November 28, 2008

Yona, Mramba warudi tena Keko

Wh. Basil Mramba na Daniel Yona wataendelea kusota tena rumande hadi Jumatatu pamoja na mahakama kuu kuwalegezea masharti ya dhamana.

Mahakama kuu katika uamuzi wake wa jana, ililegeza sharti la kuwataka washitakiwa hao kutoa fedha taslimu, badala yake ikawapa mbadala wa kuwasilisha hati za mali yenye thamani ya Sh bilioni 2.9 kila mmoja.

Uamuzi wa kuwataka washitakiwa waweke fedha taslimu ulitolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Hakimu Hezron Mwankenja. Lakini sharti hilo lililegezwa jana na mahakama hiyo ya juu.

Uamuzi huo wa Jaji Njegafibile Mwaikugile licha ya ulipokewa kwa furaha na ndugu wa washitakiwa, haukuwasaidia sana kutokana na hati walizokuwa nazo kuonekana kuwa na dosari kadhaa ambazo zilihitaji uthibitisho kutoka kwa mamlaka zingine.

Mama Maria apata ugeni leo

Waziri Mkuu wa Msumbiji Luisa Diogo akimvisha zawadi ya nguo aina ya kikoi Mama Maria Nyerere wakati alipomtembelea nyumbani kwake Msasani Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumjulia hali na kutembelea bustani yake.
Ni wageni wachache sana wanaomkumbuka Mama Maria hata kumtembelea, kwa Mama Maria au mama wa Taifa kuna mengi sana ya kujifunza budi tuwe twamtembelea jamani.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...