MAKUBALIANO YA RAIS NA CHADEMA YALIVYOLIPOTIWA:
HABARI LEO: JK, CHADEMA MWAFAKA.
MUSWADAwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011
uliopitishwa na Bunge hivi
karibuni utasainiwa na Rais Jakaya Kikwete kama
ilivyopangwa.
Hali hiyo inatokana na makubaliano yaliyofikiwa jana kati ya
Rais na Kamati ndogo ya Chadema iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho
Freeman Mbowe.
Juzi na jana, pande hizo mbili zilikuwa na mazungumzo kuhusu
Muswada huo ambao ulipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila
ushiriki wa wabunge wa Chadema na wa NCCR-Mageuzi ambao walisusia.
Kususia mjadala wa Muswada huo kwa wabunge hao wa vyama
hivyo, ulitokana na madai yao
ya kutaka Muswada huo usomwe mara ya kwanza bungeni wakidai haukuwa umesomwa na
wananchi na kuuelewa, hivyo kukosa kuuchangia, lakini walikataliwa na Spika
Anne Makinda.
Kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa jana Ikulu Dar es
Salaam na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi na
Kaimu Katibu Mkuu Chadema, John Mnyika, kutakuwa na haja ya sheria hiyo baada
ya kusainiwa kuendelea kuboreshwa, ili ikidhi mahitaji ya kujenga na kuaminiana
na mwafaka wa kitaifa.
Pia kutakuwa na mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara
kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la
kudumisha mwafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba mpya.
Awali ilielezwa kuwa mazungumzo hayo yalifanyika katika
mazingira ya uelewano ambapo Rais Kikwete aliwahakikishia Chadema kuwa yeye na
Serikali yake wana dhamira ya kuhakikisha Tanzania inapata Katiba mpya.
Kulingana na hatua iliyofikiwa jana, Rais atasaini Muswada
huo kuwa sheria ambayo inatarajia kuanza kutumika Desemba mosi, lakini wakati
ikiendelea kutumika, kutakuwa na fursa ya kuifanyia marekebisho endapo haja
itajitokeza.
Hili si jambo jipya kwa masuala ya uandishi wa Katiba mpya,
kwani hata ya Kenya
ilipitishwa na mpaka sasa zipo taarifa kuwa imeshafanyiwa marekebisho mara 11
kutokana na mahitaji yanayoibuka kwa kuzingatia mazingira na muktadha.
Makubaliano ya jana, yanamaliza sintofahamu iliyokuwa
imeanza kuibuka kwa Chadema na makundi mengine kutaka kufanya maandamano nchi
nzima, kupinga Muswada huo kusainiwa na kushinikiza urejeshwe bungeni kusomwa
kwa mara ya kwanza.
Lakini pia kunatoa fursa pana kwa wawakilishi na wabunge
kurudi kwa wananchi kuwahimiza kujitokeza kutoa maoni na mawazo yao kuhusu aina ya Katiba
inayotakiwa na Watanzania wote.
MWANANCHI - JK, CHADEMA WAKUBALIANA KUBORESHA MUAFAKA.
RAIS Jakaya Kikwete na viongozi wa Chadema wakiongozwa na
mwenyekiti wao, Freeman Mbowe wamekubaliana kwamba ipo haja ya kuendelea
kuuboresha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 ili ukidhi
mahitaji ya kuaminiana na mwafaka wa kitaifa.Pia, wamekubaliana yawepo
mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau
mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha mwafaka wa
kitaifa kwenye mchakato wa Katiba Mpya.
Makubaliano hayo yamefikiwa jana na kusainiwa na Kaimu
Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Emmanuel Nchimbi baada ya kumalizika kwa mkutano wa siku mbili baina
ya pande hizo mbili kuhusu muswada huo.
Katika kikao cha jana Mbowe aliongozana na wajumbe wa kamati
hiyo Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara) Said Arfi na Makamu Mwenyekiti
(Zanzibar) Said Issa Mohamed, Mshauri wa Masuala ya Siasa wa chama hicho,
Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Mnadhimu wa Kambi ya
Upinzani bungeni, Tundu Lissu na John Mrema.
Katibu Mkuu Dk Willibrod Slaa ambaye ni mjumbe hakuwapo
katika kikao cha juzi na cha jana na taarifa zilizopatikana baadaye na
kuthibitishwa na yeye mwenyewe ni kwamba alikuwa safarini kwenda kuhudhuria
kesi yake mahakamani Arusha jana.
Kabrasha lililokabidhiwa na ujumbe wa Chadema kwa Rais
Kikwete lilikuwa lina waraka uliotoa mapendekezo mbalimbali ya kurekebisha
muswada huo huku wakitaka sheria iweke wazi kwamba Rais hana mamlaka yoyote juu
ya Bunge Maalum la Katiba zaidi ya mamlaka ya kuliitisha kwa mara ya kwanza na
kwamba mamlaka ya Bunge hilo yataisha mara baada ya kupitishwa kwa Katiba Mpya
katika Bunge Maalum la Katiba.
Wametaka ifanyike hivyo kwa kuwa sheria hiyo inampa Rais
mamlaka juu ya Bunge Maalum la Katiba wakati Bunge hilo linatakiwa kuwa chombo huru na chenye
mamlaka ya juu kuliko mamlaka nyingine zozote katika nchi.
Katika waraka wao, Chadema wameeleza kutaka vifungu vyote
vinavyokiuka haki za kimsingi za kikatiba vifutwe na kuwapo na uhuru kamili wa
kujadili, kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi juu ya utungaji wa Katiba
Mpya hata kama itakuwa kinyume na matakwa ya
Tume ya Katiba na masharti ya Sheria hiyo.
Katika ukusanyaji na uratibu wa maoni ya wananchi juu ya
Katiba Mpya na masuala ya muungano wametaka ziundwe tume mbili za katiba, moja
itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya kwa ajili ya
masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanganyika na ya pili
itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi juu ya masuala ya Muungano.
THE CITIZEN – JK, CHADEMA Talks: The Way forward
The government and the opposition Chadema party have agreed
in principle that the newly passed Constitutional review Act 2011 bill needs
major amendments.
A joint statement issued yesterday by the two sides at the end
of two days of consultations, said that
the bill should be improved so as to bring
it to the requirements of building a national consensus as well as
cohesion. The one page statement signed by the minister for Information, Youth,
Culture and Sports, Dr Emmanuel Nchimbi, on behalf of the government and
Chadema Director for Foreign Affairs and International relations, Mr John
Mnyika, notes also that the talks were conducted in a cordial atmosphere.
The two sides also agreed in the closed door talks that
there was a need for the government and
other stakeholders to hold constant
meetings and consultations, for the purpose of building and
strengthening national consensus during the process of crafting a new
Constitution.
The agreement has brought the two sides at the middle
ground. The Chadema team, which was led by its national chairman, Mr Freeman
Mbowe, went into the talks with a strong
proposal that President Kikwete should not sign the new Bill into law.
On the other hand, the government believed that the bill was
perfect and President Kikwete indicated that he would endorse it despite sentiments from Chadema
and a number of activists under the banner of Tanzania Constitution Forum
(TCF).
President Kikwete, his government and the Parliament,
insisted that the Bill has no flaws as it followed all legal processes and procedures during its
processing before it was passed by the Parliament more than a week ago.
Chadema MPs boycotted the debate on the Bill in Parliament
in protest over claims that the authorities did not give common Tanzanians
an opportunity to widely discuss one of
“the most important pieces of legislation to have been drafted in the last 50
years.”
And the thrust of the
Chadema message to President Kikwete and his team during the talks centred on
rejecting the Bill, asking that it should not be assented, and its processing
start afresh.
In their letter to the President, a copy of which was seen
by The Citizen, the opposition party pleaded with the Head of State not to assent the Bill so
as to give time for wananchi to air their views on it. They also argued that
there is a need for wananchi to be educated about the Bill as experience has
shown that most people believe that what was passed was a new Constitution.
Chadema said there was a need to first amend the current constitution in order
to align it with prevailing conditions, in order to have a level playing field
between the two sides of the Union during the
writing of a new Constitution.
DAILY NEWS - Kikwete, Chadema reach consensus
PRESIDENT Jakaya Kikwete will soon sign into law the
Constitutional Review Bill following a two-day meeting with a delegation from
the opposition Chadema that apparently held different views.
This means that the review process will start anytime from
now, putting to an end heated debate and forums on the same that recently
dominated the country’s political scene.
A press statement signed by the Minister for Information,
Culture and Youth, Mr Emmanuel Nchimbi, and Chadema Acting Secretary General
John Mnyika reiterated that the meeting was conducted in a friendly atmosphere.
The five-hour long meeting that started from 10am at the
State House in Dar es Salaam on Monday, concluded that despite the Bill being
passed by Parliament, it would be amended if and when necessary for it to win
public trust and national consensus.
The two parties also underscored the need for frequent
communications and cooperation between the government and other stakeholders on
improving the law to maintain national consensus during the constitutional
review process.
The CHADEMA delegation was led by the party’s National
Chairman, Mr Freeman Mbowe. On Sunday, President Kikwete received
recommendations on constitution review from CHADEMA. Both parties agreed that the
process should adhere to the interest of the nation much as it should also
refrain from dividing the public according to their religion, tribe and region.
Last week, CHADEMA sought the president’s audience over the
constitutional review Bill after their bid to stop a second tabling of the
constitutional review Bill in parliament by staging a walk-out failed.
Demonstrations planned by activists scheduled for Saturday
to press President Kikwete not to sign into law the constitutional review Act
were banned by police for fear that they would escalate into chaos.
My take:
Hizo YELLOW, sijaelewa sawasawa, labda wataalamu wanaweza kunisaidia, mnisamehe kwa kutokuelewa kwangu muafaka huu hasa kutokana na nukuu hizo.