupiga picha na kuhariri kwenye duka la picha sijawai sikia kuwa kuna kamera inavua watu nguo, tena za ndani! hiki ni kioja kingine cha Malkia mtarajiwa wa Miondoko ya Mutwashi.

 Huyu ndie MEJE 30 Mrithi mtarajiwa wa Tshala Muana aliyeamua kupanda jukwaani bila nguo ya ndani ama kanguo kadogo na sasa analalama kuwa kamera zimemvua hako kanguo na kuanika kitumbua chake hadharani. Nabaki najiuliza, mbona Dada huyu ni mrembo, anasauti na kipaji pia kipo, kwanini afanye vile? ni nini anataka zaidi? 


November 20, 2011

TAQWA YATEKETEZA WANAHISABATI 6 WA UDSM

Moses Mwale (Zambian) mmoja wa Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam aliyesalimika  kati  ya kumi, watatu wamelaza Hospitali ya Ngara. 



  • Vifo vyafikia 18,
  • Wote watambuliwa,
  • Mtoto ahamishiwa Bugando


Ajali ya Basi la Taqwa na Lori la Azam iliyotokea jana Lusaunga wilaya ya Biharamulo imeteketeza wanafunzi 6  wa mwaka wa pili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliokuwa wakichukua Masters of Science in Mathematical Modelling, walikuwa wakienda Rwanda kwenye warsha ya Pure Mathematics.

Kwa mujibu wa Mratibu wa Kozi hiyo yenye wanafunzi toka mataifa mbalimbali katika UDSM Dk Wilson Manera Charles  alisema wanafunzi hao ni kati ya kumi ambao waliteuliwa kuwakilisha katika warsha hiyo ya wanahisabati inayofanyika kila mwaka, wannne wamejeruhiwa na wanaendelea na matibabu, aliongeza kuwa waliokufa ni Mzambia mmoja, Malawi 2, Mganda 1 na Watanzania 2.

Naye Mganga Mkuu wa Hospitali ya Biharamulo Dr Grasmus  Sebuyoya alisema vimeongezeka vifo 2 na kufikia jumla 18 na kuwa mpaka sasa maiti zote zimetambuliwa na nane kuchukuliwa na ndugu zao kwa maziko, mingine insaburi ndugu.

Pia aliongeza kuwa Mtoto mdogo wa kiumu anayekadiriwa kuwa na miaka miwili na nusu ambaye mama yake amefariki ajalini amehamishiwa hospitali ya Bugando Mwanza kwa matibabu zaidi.


Majeruhi walioko Biharamulo ni Tina Elisha, Rose Nula, Janet Kisanga, Moses Mwale, Joseph Bigilimana, Anicet Mrundi, Joseph Baltazary na Masalu Leonard.

Maiti zilizotambuliwa ni Abiba Juma, Faida Abdalah, Aziza Said, Andi Ibrahim, Chanda Congo, Nshaija Muganyizi na  Kasimu Dadi, wengine ni Erick Eliude, Chinuka Hamajata na Ndizeye Pili.  

Bunge wants, Luhanjo, Jairo Utouh taken to task






THE National Assembly on Saturday resolved that the government should take appropriate action against the Chief Secretary, Mr Phillemon Luhanjo, and the Controller and Auditor General, Mr Ludovick Utoh, following unlawful collection of money to finance endorsement of the Ministry of Energy and Minerals' annual budget.

 
The House has also resolved that the government should take disciplinary and legal action against the Minister for Energy and Minerals, Mr William Ngeleja, his Deputy Minister Mr Adam Malima and the Permanent Secretary for the Ministry of Energy and Minerals, Mr David Jairo, over similar offences.

 The resolutions followed a report by a Parliamentary Select Team that established that Mr Jairo collected the money contrary to the laws of land and government's regulations.

 Mr Jairo wrote letters to Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) requesting 50m/-, the Rural Energy Authority (REA) asking for 50m/-, TANESCO (40m/-) and EWURA (40m/-) for finalization of a budget process of the ministry.

 Three institutions contributed as requested except for EWURA who resorted to financing dinners at a total cost of 9,797,600/-. Presenting the report, the Chairman of the team, Eng. Ramo Matala Makani (Tunduru North-CCM), revealed that the ministry, through Mr Jairo's initiative collected 418,081,500/- posting it in the bank account of the Geological Survey of Tanzania (GST).

 Mr Makani revealed further that out of the amount, payment of 126,044,480/- were doubtful and therefore the National Assembly resolved that a forensic audit should be conducted to establish the validity of the payments.
 

The team questioned the rationale of such initiative considering the fact that the ministry had in June this year received 171,542,000/- from the Treasury as other charges. Available documents show that the ministry had 35,500,000/- for such purpose while requirements stood at 207,042,000/-.

 According to the report, available ministry's documents showed that 17,480m/- were paid on July 19, 2011 to African Dreams Conference Centre Ltd for food and entertainment for five consecutive days without supporting documents.

Source: Daily News

UPDATES: AJALI YA TAQWA - 16 WAFARIKI PAPO HAPO

Watu 16 wamefariki papo hapo na wengine 17 kujeruhiwa baada ya basi la Taqwa No T635 AVC lililokuwa likitokea Dar kuelekea Bujumbura kugongana uso kwa uso na lori la Azam No RAB 255 W eneo la Lusaunga, Wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera, 


Madereva ni miongoni mwa waliokufa, akiongoea na Bongo Pix kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Biharamulo Dr Michael Abila amethibitisha kupokea maiti 15 na majeruhi 12 huku majeruhi watano na maiti moja wakipokelewa katika Hospitali ya Ngara. 


Mongoni mwa waliofariki ni wanawake saba na wanaume 9 huku mtoto mdogo ambaye amepoteza mama yake katika ajali akijeruhiwa vibaya, pia miongoni mwa waliofariki walikuwepo watu watatu wa familia moja waliokuwa wakielekea harusini ambao miili yao ilichukuliwa jana. 


Majina ya marehemu na majeruhi yatapatikana muda si mrefu. 

November 19, 2011

NEWS ALERT: Ajari ya Basi la TAQWA na Lori la AZAM Watu zaidi ya 10 wafa papo hapo!!!!!!!!!!








Watu zaidi ya kumi wamekufa papo hapo huku wengine kedhaa wamejeruhiwa vibaya baada ya basi la Taqwa lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Bujumbura kugongana uso kwa uso na lori la mizigo la Azam eneo la Lusaunga, Biharamulo.

 Bongo Pix imeshuudia miili kumi ikishushwa kutoka katika Fuso no UAM 267 N ambalo lilichukua miili hiyo eneo la tukio, Uongozi wa hospitali ulilazimika kuita watumishi wote hata wale waliokuwa mapumzikoni kuja kuokoa jahazi kwani ni wazi huduma yao ilikjuwa yahitajika katika kipindi hiki.

 Taarifa zaidi za idadi rasmi ya majeruhi, walliofariki na majina yao tutaipata baadaye baada ya kuongea na mamlaka husika, RPC na Mganga Mkuu wa Hospitali.

 Bongo Pix inawapa pole waliofikwa na msiba huu, na zaidi kuwaombea waliojeruhiwa wapate matibabu na kurejea katika shughuri zao.Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi. 

Breaking Newzzzzzzzzzzzzzzz AJARI MBAYA BASI LA TAQWA

Taarifa zilizotufikia ni kuwa kumetokea ajari mbaya eneo la Lusaunga, Biharamulo iliyohusisha Basi la Taqwa toka Dar es Salaam na Lori la mizigo, kulinga na shuhuda wa ajari hiyo mbaya anasema wameona miili ipatayo 30 ikiwa imezagaa eneo la tukio, yahofiwa kuwa wengi wamekufa katika ajari hiyo. 




Majeruhi kadhaa wamefikishwa hospitali ya Biharamulo kwa matibabu na wengi wameumia sana. Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kadiri tutakapozipata, toka eneo la tukio na hospitalini.

JK - "NITASAINI SHERIA YA MCHAKATO WA KATIBA"



RAIS Jakaya Kikwete emesema licha ya kelele za wanasiasa, atasaini Sheria ya mchakato wa kuunda Katiba Mpya.

Alitoa kauli jana na kupangua hoja zote kupinga mchakato huo zilizotolewa na Chadema kwamba muswada huo haukuzingatia kanuni zitakazowezesha demokrasia.Kauli hiyo ya Rais imekuja saa chache baada ya Bunge kupitisha Muswada wa Mabadiliko ya Katiba ambao ulisusiwa na Wabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi kwa madai kuwa mchakato mzima una kasoro.

 Akizungumza na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa PTA, Sabasaba juu ya hali ya uchumi nchini na mchakato wa Katiba, Rais Kikwete alisema atatia saini sheria ya mchakato wa kuunda katiba mpya ambayo inatokana na muswada uliopitishwa na Bunge jana.

 Alikibebesha lawama nyingi Chadema kwa kile alichosema ni upotoshaji wa mchakato huo kwa lengo la kuuvuruga wakati unaendeshwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.
 

Alimtupia shutuma za waziwazi Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akisema amekuwa kigeugeu kwa sababu mwanzo alimsifu (Rais Kikwete), kwa kukubali Katiba kubadilishwa lakini baadaye akageuka na kuanza kumponda.

 “Mbowe ni miongoni mwa watu walionimwagia sifa baada ya kutangaza nia yangu ya kuanza kwa mchakato wa Katiba Mpya, nakumbuka ilikuwa Februari 11, mwaka huu wakati akichangia hotuba yangu katika Kikao cha Bunge alisema: ‘Tunampongeza Rais katika suala hili.’ Ila muda mfupi baadaye chama chake kikaja na mtizamo tofauti wa kunyang’anywa hoja yao… na kwamba Rais asiunde tume wala kuhusika katika mchakato.”

 Alisema alishangazwa na kauli za Chadema na kusema: “Hii si mara ya kwanza kwa nchi yetu kufanya zoezi la marekebisho ya Katiba na hata kuandika Katiba Mpya.”

 Alisema kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi, katika suala la upatikanaji wa Katiba anayeunda tume ni Rais na akisema hata katika utawala wa Awamu ya Kwanza na ya Pili, ilibadilishwa mara tatu na Rais ndiye aliyeunda tume.

 “Mwaka 1977 yalifanyika mabadiliko mengine ya Katiba ambayo yalitengeneza Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ilikuja kufanyiwa marekebisho makubwa mwaka 1984,” alisema Rais Kikwete.

 Mwaka 1991 na 1992, alisema iliundwa tume nyingine iliyoongozwa na Jaji Francis Nyalali ya kukusanya maoni ya Katiba ya kutoka mfumo wa chama kimoja kwenda vyama vingi.

 “Tume hii ilipendekeza sheria 40 zifutwe, zilifutwa na nyingine zinaendelea kufutwa ikiwemo sheria ya kumweka mtu kizuizini,” alisema.

 Alisema mwaka 1997 katika utawala wa Rais Benjamin Mkapa aliundwa Tume ya Jaji Kisanga ambayo ilikusanya maoni ya mabadiliko ya 13 na 14 ya Katiba.

 “Siku zote katika mchakato wa Katiba, tume huundwa na Rais, sasa iweje sasa?... Rais amepungukiwa sifa kikatiba?” alisema na kusisitiza kwamba ndiye mwenye mamlaka kikatiba kuunda kamati hiyo.

Alisema iwapo Chadema kitaandaa mchakato wake wa kuunda katiba itabidi mawazo yao wayakabidhi kwa kamati atakayoiunda.

 Alisema tayari CUF iliwasilisha rasimu yake ya Katiba na kuikabidhi serikalini na kwamba nayo itapelekwa kwenye kamati kama sehemu ya maoni yaliyotolewa na makundi ya Watanzania.
 Rais alisema uteuzi wa wajumbe katika tume utazingatia sifa na kwa mujibu wa kanuni akisema hana mamlaka ya kuichagua kwa kuzingatia vigezo vya urafiki.


SOURCE: Mwananchi

November 18, 2011

Biharamulo reportage kupitia ka-smart phone

Ma Bulkeria, Bibi pekee tuliyebakiw naye,, anawasalimu wadau woote wa Bongo Pix

Buseresere - Katoro, wenyeji wanapaita Buse, safari ya Kuelekea B'mulo inaendelea, hapa ni vi-hiace ,  Noah na Corola Station wagon aka Mchomoko ndo zinatamba 


Picha ya ukumbusho, cheki jicho la uba hilo, mwenyewe utapenda.

Mshikaki RUKSA 

Jamaa anavyokimbiza kibasi katika njia hizi utazani ni lami, vigari hivi vimezoea njia hizi kwenye lami havikimbii kabisa  sijui kunani hapa

November 14, 2011

The New Professional - N.W.M Taught at Universities in US | WINNERS Boulevard.

The New Professional - N.W.M Taught at Universities in US | WINNERS Boulevard.:

Constitution Confusion




The process to write a new constitution was thrown into confusion yesterday with many people rejecting the government’s decision to table the Constitutional Review Bill for the second reading.In his comments, the chairman for Jukwaa la Katiba (Constitution Platform), Mr Deus Kibamba, said MPs have an opportunity to safeguard the interests of Tanzanians irrespective of their political affiliation.He warned that if the Bill were tabled for the second reading, the Platform would lead a nationwide demonstration to protest the move.

 On top of this opposition from the Platform, members of the House of Representatives in Zanzibar have called for the shelving of the constitution writing process until people get the opportunity to debate and decide on the type of Union they want.

 However, many people who contributed on the Bill were apparently misguided in that they aired views on the kind of constitution they want instead of how the process to write a new constitution should be carried out.

 In Dodoma, the dean of School of Law at the University of Dar es Salaam, Prof Palamagamba Kabudi on Saturday pleaded with MPs not to be emotional during the discussions of the Bill so as to forestall violence and unnecessary misunderstandings.

 In Dar es Salaam, many people who contributed at the symposium organised by the Jukwaa la Katiba, urged the government to rescind its decision to table the Bill for the second reading.

 They also urged the MPs to reject the Bill if the government tables it for the second time. They wanted more people across the country to go through the Bill, which has been written afresh after the earlier version was rejected in April.
Jukwaa member Christina Kamili said that the Bill should not proceed to the second reading because it has many weaknesses.

 Ms Kamili noted that there wasn’t enough consultation with various crucial groups before the drafting of the Bill.
A professor from the University of Dar es Salaam, Josephat Kanywani, who represented the Interfaith Community, noted that what Tanzanians needed now was drastic changes in their lives that have been deteriorating since independence.

 “This (writing of new constitution) is an opportunity that has presented itself to Tanzanians and nobody should mess around with it... Laws are made to serve the people, not vice versa,” he said adding:
“We should not rush to have a constitution just for the sake of it, let us have a constitution which can work for Tanzanians.”

 A representative from the Trade Union Congress of Tanzania (Tucta) Mr Hezron Kaaya, wondered why the drafting of the Bill had sidelines the participation of the workers.

 “Let the current leaders note that times have changed. Many of voters are young people. In 2015, these youth will constitute a big voting The process to write a new constitution was thrown into confusion yesterday with many people rejecting the government’s decision to table the Constitutional Review Bill for the second reading.In his comments, the chairman for Jukwaa la Katiba (Constitution Platform), Mr Deus Kibamba, said MPs have an opportunity to safeguard the interests of Tanzanians irrespective of their political affiliation.He warned that if the Bill were tabled for the second reading, the Platform would lead a nationwide demonstration to protest the move.

 On top of this opposition from the Platform, members of the House of Representatives in Zanzibar have called for the shelving of the constitution writing process until people get the opportunity to debate and decide on the type of Union they want.

 However, many people who contributed on the Bill were apparently misguided in that they aired views on the kind of constitution they want instead of how the process to write a new constitution should be carried out.

 In Dodoma, the dean of School of Law at the University of Dar es Salaam, Prof Palamagamba Kabudi on Saturday pleaded with MPs not to be emotional during the discussions of the Bill so as to forestall violence and unnecessary misunderstandings.

 In Dar es Salaam, many people who contributed at the symposium organised by the Jukwaa la Katiba, urged the government to rescind its decision to table the Bill for the second reading.

 They also urged the MPs to reject the Bill if the government tables it for the second time. They wanted more people across the country to go through the Bill, which has been written afresh after the earlier version was rejected in April.
Jukwaa member Christina Kamili said that the Bill should not proceed to the second reading because it has many weaknesses.

 Ms Kamili noted that there wasn’t enough consultation with various crucial groups before the drafting of the Bill.
A professor from the University of Dar es Salaam, Josephat Kanywani, who represented the Interfaith Community, noted that what Tanzanians needed now was drastic changes in their lives that have been deteriorating since independence.

 “This (writing of new constitution) is an opportunity that has presented itself to Tanzanians and nobody should mess around with it... Laws are made to serve the people, not vice versa,” he said adding:
“We should not rush to have a constitution just for the sake of it, let us have a constitution which can work for Tanzanians.”
 A representative from the Trade Union Congress of Tanzania (Tucta) Mr Hezron Kaaya, wondered why the drafting of the Bill had sidelines the participation of the workers.
 “Let the current leaders note that times have changed. Many of voters are young people. In 2015, these youth will constitute a big voting bloc... Conservative leaders should beware of the changing trends,” he warned.
 He said those defending the current constitution are doing so because they benefit from it. It provides them with huge material benefits and protection upon their retirement, he charged.
 “We don’t expect them to crave for a new constitution which comes from the people. We don’t expect a minister to agree to a constitution which reduces hi powers,” he said.
He said workers should not agree with a constitution they had no say during its writing.bloc... Conservative leaders should beware of the changing trends,” he warned.
 He said those defending the current constitution are doing so because they benefit from it. It provides them with huge material benefits and protection upon their retirement, he charged.
 “We don’t expect them to crave for a new constitution which comes from the people. We don’t expect a minister to agree to a constitution which reduces hi powers,” he said.
He said workers should not agree with a constitution they had no say during its writing.

Read in CITIZEN

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...