Afisa
Mawasiliano wa Airtel Tanzania Bi. Dangio
Kaniki akikabidhi mfano wa hundi kwa mshindi wa promosheni ya KWANJUKA Padri Isaya
Gowa wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mahenge wakati wa droo ya mwisho ya promosheni
hiyo iliyofanyika katika ofisi za Airtel jijini Dar es salaam, Katikati ni Meneja
Uhusiano Jackson Mmbando
September 19, 2011
Mtoto wa Mkulima at Mwitongo
Waziri mkuu Mizengo Pinda akiwa na Mama Maria Nyerere mara baada ya kufika kijijini Mwitongo, WM yuko ziara ya kikazi Mkoani Mara.
Igunga kumekucha, Mabalozi CCM wanaswa wakiandikisha wapiga kura.
WAKATI joto la uchaguzi mdogo wa Jimbo a Igunga likiendelea kupanda, Chama cha Wananchi (CUF) kimekituhumu CCM kuwa kimeanza kukusanya na kuorodhesha kadi za wapiga kura na kwamba, kimemkamata mmoja wa mabalozi wa nyumba kumi wa CCM wakati akifanya kazi hiyo.
Tuhuma hizo dhidi ya CCM zilitolewa jana na mgombea wa CUF, Leopold Mahona, ambazo tayari zimeshapingwa na Mratibu wa Kampeni wa CCM, Mwigulu Nchemba.
Akiwa katika kijiji cha Imalilo, Kata ya Nguru, jimboni humo, Mahona alisema kazi kuorodhesha majina ya wapiga kura na kadi zao inaratibiwa na kusimamiwa na wajumbe wa nyumba kumi wa CCM.
Mahona aliwataka wakazi wa kijiji hicho kukataa mpango huo kwa kutotoa vitambulisho vyao vya kupigia kura, kwani wakikubali kufanya hivyo watashindwa kuchagua mwakilishi mwenye uwezo wa kuwasaidia.
Kauli ya Mahona imekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahimu Lipumba, kuwataka wakazi Igunga kujiandaa kukabiliana na hujuma zinazotarajiwa kufanywa na CCM kwa lengo la kulazimisha ushindi, kutokana na chama hicho kupoteza mvuto kwa wananchi.
"Wakija kuwaomba shahada kataeni, hata wakiwatisha msikubali, mkae kimya na msiwafanye chochote. Subirini siku ya kupiga kura na mnichague mimi nikaletee maendeleo,’’ alisema Mahona.
Mahona alidai kuwa, wajumbe hao wanawatisha wakazi wa jimbo hilo wanaounga mkono upinzani na kulaani kuwa, kitendo hicho kinakwamisha maendeleo na juhudi za mabadiliko ya kidemokrasia.
Hujuma sehemu mbalimbali
Wakati mgombea huyo wa CUF akilalamikia kitendo hicho, mwandishi wa habari hizi imeshuhudia tukio la uandikishaji kadi hizo ukiendelea katika maeneo mbalimbali.
Mwandishi alishuhudia kijana mmoja, mkazi wa kata ya Iborogero, nje kidogo ya mji wa Igunga akiorodhesha majina ya wenye vitambulisho vya mpiga kura pamoja na namba za vitambulisho vyao vya mpigakura.
Kijana huyo alipoulizwa na Mwananchi, huku akisita kutaja jina lake, alisema kazi hiyo amepewa na wakubwa wake ambao alikataa kuwataja na kusisitiza kuwa, anachofanya ni kuorodhesha majina ya wapiga kura na vitambulisho vyao kupigia kura kisha kuviwasilisha kwa wakubwa.
‘’Mimi kazi yangu kukusanya taarifa za watu wenye vitambulisho vya mpigakura. Ninaandika majina yao pamoja na namba ya kitambulisho nawasilisha kwa wakubwa, wao watatoa maelekezo na hatua za kuchukua,’’ alisema kijana huyo.
Mmoja watu waliotoa kadi zao, Chiristina Kaloli, mkazi wa Iborogero alipoulizwa na gazeti hili alikiri kuwa, kadi yake imeishaandikishwa mjumbe wa CCM huku kusisitiza kuwa hiki ni kipindi cha mavuno kwao.
Kadi hiyo ambayo mwananchi iliona kumbukumbu zake Ikiwa na namba 05262605 inaonyesha kuwa, ‘Chritina Kaloli alijiandikisha kuwa mpiga kura Desemba 26, 2004 katika Shule ya Msingi Mpogoro, Wilaya ya Igunga’.
CCM wakanusha
Mratibu wa kampeni wa CCM, Nchemba alipoulizwa juu ya tuhuma hizo alisema ni kitu kisichoweza kufanywa na CCM.
"Hivyo vyama vingine vinatapatapa, sisi ndio wenye wanachama wengi Igunga, tukifanya hivyo tutakuwa tunapunguza wapiga kura wetu, hatuwezi kufanya hivyo bali wao,’’ alisema.
Alisema kitambulisho ni mali ya mwenye nacho na kwa mujibu wa sheria za nchi, hakuna mtu anayeruhusiwa kuchukua kitambulisho cha mtu mwingine.
Nchemba alisisitiza kuwa, suala la kukusanya vitambulisho vya wapiga kura linaw....ifuate hapa.
JK awasili New York.
JK akisalimiana na Maura Mwingira, mmoja ya maafisa ubalozini. |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete Jumapili amewasili New York, Marekani kuhudhuria Kikao cha 66
cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) na kushiriki katika mikutano mingine
ya viongozi wa nchi na Serikali yenye maslahi kwa Tanzania na Afrika.
Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, Mheshimiwa Rais Kikwete
asubuhi ya leo, Jumatatu, Septemba
19, 2011, atashiriki mkutano wa ufunguzi wa UNGA wa viongozi wa nchi na
Serikali utakaojadili “Jinsi ya Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa Yasiyokuwa ya
Kuambukiza (Prevention and Control of Non-Communicable Disease) ambayo ndiyo
mada kuu ya majadiliano ya Baraza Kuu la UN mwaka huu.
Rais Kikwete
leo pia atakuwa Mwenyekiti wa
mkutano wa waandishi wa habari kuhusu Maendeleo ya Umoja wa Viongozi wa Afrika
Kupambana na Malaria (African Leaders Malaria Alliance - ALMA) ambao yeye ni
mwenyekiti.
Pamoja naye katika mkutano huo, miongoni mwa waalikwa
wengine, watakuwa marais Paul Kagame wa Rwanda na Goodluck Jonathan wa Nigeria,
na Rais wa zamani wa Marekani Mheshimiwa Bill Clinton.
Rais Kikwete
pia leo atashiriki katika Mkutano wa Mwaka wa Taasisi ya Rais Clinton ya
Clinton Global Initiative, na atahudhuria mkutano maalum wenye mada ya Putting
Teeth into Non-Communicable Disease unaondaliwa kwa pamoja na Tanzania,
Australia na Sweden.
Baadaye jioni atakuwa msemaji mkuu katika hafla ya viongozi
ya nchi na Serikali kusheherekea mafanikio ya muongo uliopita ya kupambana na
ugonjwa wa malaria ulioandaliwa na taasisi ya Roll Back Malaria. Miongoni mwa
watakaohudhuria halfa hiyo ni Naibu Katibu Mkuu wa UN, Mheshimiwa Asha Rose
Migiro.
Jumanne,
Septemba 20, 2011, Rais Kikwete atashiriki katika mkutano wa viongozi wa nchi
na Serikali kuhusu Lishe na baadaye mchana atajiunga na Katibu Mkuu wa UN,
Mheshimiwa Ban Ki Moon kushiriki katika hafla ya viongozi iitwayo “Every Woman,
Every Child Leaders Event”. Mchana, Mheshimiwa Rais Kikwete atashiriki katika
tukio maalum la kujadili mikakati ya kimataifa kuhusu afya ya akinamama na
watoto ya Global Strategy for Women’s and Children’s Health.
Asubuhi ya Jumatano, Septemba 21, 2011, Rais Kikwete
atashiriki katika ufunguzi wa majadiliano ya mada kuu ya UNGA mwaka huu, pia
atashiriki katika mjadala kuhusu hali ya chakula wa Beyond Food Security, na
vile vile atashiriki katika mkutano wa viongozi wa Social Good Summit ambako
atapewa tuzo maalum kutoka Umoja wa Mataifa kwa mchango wake mkubwa wa
kuimarisha afya ya akinamama na watoto.
Baadaye mchana, Rais Kikwete atashiriki katika chakula cha
mchana kilichoandaliwa na Mheshimiwa Ban Ki Moon kwa ajili ya viongozi wote
wanaoshiriki katika mkutano wa 66 wa UNGA, na pia atashiriki katika tukio
jingine kuhusu afya ya akinamama lililoandaliwa na Soko la Mitaji la NASDAQ.
Baadaye jioni ya siku hiyo atahudhuria hafla iliyoandaliwa
na Rais Barack Obama wa Marekani kwa ajili ya viongozi wanaoshiriki mkutano wa
mwaka huu wa Baraza Kuu la UN.
Asubuhi ya Alhamisi, Septemba 22, 2011, Rais Kikwete
atahutububia UNGA akiwa msemaji wa pili wa siku hiyo baada ya nchi ya Cyprus,
shughuli ambayo itafuatiwa na shughuli nyingine nyingi za mikutano na viongozi
ukiwamo ule wa kuadhimisha miaka 10 ya Azimio la Durban kuhusu ubaguzi wa
rangi. Ijumaa, Septemba 23, 2022, Rais Kikwete atashiriki katika mkutano wa
viongozi wa nchi na Serikali juu ya usalama wa nguvu za nyuklia wa Nuclear
Safety and Security.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
The Himba are an ethnic group of about 20,000 to 50,000 people living in northern Namibia, in the Kunene region (formerly K...
-
Mineral occurrence in Tanzania by TMAA UONGEZAJI WA PATO LA MTANZANIA Mheshimiwa Spika, 46. Lengo la Dir...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...