September 14, 2011

Miaka 5 sasa.


Miaka mitano ni michache sana kwa mwanadamu, ni umri ambao mtoto kama atakuwa ameenda vyema basi atakuwa chekechea ambapo atatarajia kukaa ama mwaka au miaka miwili kabla ya kwenda shule ya msingi, huyu ni mtoto bado, lakini kwa Shirika, kampuni, biashara, na hata blog si umri mdogo huo, ni mkubwa.

 Ni umri mkubwa kwa bloga kama ilivyo kwa kampuni, Shirika, ama nchi, ingekuwa ni urais iki ni kipindi ambacho ama rais anamaliza muhula wa kwanza au wapili na hivyo kuhitaji ufanyike uchaguzi ili apatikane mwingine, hivyo si muda mchache hata kidogo.

 
Kwa blog kufika muda huu ikiwa hai na bado iko ewani si kazi ndogo, ebu fikiria ni vitufe (keyboards) ngapi zimegingwa na pengine kuharibika katika juhudi za bloga kurusha ewani kile atakacho wadau wakisome? au ni sikirini ngapi zimemmulika bloga na pengine kutaka kumpofusha ili mradi tu wadau wapate kinachoendela?, au labda ni viti vingapi amekalia, vibanda vingapi (vyaitwa @ café) ameingia na pengine kulazimika kukaa kusubiri muda wake ama kugombana na wahusika kwa kumruka katika foleni ilimradi tu aingie mtandaoni na kuweka blogini kile alicho nacho? je alipotishiwa kufukuzwa kibarua, kisa! kuwajuza wadau.

 Utatambua kuwa si muda mchache hata kidogo, ni mwingi wa kutosha, Bongo Pix Blog kama zilivyo blog nyingine pia imepitia hayo na mengi zaidi ya hayo, lakini ilivuka na sasa inatimiza miaka mitano, shukurani za pekee ziwaendee wadau wote kote ulimwenguni, kwani BPB ina wadau katika mabara yote matano, kinara ikiwa ni Africa, Amerika, Ulaya na Asia.

 Si rahisi kumtaja kila mdau, lakini itoshe kusema kuwa BPB inawashukuru sana nyote, wapo ambao wamekuwa wakichangia, asanteni sana, wapo pia waliokuwa wanapiga simu kutaka kujua kulikoni pale tunapokuwa tumetingwa, nao pia nasema asante, lakini wapo ambao piga uwa lazima wapiti blogini kila siku kuona na kusoma kilichorushwa humo nao nawashukuru lakini shukurani za pekee kwa wewe uliyeamua kuifanya BPB kama favourite yako au home page, wewe ubarikiwe sana.

 Miaka mitano ijayo (panapo majariwa ya Muumba) kutakuwa na mabadiliko makubwa sana, endelea kuitembelea utajionea.
 Asanteni sana Nyote, Bernard Rwebangira,  

Miaka 5 ya Kublog


Miaka mitano iliyopita mwezi kama huu na tarehe kama Bongo Pix Blog ilizaliwa, post ya kwanza iliwekwa katika blog, hayakuwa maamuzi mepesi kuanza ku-blog katika mazingira ya wakati ule, wengi walikuwa wakiogopa hata kusikia, wakiichukulia kwa mtizamo hasi zaidi, bila shaka, ni hurka ya binadamu, kutokubali kwa urahisi jambo lolote jipya, hasa liwajialo tofauti na mazoea yao.

 Ilikuwa ngumu, wengi walikuwa wakituangalia kama watu wa ajabu kuwa na blog au globu (msemo wa gwiji la kublog nchini Ankal Michuzi), japo BPB ilianzishwa kwa kujifunza (self taught) lakini ilitokana na hamasa toka kwa blogaz kadhaa ambao walishatangulia katika fani kama Ndesanjo Macha, Isaa Michuzi na pia jukwaa la Jamii Forums wakati huo likijulikana kama Jambo Forums.

 Nikiangalia tulipo sasa sina shaka kukiri kuwa tumepiga hatua kubwa katika nyanja hii ya mitandao ya kijamii, hivi sasa watu wengi zaidi wameanzisha na kuendesha blogs, pia wapo wanaoendesha maisha yao kupitia blogs, yaani ni kama kina Murdoch au Mengi wadogo, wanamiliki vyombo vyao vya habari, mashirika makubwa na kampuni kadhaa zina viunganishi vya blogs katika wavuti zao, hii ni hatua kubwa.

 Jambo ambalo sikujua wakati ule naanza ku-blog ni kuwa huu ni kama ulevi vile, kila unapokaa wahisi kuandika ama kuhabarisha watu, kujuza ulimwengu juu ya yale yanayokuzunguka, wahabarisha watu ambao hamuonani, kuna wakati nilikuwa namaliza siku mbili au tatu sijapost kitu, najikuta napata comment au email, kuhoji kimya changu au kutaka kujua jambo fulani, ndipo wajua kumbe kuna watu wanakusoma mahali fulani. 

Katika kutimiza miaka mitano BPB ina mikakati kadhaa, mojawapo ni kufanya kile ambacho kilifanya kuanzishwa kwayo, UPASHANAJI HABARI KWA NJIA YA PICHA ZAIDI, hili lilikuwa lengo kuu la kuanzishwa kwake, picha ambazo mwisho wa siku zitaleta mabadiliko chanya katika jamii yetu, picha zina nguvu sana katika kuhabarisha na kuleta mjadala ambao mwisho wa siku ni mabadiliko chanya katika jamii.

 Toka kuvumbuliwa kwa fani hii ya picha dunia imeshuhudia mabadiliko mengi yaliyotokana na watu kuona picha na hivyo kuoji na kujadili na hatimaye kufikia makubaliano kuwa inabidi lifanyike jambo fulani kubadili hali husika, kwani picha si tu kwamba inaongea maneno 1000 bali inamfanya msomaji kuona uhalisia jambo kama yuko hapo kuliko maandishi ama sauti. Yapo mambo mengi sana katika jamii zetu (mazuri na mabaya, ya kuigwa na kukemewa) yanayo paswa kumulikwa hili yajulikane na kisha hatua fulani zichukuliwe, BPB katika miaka mitano ijayo itajikita katika jukumu hilo zaidi.

 
 Bongo Pix Blog

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...