April 10, 2009
Michelle Obama lipi kosa lake hapa??
HATI MALKIA WA UINGEREZA UWA HAGUSWI NA AWEYE YOTE YULE!!!
Kitendo cha US First Lady kupeana mikono na Malkia Elizaberth bila Queen kuvaa glovu na hatimaye kukumbatiana hivi karibuni kimezua mjadala ambao nadhani hauna maana yoyote kwa waingereza huko UK.
People are supposed to curtsey and not hug the Queen , yet Michelle Obama did both and got away with it. No one ever does it, it is remarkable she was able to get away with it without the intervention of the ladies in waiting and other hangers on around Queen Elisabet II. blogger
Less than 24 hours after her protocol-breaking hug of Queen Elizabeth, Michelle Obama pulled up in front of the Elizabeth Garrett Anderson school for a surprise visit.
On her way to the school, her motorcade passed newsstands teeming with reports about The Hug.
The Daily Mail, for one, called it "an electrifying moment of palpable majesté: A breach of centuries-long protocol ..."
While generally approving, reports noted that protocol "has been set in stone for generations. 'Whatever you do,' courtiers are apt to warn, 'don't touch the queen.'" Pata zaidi hapa
Msemaji wa Kasri asemaje?
A Buckingham Palace spokesman who asked not to be identified because of palace policy said he could not remember the last time the queen had displayed such public affection with a first lady or dignitary.
"It was a mutual and spontaneous display of affection," he said. "We don't issue instructions on not touching the queen."
NYERERE, AMINI WAKUTANA
WATOTO wawili wa viongozi wa zamani wa Uganda na Tanzania jana waliandika historia mpya baada ya kukutana kwenye kijiji cha Butiama alikozaliwa na kuzikwa Rais Julius Nyerere na kukubaliana kuanza umoja mpya.
Watoto hao, Madaraka Nyerere na Jaffar Amin, ambao baba zao walionekana kuwa mahasimu wakubwa katika vita vya mwaka 1978 baina ya nchi hizo mbili, walionyesha kusikitikia vita hiyo, huku mtoto wa Idd Amin wa Uganda akisema "ilisababisha maafa makubwa" kwa wananchi wa Tanzania na Uganda.
"Vita ile ilisababisha maafa makubwa kwa wananchi," alisema Jaffar akionekana kusikitikia kitendo cha baba yake ambaye alikuwa chanzo cha vita hiyo kwa kuishambulia Tanzania kabla ya Nyerere kuamua kujibu mapigo kwa kuiondoa serikali yake madarakani.
"(Nyerere) ametuonyesha umoja, huyu ni bingwa wa suala hili. Mimi sijui kabila lolote hapa Tanzania. Najua nyinyi wote ni Waswahili, lakini kule kwetu wakiona wewe ni mrefu watasema ni kabila fulani, wakiona mweupe kidogo, mwembamba watasema wewe ni Mnyankole.
"Lakini tangu wanajeshi wenu walipokuja kwetu, mnamwita kila mtu Mganda."
Jaffar, ambaye alikuwa akizungumza lugha ya Kiswahili, akiwa amevalia kanzu ya bluu likiwa kama vazi la mitindo ya nchi za Afrika magharibi, alitaka mkutano huo, ulioandaliwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), baina yake na Madaraka uwe mwanzo wa mshikamano baina ya wananchi wa Tanzania na Uganda.
Mtoto huyo wa Idd Amin alienda kwenye kaburi alilozikwa Nyerere na pia kutoa zawadi ya mkeka kwa mke wa muasisi huyo wa taifa la Tanzania, Mama Maria Nyerere.
Naye Madaraka alisifu mkutano huo akisema umeongeza nia ya kuleta umoja.
Vita huyo ilidumu kwa miezi kadhaa na kufuatiwa na hali ngumu ya kiuchumi kwenye nchi zote mbili, Tanzania ikitangaza kujifunga mkanda kwa miezi 18 huku Uganda ikifuatiwa na mapinduzi mfululizo yaliyofikia ukomo mwaka 1986 wakati Rais Yoweri Museveni alipoingia Ikulu akitokea msituni.
Source: Mwananchi
Subscribe to:
Posts (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
The Himba are an ethnic group of about 20,000 to 50,000 people living in northern Namibia, in the Kunene region (formerly K...
-
Mineral occurrence in Tanzania by TMAA UONGEZAJI WA PATO LA MTANZANIA Mheshimiwa Spika, 46. Lengo la Dir...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...