Kila kuchapo bongodaslam kuna mengi ya kustaajabisha na kusikitisha tena toka kwa watu wenye dhamana kubwa ya uongozi wa nchi hii, Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Filauni....... Hivi tuseme kweli tu, hawa waheshimiwa walipokuwa wakiendaomba kuwekewa maji haya walienda ka akina siye pangu pakavu kweli? au wengine walienda ama na bendera zinapepea ktk mashangingi yao na wengine na bastola mkononi kama wanavyojulikana. all in all ni kuwa huduma hii lazima ilipiwe, najiuliza ni mangapi au huduma ngapi wanayokwepa kulipa? je hawa wanalipa kweli kodi zote za nchi hii? Na iwapo uongozi ni mfano au kuonyesha njia wengine wafuate, je "kiongozi" mtawala wa namna hii anataka wananchi tumfuate kwa yepi hasa? anayotenda au anayosema? inasikitisha kuona watu mwenye dhamana au mawaziri kama hawa ndio wanashindwa au kukataa kulipia huduma ambayo wanaitumia hata kunnyeshea bustani zao za maua wakati wakazi wa maeneo ya walalahoi hawapati hata ya kunywa tu. Hivi hii si kashfa tosha ya kumfanya kiongozi kuachia wadhifa wake? mi sijui ni nini uadilifu la maanisha lakini kwa vyovyote vile ni msamiati uliopiga chenga viongozi wetu halipatikani katika kamusi za viongozi hawa any way sina hakika kama tuna VIONGOZI AU WATAWALA AU PENGINE NI WAFALME WA HIYARI? sina hakika naomba mnisaidie.
Nyoka uzaa nyoka! mwana kama aiba je sikaona kwa baba kwanza?