December 31, 2009

Ondoka, Uangaze kwa maana nuru yako......2010

Kuanza na hatimaye kuumaliza mwaka ni neema ya MUNGU, hakika sisi binadamu hatuna cha kujivunia hapo, sote twajua na hata mzee wetu Simba wa Vita alipenda bila shaka kuuona mwaka 2010 lakini Bwana amempenda zaidi na hivyo amemuita kwake siku ya mwisho kabisa ya mwaka.
Kwa namna ya pekee napenda kuchuka nafasi hii kuwashukuru wadau wote ambao mmesafiri nami katika blogu kwa mwaka 2009, kabla ya kuwatakia heri ya mwaka mpya naomba kwanza kuwaomba msamaha wale wote ambao kwa namna moja ama nyingine niliwakosea ama kuwakwaza ktk jambo lolote lile, sisi ni binadamu na katika ubinadamu wetu hatukukamilika hivyo kukwaruzana hapa na pale ni vitu vya kawaida kabisa kwa kujua ama kutojua, jambo la msingi mara utambuapo umemkwaza mtu basi ni kuomba msamaha, nami pia nawasamehe wote ambao walinikwaza na zaidi na waombea pia.
KWA UPENDO MKUU NAWATAKIA WASOMAJI WANGU WOOOOOOTE HERI YA MWAKA MPYA WA NEEMA NA MAFANIKIO WA 2010,
Naomba kuwapa neno hili la kinabii toka kwa Nabii wa Mungu Isaya lituongoze mwwaka huu 2010. Naamini Neno hili litafanyika baraka kwetu sote bila kujali dhehebu au dini.
1 "Arise, shine, for your light has come, and the glory of the LORD rises upon you.

2 See, darkness covers the earth and thick darkness is over the peoples, but the LORD rises upon you and his glory appears over you.

Isaiah 60:1-22

Maombolezo ya Kitaifa siku saba

Rais Jakaya Kikwete ametangaza Maombolezo ya Kiataifa ya siku saba kufuatia kifo cha Waziri Mkuu msataafu Mzee Rashid Mfaume Kawawa ambapo bendera bendera zote zitapepea nusu mlingoti.
Mipango wa mazishi wa mpendwa Mzee wetu bado inaendelea na taarifa zitatolewa muda si mrefu.

Neno la leo

“This is what the LORD says— he who made a way through the sea, a path through the mighty waters, "Forget the former things; do not dwell on the past. See, I am doing a new thing! Now it springs up; do you not perceive it? I am making a way in the desert and streams in the wasteland.”- Isaiah 43:16, 18-19

Simba wa Vita hatunaye tena.

Taarifa zilizotufikia ni kuwa Waziri Mkuu Mstaafu al maarufu Simba wa Vita amefariki leo asubui ktk Hospitali ya Muhimbili alikolazwa jana baada ya kuzidiwa, viongozi mbalimbali walipata nafasi ya kumtembelea jana hiyo wakiongozwa na Rais JK na Mama Salma. Mungu ilaze Roho ya marehemu mahala pema peponi.
Wasifu wa Mzee Kawawa:
Mzee Kawawa alizaliwa tarehe 27 mwezi Mei 1926 ktk Kijiji cha Matepwende, Songea, Mkoani Ruvuma. Alikuwa Waziri Mkuu wa Pili wa Tanganyika 1962 baada ya Mwalimu Nyerere na Waziri Mkuu wa Kwanza wa Tanzania 1972 - 77, akifuatiwa na marehemu Sokoine.
soma wasifu hapa
Mr. Kawawa was born on 27th May, 1926 in Matepwende, Songea Ruvuma Region. He was the 2nd Prime Minister of Tanganyika (1962) and the 1st Prime Minister of Tanzania (1972-77). He was preceded by Mwl. Nyerere and succeded by Mr. Sokoine. Kawawa was the effective ruler of the country from January to December 1972 while Julius Nyerere toured the countryside. Kawawa was a strong advocate of economic statism. Kawawa remains a behind-the-scenes influence on the Tanzanian political process.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...