September 29, 2011

Mv Spice Islanders 1 UPDATES - Nabii T. B Joshua achangia waathirika


Mwakilishi wa Emmanuel Televisheni  na Kanisa la The Synagogue Church  Of All Nations Bi. Martha Harvey akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete jumla ya shilingi milioni ishirini na tano 25,000,000/- kwaajili ya wahanga wa ajali ya Meli ya MV Spice Islander  iliyozama katika mkondo wa Nungwi huko Unguja na kusababisha vifo vya watu wengi hivi karibuni. Mchango huo uliokabidhiwa leo ikulu jijini Dar es Salaam umetolewa na Kiongozi wa Kanisa hilo Nabii Themitope Balogun Joshua ambaye anaishi katika MAKao makuu ya Kanisa hilo jijini Lagos Nigeria.
 Picha na Ikulu

Nani kuwalipa Dowans Bilions 111?



Nani kuwalipa Dowans Bilions 111

Je ni nani atalipa Mabilioni hayo, kati ya Serikali na Tanesco, baada ya Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam kutupilia mbali pingamizi la kutaka kuzuia kusajiliwa Mahakama Kuu ya Tanzania kwa tuzo ya Billion 94 (na riba ya 7.5% toka Nov 2010) dhidi ya Dowans Tanzania iliyotolewa na Mahakama ya kimataifa ya usuluishi ya kibiashara ICC?


Wengi tulitarajia hukumu hii, sababu ni nyingi, moja wapo ni ukweli kuwa Serikali kupitia kwa Mwanasheria Mkuu walishasema tuzo hii haipingiki, hivo walienda kupambana wakiwa wameshashindwa (psychologically), hivyo kilichokuwa kinafanyika ni ucheleweshaji tu.


Mjadala sasa ni nani anastahili kulipa tuzo hii au Mibilioni hii? kati ya Serikali kupitia wizara ya nishati na madini na Tanesco.


Akitoa maoni yake juu ya hukumu hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe alisema hukumu hiyo ni matokeo ya siasa mbovu.“Tumeingiza nchi hasara kwa sababu ya uongozi dhaifu na siasa za makundi ya CCM,” alisema Zitto na kuongeza:
“Hata hivyo, Tanesco hawawezi kulipa fidia hiyo kwani walilazimishwa kuingia mkataba na hata kuvunja mkataba huo.”


Alisema kamati yake imeshaagiza deni hilo lisitokee katika hesabu za Tanesco na badala yake lilipwe na Serikali.


“Hata Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amegoma kusaini hesabu za Tanesco za mwaka 2010 mpaka Serikali ikubali kubeba mzigo huo,” alisema Zitto.


Ikiwa hivyo ndivyo, kwamba Tanesco walilazimishwa kuingia mkataba ule na pia kulazimishwa kuuvunja, je ni nani aliyekuwa akiotoa ushauri huu wa kisheria, wa kulazimisha kuingia mkataba na baadaye baada ya kuona mazingira ni mwafaka kwake au kwao kuilazimisha Tanesco kuvunja mkataba?


Je ni mwanasheria mkuu wa serikali, ni waziri wa wizari husika au ni nguvu fulani juu ya wote hao? Anyway hilo lahitaji mjadala wake, lakini kwa sasa tuulizane, ni nani alipe deni hili? Kama ni wizara ambayo sote twajua kuwa bajeti yake ilipita kwa mbinde baada ya kukataliwa mara ya kwanza, je itakuwa na fungu la kulipa deni hili?



Ikumbuke kwamba tuzo hii ina riba ya asilimia 7.5, hivyo hakuna hasara yoyote kwa Dowans bali serikali na taifa kwa ujumla, hata hivyo ni nani mmiliki halali wa Dowans anayestahili kulipwa mabilioni yote hayo? Je ni huyu Mheshimiwa wetu aliyetajwa mara kadhaa ktk hukumu ya ICC au ni yule mwarabu aliyekuja na kusema yeye ndio mwenyewe na kuacha maswali mengi kuliko majibu?



Kama ni yule siwezi kumsemea, hatujui watanzania na wala hajui matatizo yetu, wala hajui kuwa kuna watu wagonjwa wanakufa kila siku kwa sababu hospitali hazina dawa na yeye hana pesa ya kununulia wanakufa, au kwamba kuna shule tena za sekondari hazina madawati wala vitabu vya kiada achilia mbali maabara na uhaba wa wali, hajui kuwa kuna migomo inayoashiria kuanza ata kabla muhula wa masomo haujaanza wa vyuo vya elimu ya juu kwa sababu tu ya wanafunzi wengi wanaostahili kukosa mkopo, siwezi kumsemea, kwa hayajui haya.



Lakini kama ni huyu mheshimiwa wetu, ambaye “tunadhani” (pengine sivyo) anaijua Bongo yetu kindakindaki, anajuia changamoto zetu zoote, za elimu, afya, miundombinu, uchumi nk. Huyu naweza kidogo si kumsemea bali kumuomba awe na huruma kidogo na watanzania “wenzake” (sina hakika), awe na imani ata kama ni siasa uchwara ndio zimemuondoa katika kiti kile afahamu kuwa kwa Mungu hakuna kiti kile, hakuna uheshimiwa, hakuna utajiri wala utapewa nafasi ya mbele kwa sababu ulishinda kesi ICC.



Huyu namuomba avae viatu vya wale kina mama wajawazito wanaokufa kila siku kwa matatizo ya kukosa huduma bora wakati wa kujifungua, au ajiweke katika nafasi ya watoto hawa ambao madawati kwao ni msamiati usiokuwepo kwenye kamusi yao, pengine avae japo kihisia uhusika wa kijana yule aliyeuwawa kwa deni la sh 500 tu!, na labda avae viatu vya ndugu zetu Wazanzibar na madhira yaliyowakuta hivi karibuni kwa kukosa tu usafiri wa uhakika, roho nyingi zimepotea. 



Mifano ni mingi sana mingine anayo yeye mwenyewe, amewai pengine kukutana nayo, ya jinsi gani watanzania wana changamoto ambazo zinahitaji pesa nyingi sana kukabilina nazo na si kutoa katika kile kiduchu walichobahatika kukipata, pesa haiwezi kutufikisha mbinguni, ata kama tutajikusanyia pesa na mali nyingi kiasi gani hatuwezi kuondoka nazo, tutaziacha hapa hapa duniani.



Yawezekana tukasema kuwa twawekeza kwa ajiri ya watoto wetu, lakini je kwa mali ya dhuruma twaweka msingi gani kwa waridhi wetu? labda salamu za Nabii T. B Joshua za mwaka mpya zinaweza kumpa ujumbe.  

Chonde chonde Mheshimiwa kuwa na moyo wa imani kwa watanzania wenzio, samehe tuzo hii au itoe kwa idara au asasi maalumu, labda iboreshe elimu, afya au ata miundombinu, ata kama ni kwa jimbo la Igunga, hii itakupa heshima kubwa mbele ya jamii na dunia kwa ujumla kuliko yale yatakayo tokea iwapo serikali italazimika kukopa ama kuchukua fungu la fedha toka kwenye bajeti ambayo ni finyu kukulipa wewe. 

Huu ni mtizamo wangu, binadamu tumeumbwa tofauti, si ajabu wewe au mtu mwingine asikubaliane nao. 

Bernard Rwebangira,
Bongo Pix Blog. 

September 28, 2011

Chips Mayai hatari kwa afya yako!?


WATAALAMU wa Kilimo na Afya wamesema kuwa vifo vingi husababishwa na ulaji hafifu wa matunda na mboga za majani huku wakihadharishwa kuwa ulaji wa chipsi mayai unachangia unene unaosababisha vifo vya ghafla.

 Katika mkutano wa kwanza wa uhamasishaji matumizi ya bidhaa za matunda na mboga unaofanyika mjini Arusha, wataalamu hao walisema inapotokea vifo vya namna hiyo, baadhi ya watu kusingizia sababu mbalimbali hususani uchawi.

 Wamebainisha kwamba watu wengi wanakula matunda na mboga chini ya kiwango cha gramu 400 kilichowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), jambo ambalo ni hatari kwa afya.
 

Mtaalamu kutoka WHO, Godfrey Xuereb alisema jana kwamba takribani watu milioni mbili hufa kila mwaka kutokana na maradhi yanayosababishwa ukosefu wa lishe za matunda na mboga.

 Mwenyekiti wa Baraza la kuendeleza Kilimo cha Matunda na Mboga (Hodect), Felix Mosha alisema viazi vilivyochomwa kwenye mafuta na kuchanganywa na mayai ya kukaanga maarufu kama Chipsi Mayai unaonesha kushika hatamu katika lishe za wakazi wa mijini hasa vijana na wanawake.

 Akielezea chakula hicho kama mlo ‘mchafu’, Mosha Alisema: “Matokeo yake taifa sasa limekumbwa na tatizo la unene uliokithiri hasa miongoni mwa watoto na akina mama na kuchangia vifo vingi isivyotarajiwa.” Ofisa kutoka Wizara ya Kilimo na Chakula, Geoffrey Kirenga Alisema:

 “Na mara nyingi mtu akionekana mnene huchukuliwa kuwa na afya lakini ukweli wengi huwa na utapiamlo na wanapofariki ghafla wanakuwa chanzo cha uvumi, tetesi na hisia za ajabu wakati chanzo hasa huwa ni ukosefu wa vitamini na madini yatokanayo na matunda na mboga”.
 

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe akifungua mkutano huo, alisema wastani wa mtanzania mmoja hula gramu 80 pekee za matunda na mboga kwa siku.

 “Hii ni asilimia 20 tu ya kiwango kilichowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) ambacho ni gramu 400 kwa mtu mmoja kwa siku.”

 Alisema Maghembe na kuongeza kuwa asilimia kubwa ya Watanzania humaliza hadi miezi miwili bila kugusa hata tunda moja.

 “Na hii ni aibu maana hapa nchini kuna matunda ya kila aina ambayo pia hupatikana kwa bei ya chini sana, lakini bado watu hawana mwamko wa kuyatumia kiafya na hata katika mila zingine matunda na mboga huonekana kuwa ni vyakula vya watoto,” alisema Waziri Maghembe.

Source: Habari Leo

Kibaki atangaza siku mbili za maombolezo


Rais Mwai Kibaki ametangaza siku mbili za maombolezo ya kifo cha Mwanaharakati Prof Wangari Maathai, pia kesho itakuwa siku ya mapumziko nchini Kenya ili kutoa nafasi kwa wakenya kushiriki Mazishi ya Mwanaharakati huyo. 

Newzzzz Alert. Tanesco yabwagwa, Dowans Kulipwa Mabilioni yake.

Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali pingamiz lililoweka na Tanesco dhidi ya Dowans Tanzania ya kusajiliwa kwa tuzo ya Billion 94 iliyotolewa na ICC.


Kusajiliwa kwa tuzo hiyo kutaipa nguvu kisheria Dowans kulipwa Mabilion hayo ambayo bila shaka yatakuwa yameongezeka kutokana na riba iliyokuwa inaendana nayo toka kutolewa tuzo hiyo na ICC November Mwaka jana.

Nimeombwa na Michelle Obama!





Bernard --

I see the day-to-day challenges my husband faces, and the difficult decisions he has to make.

I know that everyone supporting the campaign now has stood with Barack even during the hardest times, just like I always do. It gives him strength to know that we have his back.

Will you let Barack know you're with him by making a $3 donation today?

https://donate.barackobama.com/Friday-Deadline

Thank you,

Michelle






Thank You First Lady,
I will make sure I donate before the dead line



Dowans kulipwa yale mabilioni leo??




KITENDAWILI cha iwapo Kampuni ya kufua umeme ya Dowans inastahili kulipwa tuzo ya Sh94 bilioni na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) au la kinatarajiwa kuteguliwa leo wakati Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam itakapotoa uamuzi wake wa kisheria.

 Dowans iliwasilisha maombi katika mahakama hiyo ikiomba tuzo ya kiasi hicho cha fedha dhidi ya Tanesco, baada ya kuamriwa na jopo la majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) ya Paris, Ufaransa Novemba mwaka jana.

 Jopo hilo liliketi chini ya Mwenyekiti Gerald Aksen akisaidiwa na  wasuluhishi Swithin Munyantwali na Jonathan Parke na kutoa uamuzi huo wa kuitaka Tanesco ilipe tuzo hiyo ya mabilioni.

 Vyanzo vya habari kutoka Mahakama Kuu, vilidokeza jana kwamba uamuzi wa maombi hayo ya usali wa tuzo hiyo ya Dowans unatarajiwa kutolewa leo.

 Endapo Mahakama Kuu itakubaliana na maombi ya Dowans, basi tuzo hiyo itasajiliwa na kuipa nguvu ya kisheria kulipwa mabilioni hayo.Hata hivyo, Dowans kwa kujihami, imeshafungua maombi mengine ya utekelezaji wa hukumu hiyo ya ICC katika Mahakama Kuu Uingereza kupitia kwa mwanasheria maarufu nchini.

Source: Mwananchi

Kampeni Igunga zahamia angani, CHADEMA waanza, CCM na CUF kufuata leo.



WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilitikisa anga la Igunga baada ya kuanza kutumia helikopta kufanya kampeni zake, zile mbili za wapinzani wao, CCM zikishindwa kuwasili jimboni humo na kubaki Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kutokana na sababu za kiufundi.Wakati Chadema ikipasua anga na mbili za CCM zikibaki KIA, helikopta ya Chama cha Wananchi (CUF) nayo imeshindwa kutua Igunga jana na sasa inatarajiwa hapa leo.

 Helikopta ya Chadema ilianza kuonekana katika anga la Igunga saa 10:40 jioni ikiwa na maandishi makubwa ya chama hicho na rangi ya bluu.Ujio wa helikopta hiyo ulivuta kwa muda idadi kubwa ya wananchi waliokuwa kwenye Viwanja vya Sabasaba wakisubiri ujio wa helikopta mbili za CCM, ambazo awali, ilielezwa kuwa zingewasili saa 8:00 mchana.

 Baadaye ilielezwa kwamba helikopta hizo za CCM zingetua Igunga saa 11:30 jioni zikiwa na makada wa chama hicho akiwamo Katibu wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Bumbuli, January Makamba.

 Hata hivyo, ilipofika saa 12:00 jioni, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akitumia gari la matangazo la Bendi ya muziki ya ToT Plus alitangaza kwamba helikopta hizo zisingeweza kutua Igunga kutokana na sababu za kiufundi.

Alisema zilichelewa kupata vibali kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam na kwamba baada ya kutua KIA ilishauriwa kuwa ni vyema zilale hapo.

 Alisema kama helikopta hizo zingeondoka KIA jana jioni na kufika hapa usiku wakati tayari kungekuwa na giza kitu ambacho kisingekuwa kizuri kiusalama. Alisema helikopta hizo sasa zitawasili leo saa 4:00 asubuhi.

 Matumizi hayo ya helikopta yanawafanya wananchi wa Igunga kushuhudia kampeni nzito na za aina yake tangu kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza wa vyama hivyo mwaka 1994 na Rostam Aziz kushinda.Jimbo hilo lenye wapiga kura 170,000 katika vijiji 96, halijawahi kushuhudia kampeni nzito kiasi hicho zinazohanikizwa na magari yenye vifaa vya kisasa vya muziki.
 

Habari kutoka ndani ya CCM, zinaeleza kuwa katika kujihakikishia kura katika kipindi hiki cha lala salama, chama hicho kitawatumia makada wake, Makamba na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli wanaoelezwa kuwa na ushawishi mkubwa.

 Kulingana na vyanzo mbalimbali vya habari, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa aliyekuwa mgeni rasmi katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CCM anatarajiwa kurudi tena hapa keshokutwa.Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye aliwasili hapa jana kuongeza nguvu kwa viongozi wa chama hicho ambacho idadi kubwa ya wabunge wake wameweka kambi hapa.
soma zaidi hapa 

Source: Mwananchi

Elimu kibongo bongo, Migomo kabla ya darasa.

University students display placards as they wait for the outcome of a meeting between their leaders and the Ministry of Education and Vocational Training officials in Dar es Salaam on Tuesday, on their overdue loans which they would have collected on the 27th of this month. (Photo by Robert Okanda)



Elimu ya namna hii kweli tutafika? Elimu ya msingi wasoma kwa taabu, hakuna madawati, vitabu, walimu wa kutosha.

 wafaulu kiMungu Mungu, waenda shule za kata, wakaa gheto kama si kwenda na kurudi zaidi ya kilomita ishirini kwa siku, nako darasani hakuna madawati, hakuna maabara, maktaba hazina vitabu, walimu ni kasheshe. 

Lakini nako wafanikiwa kufaulu kiaina, hatimaye waja chuo, ukidhani kuna unafuu, hali ndo kasheshe zaidi, mkopo hauupati mpaka kwanza muemdeshe mgomo, upigwe virungu na mabomu ya machozi na hii ni kipindi chote mpaka umalizapo kozi yako.



 Muhitimu huyu aliyepitia haya yote mwisho wa siku anakuja kuwa mtu wa namna gani? tunakuwa tumejenga taifa la aina gani kupitia mfumo huo?


 Mimi sijui, wewe je? 

September 27, 2011

CHADEMA OMBENI RADHI WAISLAM, VINGINEVYO...!

File picture


KATIBU wa sekretarieti ya Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania (Hay- Atul Ulamaa) Sheikh Sherally Huseein (kulia)akitoa tamko kwa waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu wafuasi wa Chama cha CHADEMA kukaidi kuomba radhi kwa umma wa Kiislamu kufuatia tukio la udhalilishaji kwa kumvua Hijjab Mkuu wa Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Mama Fatma Kimario hapo septemba 15 mwaka huu. Katikati ni Naibu Mwenyekiti wa Umoja huo, Sheikh Abdallah Bawazir na kushoto ni Sheikh Manzi Said Manzi wa taasisi ya Mwinyi Mkuu.Picha na Mwanakombo Juma-
MAELEZO







The Union of Islamic Scholars in the country (Hay-ATUL) has pressured CHADEMA to apologize following the assault of Igunga District Commissioner, Ms Fatma Kimario.

 "We request CHADEMA to issue an apology statement to all Muslims in the entire country on what had happened," said Sheikh Hussein.

 He said if Chadema won't issue a statement, the union would mobilize Muslims in the country and all peace well-wishers not to support the party by any means.

 Sheikh Hussein noted that the union's mission was to protect the rights of Muslims and warned any malicious acts that threatened the security of the country.

 Another Party's Legal Advisor, Mr Mabere Marando, accused the leaders of the Muslim organizations who have involved in giving ultimatum to CHADEMA as being touts of CCM. 

source: Daily News

TACCEO kupeleka Waangalizi wa uchaguzi 226 Igunga.




THE Tanzania Civil Society Consortium for Election Observation (TACCEO) will deploy 226 national observers in Igunga for the forthcoming by-election scheduled for this Sunday.

 The TACCEO Chairperson, Ms Martina Kabisama, told a press conference on Tuesday in Dar es Salaam that the consortium that comprises 17 NGOs coordinated by the Legal and Human Rights Centre will cover all polling stations.

 "Since the campaigns started this September, our observers have visited all 26 wards of the district and have visited the polling stations," she said.

 Ms Kabisama explained that the observers would be part of the continued process from the General Elections conducted on October 30, 2010 and aim to establish how the National Electoral Commission (NEC) coordinates and conducts elections.

 She said since elections was a process, the consortium had conducted preliminary observations on the aspects of the campaign preparations of different political parties, coordination of the NEC of the by-election process in Igunga and the actual campaigns of different parties.

 "Our observers have established that there are a lot of good things taking place but there are challenges as well that seriously need to be addressed by the improvement of further elections," she said.
 

Ms Kabisama highlighted the biggest shortcoming in Igunga as decision not to update the permanent voters' register after the 2010 General Elections meaning that hundreds of people will be denied their fundamental constitution right to vote.

 LHRC Lawyer, Mr Merick Luvinga interpreting the Election Act, said it was silent on specific time the voter register is supposed to be updated and that the wording of the law just said 'when possible'.

Dr Shein aapisha maafisa kadhaa Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Moh'd Shein akimuapisha Khamis Haji Khamis kuwa Kadhi Mkuu mpya wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar.Picha zote na Hamadi Hija-Maelezo Zanzibar





Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Moh'd Shein akimuapisha Balozi Hussein Said Khatib kuwa Mjumbe wa Kamisheni ya Utalii wa Umma Zanzibar.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Moh'd Shein akimuapisha Khalifa Hassan Chum kuwa Kamishna wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar.



"Vijana mna very problem, mnaota jua kama solar power"

Swagaz za mgombea wa Ubunge Jimbo la Igunga chama cha UPDP.

Mgombea Ubunge UPDP azindua kampeni Igunga

Msafara wa mgombea ubunge Igunga UPDP Hemed. 


Vimbwanga vya mgomea Ubunge wa UPDP kama ilivyolipitiwa na TBC na kupewa muda wa kutosha tu,

Kwanza kabisa Tangazo “Vinywaji vyooote vinapatikana palee na chips na kila kitu, hapa ni "breki ya nyau”

“ Samaki hana rivasi”

Kauli za Mgombea,
...Vijana mna very problem, mnaota jua mchana kutwa kama solar power! >>>why hakuna ajira, >>> nichagueni mimi, nitafungua lanchi ya mifugo mtalipwa dola, >>> hakuna mwanafunzi kwenda shule na jembe, >>> nitauza VX langu na kununua power tillers, >>; hii ni elimu kwanza na sio kilimo kwanza, >>> nitanunua matrekta na nyie vijana ndio mtakuwa madereva, naombeni kura zenu”


Bahati mbaya sikulipata jina sawasawa, lakini ilikuwa full bururani kama komedi vile kumwanaglia mgombea huyu, cjui kwanini TBC walimpa muda mwingi kiasi kile, 


Picha na Lukansola JF

JK na Kiongozi wa waasi Libya - Je ruksa sasa kwa balozi kupandisha bendera ya NTC?

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Kiongozi wa Serikali ya Mpito ya Libya Bw.Mustafa Abdel Jalil


CCM WOYEEE


September 26, 2011

Zanzibar UPDATES - Meli tano zapigwa marufuku

Ajari ya Mv Spice Islander 1 yazindua Mamlaka toka usingizini, yazipiga marufuku meli tano kwamba hazina sifa ya kubeba abiria. 

MAMLAKA ya vyombo vya baharini Zanzibar, zimesimamisha huduma za meli tano kutokana na meli hizo kutokidhi viwango vinavyotakiwa kusafirisha abiria na mizigo.

 Meli zilizositishwa safari ni Mv Serengeti, Nura, Buraq One, Buraq Two pamoja na Mubarak kutokana na usajili wa meli hizo ulikuwa ni kusaidia kuvuta meli baharini (tagi) na siyo kubeba abiria.

 Akitoa taarifa hizo kwa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Mamlaka wa Vyombo vya Bahari Zanzibar, Haji Vuai Ussi alisema kukatishwa kwa safari kwa vyombo hivyo kumetokana na kukosa usalama wa uhakika kwa abiria wake.

 Aidha, alisema ingawa meli hizo zilianza kazi za kuchukua abiria kwa muda mrefu, lakini zilishindwa kujisajili kwa kazi hiyo, jambo ambalo limekuwa likienda kinyume cha taratibu za vyombo vya bahari.

 Vuai alisema meli hizo pia zilikuwa zikihudumiwa na wafanyakazi wasiokuwa na sifa wala taaluma ya ubaharia pamoja na kushindwa kutoa taarifa za usalama kwa wasafiri wakati wanapokuwa safarini.

 Alisema Mamlaka imebaini tatizo kubwa katika meli hizo baada ya kufanya ukaguzi na kugundua kuwa meli zote hizo zimekosa mfumo mzuri wa mawasiliano pale linapotokea tatizo la kiufundi.

 Akizungumzia kuhusu usalama wa vyombo vya baharini kwa ujumla, alisema mamlaka imegundua pia matatizo lukuki kwa manahodha wa meli hizo kwa kuondoa meli bila kujua taarifa za usalama wa abiria wao.

 Mkurugenzi huyo alisema mamlaka yake imejipanga upya kuhakikisha kuwa wanachukua hatua za kisheria kwa nahodha ye yote ambaye atabainika kuondoa meli bila ya kuwa na taarifa sahihi za abiria.

 Hivyo amewataka wamiliki wa vyombo vya baharini kutoa ushirikiano kwa mamlaka.

Source: Habari Leo

WINNERS Boulevard.: ARE YOU BUILDING PIPELINES OR HAULING BUCKETS?

WINNERS Boulevard.: ARE YOU BUILDING PIPELINES OR HAULING BUCKETS?: Hapo zamani za kale kulikuwa na kijiji Fulani, kilikuwa kizuri sana kwa kuishi isipokuwa tatizo hakukuwa na majim ya uhakika mpaka mvua in...

NEC WEBSITE KULIKONI?

Hii ni screen shot ya Wavuti ya Tume ya Uchaguzi iliyopigwa saa 12:03 jioni hii, nilitarajia kukuta updates zozote kuhusiana na yale yanayojiri yanayowahusu, lakini iki ndicho kilicho hapo.
]
Update pekee inayoonekana baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana ni sentensi hii yenye maneno yapatayo 19:- "Tume ya Taifa ya Uchaguzi Yatangaza Ratiba ya Uchaguzi wa JImbo la Igunga pamoja na Chaguzi Ndogo za Madiwani"



Hata kwa sentensi hii mtu alitarajia kupata hiyo ratiba inayosemwa, lakini sivyo ilivyo. Mtu anajiuliza kulikoni huko NEC? yaani toka mwaka jana hakuna lolote lililotokea kuhusiana nanyi litupasalo wanachi kuhabarishwa? mtu aliyeikumbuka website hii na kupost hako ka-update ka maneno 19 ilimchukua muda gani hata kushindwa kuweka taarifa kamili?

  Hii yasikitisha kwa kweli, karne hii ya 21 na Zama hizi za Taarifa (Information Age) bado asasi muhimu kama hii inashindwa kuitumia ipaswavyo, mtu alitarajia loe hii kuwe si tu na ratiba bali majina, picha za wagombea na vyama na pengine taarifa kuhusu idadi halisi ya wapiga kura, vituo, na mambo mengine kama hayo.

Shule za Kata hazifai!


Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk. Valentino Mokiwa, amesema haungi mkono shule za sekondari za kata nchini kwa sababu hazijaandaliwa vizuri kuwawezesha watoto kukomaa na kupata elimu iliyo bora.

Aliyasema hayo jana katika mahubiri yake kwenye kanisa kuu la Anglikana Mbeya ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara yake ya kutembelea Dayosisi ya Nyanda za Juu Kusini ya kanisa hilo. Dk. Mokiwa alisema shule nyingi za kata zimejengwa kisiasa na ndiyo maana hata elimu inayotolewa katika shule hizo haikidhi mahitaji ya ushindani wa kielimu. 

Alisema kutokana na shule hizo kujengwa kwa manufaa ya kisiasa, wanafunzi wake wamekuwa wakisoma kwa mtindo wa kinadharia na kukaririshwa, alisema hali ambayo haimfanyi mwanafunzi kuelewa vizuri. “Vijana wa siku hizi mnafundishwa maswali yote mnapewa majibu ya kuchagua, mnapofundishwa suala la ufahamu mnashindwa kuelewa,” alisema Dk. Mokiwa.

 Askofu Dk. Mokiwa alisema ili kurudisha elimu katika kiwango bora, serikali irejeshe shule za  zilizokuwa zikimilikiwa na taasisi za dini ili wao waziendeleze kwa sababu shule hizo zilimjenga mwanafunzi kiroho na kiakili. 

Alisema serikali ilizichukua shule hizo  kama majengo na kuacha msingi ambao ulikuwa umewekwa na shule hizo ambao ulikuwa na mfumo mzuri wa ufundishaji uliozingatia maadili ya mwalimu na mwanafunzi. “Shule za misheni zirudi ni mali ya kanisa, na zitarudi zenyewe au kwa kurudishwa na waliozichukua,” alisisitiza Dk. Mokiwa. 

Akizungumzia suala la ufisadi, Dk. Mokiwa alisema ufisadi ni roho na tabia mbaya ambayo ipo katika kada mbalimbali kuanzia ngazi ya familia mpaka taifa. 

Alisema ufisadi unapaswa kukemewa kuanzia ngazi ya familia kwani ikiachwa  baadaye unaharibu taifa katika sekta za bararabara na umeme na hivyo kuzua malalamiko mengi kutoka kwa Watanzania.


SOURCE: NIPASHE

CCM WATWANGA MWANDISHI WA HABARI


MAKADA wa Chama cha Mapinduzi (CCM) walio katika timu ya kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga, wameendelea kuandamwa na kashfa za matukio ya vurugu baada ya walinzi wa chama hicho (mabaunsa) kumpiga mwandishi wa habari wa gazeti la Dira ya Mtanzania, Mussa Mukama, na kunyang’anywa vifaa vya kazi na fedha. 

Akizungumzia tukio hilo, Mukama alisema alikwenda katika Hoteli ya Peak saa moja jioni walikofikia viongozi wa CCM kufanya mahojiano na Mbunge wa Viti Maalum, Ester Bulaya, kuhusu tukio la juzi la kurushiana risasi na kusababisha gari lake kuvunjwa vioo.

 Mukama alisema akiwa ameambatana na mwandishi wa kujitegemea, George Maziku, alizuiwa na walinzi wa CCM kuingia ndani, hali iliyowalazimu kuwasiliana na Bulaya kwa njia ya simu. 

“Tulimpigia simu Bulaya, ambaye alikuja langoni na kuwataka walinzi waturuhusu kuingia ndani,” alisema mwandishi huyo.

 Hata hivyo, alisema, ilipofika saa 3 usiku, waliagana na Bulaya lakini walipofika langoni yeye aliitwa na mlinzi mmoja ambaye baada ya kumfikia, alishangaa akimkaba na baadaye watu wengine wakajitokeza na kumshambulia kwa mateke, ngumi na makofi na kumnyang’anya fedha sh 423,000, modem na flash.

 Aliongeza watu hao wapatao wanane waliokuwa na sare za CCM na wengine nguo za kawaida waliendelea kumshambulia hadi walipozuiwa na mtu mmoja aliyetoka ndani ya hoteli hiyo. 

“Jamaa walipokuwa wakinipiga walitaka kuninyang’anya laptop yangu; nilipojaribu kumpigia simu Bulaya kumjulisha kilichonipata langoni, simu yake iliita bila kupokelewa,” alisema. 

Aliongeza kuwa baada ya hapo alipata msaada kutoka kwa mwandishi mwenzake, Maziku, aliyekwenda kutoa taarifa katika kituo cha polisi Igunga na kupewa PF3 ya kutibiwa hospitali ya wilaya. 

Alisema polisi walimpa RB namba 1673/2011 na kisha alipata matibabu na kuruhusiwa. Maziku alisema wakati wanatoka ndani ya hoteli alikuwa ametangulia mbele na Mukama akiwa nyuma; na mwenzake alipoitwa na mlinzi hakuwa na wasiwasi, lakini ghafla aliona wakimshambulia na alishindwa kutokana na wingi wa mabaunsa. 

Akizungumzia tukio hilo, Bulaya alisema amesikitishwa na kitendo ambacho ametendewa mwandishi huyo. 

Alisema kuwa baada ya mahojiano hayo aliingia katika kikao ambacho aliamua kuondoa mlio kwenye simu yake, hivyo hakusikia alipopigiwa na Mukama kuomba msaada.

Source: Tanzania Daima.
Ndipo siasa za Bongo zilipofikia sasa hivi. Hii ni hatari hatua za dharura zisipochukuliwa.  

September 24, 2011

Hakuna siri tenaaaaa!


Itakuwa vipi unapita mitaa ya Kongo unatungua Jeans yako moja swaaaafi, unaipiga sop sop kisha watinga nayo kitaani, bila kujua kumbe ina kifaa kiduchu maalumu cha mawasiliano ya kidigitali (radio-frequency identification device, RFID), ambacho kinaonesha kila unapoenda, kila mahali ulipo?

 Alafu fikiria waifu anakutwangia, we wamzuga kuwa huko Mbezi, kumbe ye anakuona kupitia mtandaoni kuwa huko chobingo! au waifu kapigilia hiyo jeans wampigia akwambia yuko home kumbe yuko chobingo, kawekwa mtu kati kisawasawa??

 Itakuwa vipi hapo wadau??

 Jibu  kila mtu atakuwa na la kwake, yaweza onekana kama uzushi au mzuka fulani hivi, lakini hapana si mzuka wa uzushi bali ndivyo ilivyo, huko majuu wametengeneza jeans za namna hiyo zijulikanazo kama “Internet of Things” IOT zenye kifaa hicho cha mawasiliano ambacho kinatuma ujumbe mfupi kupitia mtandao wa Twitter kikionesha kila mahali anakopita mvaaji wa nguo.

 Haya ndo mambo ya Teknoligia, itafika mahali bila shaka hatutakuwa na siri au faragha tena, kila kitu kitakuwa hadharani kwa yeyote kuona ama kufuatilia, mmh itakuwa vipi kwa sisi wependa vijizawadi toka majuu, kumbe jamaa anakupa ili aweze kukumonita vyema kila hatua unayofanya, kila unapokwenda, na pengine kila unachozungumza na hao unaozungumza nao?/

 Je hii ni habari njema wadau au mwaonaje? 



It sounds far-fetched, but it's possible - if one of your garments is equipped with a tiny radio-frequency identification device (RFID), your location could be revealed without you knowing about it.

RFIDs are chips that use radio waves to send data to a reader - which in turn can be connected to the web.

This technology is just one of the current ways of allowing physical objects to go online - a concept dubbed the "internet of things", which industry insiders have shortened to IoT. ..

Source: BBC

Satelite hii imeangukia wapi??

NASA (Shirika la Mambo ya Anga la Marekani) linadhani kuwa Satelite  hii chakavu yenye ukubwa sawa na basi kubwa inaweza kuwa ishadondoka mpaka kufika asubui hii, wanadhani kuwa itakuwa imedondoka kwa kishindo kikuu na pengine kutawanyika umbali wa zaidi ya kilomita 800 katika maeneo ya Canada, Afrika ama baharini.



NASA said early Saturday it was trying to confirm the crash-landing of the biggest piece of US space junk to fall in 30 years, which was over Canada, Africa and open ocean during the re-entry window.

 The US space agency stressed there was a "very remote" risk to the public from the 26 fragments of the Upper Atmosphere Research Satellite (UARS) which were expected to survive the fiery re-entry into the atmosphere.

 The debris was expected to re-enter Earth's atmosphere between 11:45 pm Friday and 12:45 am Saturday (0345-0445 GMT Saturday), NASA said in its latest update.

"During that time period, the satellite was passing over Canada and Africa, as well as vast areas of the Pacific, Atlantic and Indian oceans. The risk to public safety was very remote," the agency added.

 "NASA is working to confirm the re-entry location and time and will provide an update shortly."
The Center for Orbital and Reentry Debris Studies at the California-based Aerospace Corporation predicted the re-entry would occur at 0404 GMT Saturday, plus or minus three hours.

 The two dozen parts that survive the re-entry may weigh as little as two pounds (one kilogram) or as much as 350 pounds (158 kilograms), NASA said, and the debris field is expected to span 500 miles (800 kilometers).

Source: AFP

DICOTA CONVENTION 2011 YAFANA








About DICOTA

Overview

Diaspora Council of Tanzanians in America (DICOTA) is an organization whose purpose is to unite and strengthen the Tanzanian American Diaspora and its supporters, in order to enhance the economic, health, and social well being of Tanzanians and Americans.

Our Mission

We believe in engaging the Tanzanian American Diaspora and its supporters, thus promoting, enhancing and sustaining the relationship between the United States and Tanzania.

Objectives

  • To collaborate in identifying and implementing investment, philanthropic, and/or economic development opportunities in Tanzania and United States.
  • To utilize the intellectual and financial capital of the Diaspora in identifying and engaging in significant, long-term and sustainable project initiatives, for the purpose of improving the livelihood of all Tanzanians and Americans.
  • To seek investment and philanthropic opportunities with public and private organizations within Tanzania and the United States that will support the development of the identified project initiatives.
  • To promote the improvement of the infrastructure in Tanzania
  • To connect Tanzanians living in America and be a liaison to American friends and supporters of Tanzania.

September 23, 2011

Hotuba ya kuaga ya Rais Rupia Banda

Rupia Banda, Zambia former President as from today. 

I HAVE CALLED THIS PRESS CONFERENCE TO SAY A FEW WORDS. THE ELECTION CAMPAIGN OF 2011 IS OVER. THE PEOPLE OF ZAMBIA HAVE SPOKEN AND WE MUST ALL LISTEN. SOME WILL BE HAPPY WITH WHAT THEY HAVE HEARD, OTHERS WILL NOT.

THE TIME NOW IS FOR MATURITY, FOR COMPOSURE AND FOR COMPASSION. TO THE VICTORS, I SAY THIS: YOU HAVE THE RIGHT TO CELEBRATE BUT DO SO WITH A MAGNANIMOUS HEART. ENJOY THE HOUR BUT REMEMBER THAT A TERM OF GOVERNMENT IS FOR YEARS.

REMEMBER THAT THE NEXT ELECTION WILL JUDGE YOU ALSO.
TREAT THOSE WHO YOU HAVE VANQUISHED WITH THE RESPECT AND HUMILITY THAT YOU WOULD EXPECT IN YOUR OWN HOUR OF DEFEAT.

I KNOW THAT ALL ZAMBIANS WILL EXPECT SUCH BEHAVIOUR AND I HOPE IT WILL BE DELIVERED. SPEAKING FOR MYSELF AND MY PARTY, WE WILL ACCEPT THE RESULTS. WE ARE A DEMOCRATIC PARTY AND WE KNOW NO OTHER WAY.

IT IS NOT FOR US TO DENY THE ZAMBIAN PEOPLE. WE NEVER RIGGED, WE NEVER CHEATED, WE NEVER KNOWINGLY ABUSED STATE FUNDS. WE SIMPLY DID WHAT WE THOUGHT WAS BEST FOR ZAMBIA. I HOPE THE NEXT GOVERNMENT WILL ACT LIKEWISE IN YEARS TO COME.

ZAMBIA DESERVES A DECENT DEMOCRATIC PROCESS. INDEED, ZAMBIA MUST BUILD ON HER PAST VICTORIES. OUR INDEPENDENCE WAS HARD WON, OUR DEMOCRACY SECURED WITH BLOOD.

ZAMBIA MUST NOT GO BACKWARDS, WE MUST ALL FACE THE FUTURE AND GO FORWARD AS ONE NATION. NOT TO DO SO WOULD DISHONOUR OUR HISTORY.

TO MY PARTY, TO THE MMD CANDIDATES WHO DID NOT WIN, THE LESSON IS SIMPLE. NEXT TIME WE MUST TRY HARDER.

WE FOUGHT A GOOD CAMPAIGN. IT WAS DISCIPLINED. I STILL BELIEVE WE HAD A GOOD MESSAGE AND WE REACHED EVERY PART OF THE COUNTRY.

WE TRAVELLED TO ALL NINE PROVINCES AND WE SPOKE TO ALL ZAMBIANS. TO THOSE WHO WORKED EVERY HOUR OF THE DAY, I SAY ‘THANK YOU’. YOU HAVE DONE YOUR BEST. BUT, SADLY, SOMETIMES OUR BEST IS NOT GOOD ENOUGH.

DO NOT BE DISHEARTENED. THE MMD WILL BE BACK. WE MUST ALL FACE THE REALITY THAT SOMETIMES IT IS TIME FOR CHANGE. SINCE 1991, THE MMD HAS BEEN IN POWER. I BELIEVE WE HAVE DONE A GOOD JOB ON BEHALF OF ALL ZAMBIANS.

FREDERICK CHILUBA LED US TO A GENUINE MULTI-PARTY STATE AND INTRODUCED THE PRIVATE SECTOR TO OUR KEY INDUSTRIES. ZAMBIA WAS LIBERATED BY AN MMD IDEAL BUT MAYBE WE BECAME COMPLACENT WITH OUR IDEALS. MAYBE WE DID NOT LISTEN, MAYBE WE DID NOT HEAR.

DID WE BECOME GREY AND LACKING IN IDEAS? DID WE LOSE MOMENTUM? OUR DUTY NOW IS TO GO AWAY AND REFLECT ON ANY MISTAKES WE MAY HAVE MADE AND LEARN FROM THEM. IF WE DO NOT, WE DO NOT DESERVE TO CONTEST POWER AGAIN.

THE ZAMBIA WE KNOW TODAY WAS BUILT BY AN MMD GOVERNMENT. WE KNOW OUR PLACE IN HISTORY AND WE KNOW THAT WE CAN COME BACK TO LEAD AGAIN IN THE FUTURE. A NEW LEADERSHIP WILL BE CHOSEN, AND THAT LEADERSHIP WILL BE FROM THE YOUNGER GENERATION.

MY GENERATION… THE GENERATION OF THE INDEPENDENCE STRUGGLE– MUST NOW GIVE WAY TO NEW IDEAS; IDEAS FOR THE 21ST CENTURY. FROM THIS DEFEAT, A NEW, YOUNGER MMD WILL BE RE-BORN. IF I CAN SERVE THAT RE-BUILDING, THEN I WILL.

I MUST THANK MY CABINET FOR DELIVERING ON OUR PROMISES. WE DID A LOT OF GOOD FOR ZAMBIA. MANY OF OUR PROJECTS WILL BLOSSOM INTO BRIGHT FLOWERS. SOME OF YOU WILL BE BACK TO SERVE ZAMBIA AGAIN – I KNOW YOU WILL DO YOUR BEST FOR YOUR PARTY AND FOR YOUR COUNTRY.

TO THE CIVIL SERVANTS AND GOVERNMENT OFFICIALS, IT HAS BEEN A PRIVILEGE TO SERVE WITH YOU. WE HAVE WORKED MANY LONG HOURS TOGETHER. WE DID IT NOT FOR OURSELVES BUT FOR ZAMBIA. SERVE YOUR NEXT MASTERS AS YOU DID ME, AND ZAMBIA WILL BE IN GOOD HANDS.

I MUST THANK MY FAMILY AND MY WIFE. THEY HAVE STOOD BY ME AND I CANNOT ASK FOR MORE LOYALTY THAN THAT WHICH THEY HAVE DISPLAYED. I LOVE YOU ALL DEARLY AND I WILL ALWAYS BE IN YOUR DEBT.
BEING PRESIDENT IS HARD WORK, IT TAKES LONG HOURS OF WORK. AND BECAUSE OF IT, I HAVE NOT ALWAYS BEEN THERE FOR YOU. YET, STILL YOU WERE THERE FOR ME.

WORDS CANNOT EXPRESS THE DEPTH OF MY LOVE FOR YOU ALL. ALL I ASK IS THAT MY FAMILY CONTINUES TO SERVE ZAMBIA AS I HAVE SOUGHT TO DO.

BUT MY GREATEST THANKS MUST GO TO THE ZAMBIAN PEOPLE. WE MAY BE A SMALL COUNTRY ON THE MIDDLE OF AFRICA BUT WE ARE A GREAT NATION. SERVING YOU HAS BEEN A PLEASURE AND AN HONOUR. I WISH I COULD HAVE DONE MORE, I WISH I HAD MORE TIME TO GIVE.

OUR POTENTIAL IS GREAT. OUR RESOURCES ARE IMPRESSIVE.
I URGE YOU ALL NOW TO RALLY BEHIND YOUR NEW PRESIDENT.
YES, WE MAY HAVE DIFFERENT IDEAS BUT WE BOTH WANT THE SAME THING – A BETTER ZAMBIA.

NOW IS NOT THE TIME FOR VIOLENCE AND RETRIBUTION.
NOW IS THE TIME TO UNITE AND BUILD TOMORROW’S ZAMBIA TOGETHER. ONLY BY WORKING TOGETHER CAN WE ACHIEVE A MORE PROSPEROUS ZAMBIA.

IN MY YEARS OF RETIREMENT, I HOPE TO WATCH ZAMBIA GROW. I GENUINELY WANT ZAMBIA TO FLOURISH. WE SHOULD ALL WANT ZAMBIA TO FLOURISH. SO, I CONGRATULATE MICHAEL SATA ON HIS VICTORY.

I HAVE NO ILL FEELING IN MY HEART, THERE IS NO MALICE IN MY WORDS. I WISH HIM WELL IN HIS YEARS AS PRESIDENT.
I PRAY HIS POLICIES WILL BEAR FRUIT.

BUT NOW IT IS TIME FOR ME TO STEP ASIDE. NOW IS THE TIME FOR A NEW LEADER. MY TIME IS DONE. IT IS TIME FOR ME TO SAY ‘GOOD BYE’.
MAY GOD WATCH OVER THE ZAMBIAN PEOPLE AND MAY HE BLESS OUR BEAUTIFUL NATION.
I THANK YOU.
==========END OF AN ERA===========

Source: Lusaka Times

Ni furaha tupu Zambia baada ya upinzani kushinda Urais.


Mshindi wa Kiti cha Urais Zambia, Michael Sata. 



Jubilation and dance characterised the streets of Lusaka, the country’s capital city after final results of Tuesday’s tripartite elections were announced at the national totalling centre at Mulungushi Conference Centre shortly after midnight.

Chief Justice Ernest Sakala, who is Returning Officer of the election to the office of President, declared Patriotic Front (PF) leader Michael Chilufya Sata duly elected President of the Republic of Zambia at exactly 00:34 hours this morning.

This is after he polled 1, 150,045 representing 43 percent against his closest rival out-going President Rupiah Banda with seven constituencies remaining to be counted.
Following the announcement of results, scores of Lusaka residents took to the streets in solidarity of the President elect chanting pro-PF slogans of “Don’t Kubeba’ and trumpeting the famous Vuvuzelas.

Some merry making youths were seen approaching Mass Media complex and upon arrival at the main gate were restrained from entering by police who were manning the gate as they were in their numbers.

However, this did not deter them from continuing with their celebrations outside the complex’s premises where they remained for a couple of hours before heading to Arcades.

A check by a ZANIS crew in Kalingalinga, Chilenje, Rhodes Park, and Kabulonga among other places in the city also found people from all walks of life celebrating.
Those talked to were happy that PF had won the elections and that their prayer had been answered.

One resident from Chilenje, Mutale Wesu congratulated Mr Sata and the entire candidates who stood on the PF ticket for convincingly winning the elections.
Mr. Wesu hoped the new PF government would build on what the former administration the Movement for Multi-party Democracy (MMD) had done.

Another resident, Jane Daka of Kalingalinga Township prodded the incoming PF government to seriously look into the plight of youths whom she said had been marginalised for a long time.

Ms Daka told ZANIS that the youths contributed immensely to the PF victory hence the need for the new government to address challenges facing the youth such as unemployment, drug abuse and diseases.

Mario Mukumbuta of Rhodes Park appealed to the President-elect not to be vengeful but forgive all those that had unjustly accused him.


Meanwhile, scores of Chawama residents have received the news of victory of the incoming President with great joy.

The residents came out of their houses onto the streets to celebrate Mr. Sata’s victory as fifth republican President of Zambia since the country’s political independence in 1964.

The residents expressed happiness that their verdict had been passed peacefully through the ballot paper.

Adamson Phiri said people’s cry of a responsive Government that would look after the welfare of ordinary Zambians had been heard.

Mr. Phiri paid tribute to outgoing President Rupiah Banda who has been Head of State since the demise of third republican President Dr Levy Mwanawasa in 2008.

In Serenje distict,hundreds of residents thronged the streets and gathered at Serenje District Commissioner’s office to celebrate the election of Mr. Sata as President-elect.
The residents also carried shoulder high newly elected PF Serenje Central Member of Parliament Phillip Kosamu.

ZANIS reports that the residents who were also in a convoy of over 30 motor vehicles honked and horned as they went round chanting the PF’s political campaign slogan “Pa Bwato and Don’t Kubeba”.

A resident Nancy Kunda described Mr. Sata’s victory as a blessing to the country and wished him well in his endeavours.

Ms. Kunda further described the outcome of the result as a true reflection of the will of the Zambian people.

The 2011 presidential polls were the second heavily contested with ten candidates after the 2006 presidential elections which attracted a record 11 presidential contestants.
The MMD has ruled Zambia for the past 20 years and it ushered in among several other developments democracy, freedom of Speech and liberalised the country’s economy.

Others who contested the tripartite elections are Hakainde Hichilema of the United Party for National Development (UPND) who polled 489, 944 representing 18.5 percent, Charles Milupi of the Alliance for Democracy and Development who got 13, 382 representing 0.8 percent while National Restoration Party (NAREP) leader Elias Chipimo polled 10, 190 representing 0.4 percent.





Former President Banda and his wife Thandiwe during a farewell press conference in Lusaka

Source: Lusaka Times.

Kampeni Chadema, CCM zafika pabaya

Mbunge wa Tabora Mjini Ismail Aden Rage akipanda jukwaani kumnadi mgombea wa CCM Jimbo la Igunga Dalali Peter Kafumu.  

JOTO la uchaguzi mdogo katika Jimbo la Igunga, mkoani Tabora linaendelea kupanda baina ya vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo, huku kampeni zinazoendelea zikichukua sura ya mapambano baina ya vyama viwili vikubwa nchini, CCM na Chadema.Katika kile kinachoonekana kuwa hofu kadri siku ya uchaguzi inavyokaribia, jana CCM kupitia Katibu Mkuu wake, Wilson Mukama, kiliendeleza tuhuma dhidi ya Chadema ambacho kwa upande wake kilijibu mapigo kupitia kwa Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe.

 Mukama akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari mjini Igunga, alitoa tuhuma nzito kwa Chadema, akisema chama hicho kikuu cha upinzani nchini, kimeingiza kundi la makomandoo 33 kwa lengo la kuvuruga uchaguzi.

  Katibu Mkuu huyo aliyekuwa akizungumzia tathmini ya kampeni za uchaguzi huo mdogo, alitumia muda mwingi kukizungumzia Chadema, huku akivisahau vyama vingine sita ambavyo pia vinashiriki uchaguzi huo.

 Hata hivyo, Mbowe akizungumza na Mwananchi alijibu tuhuma hizo kwa kumshangaa Mukama na kueleza kuwa kauli zake katibu mkuu huyo wa CCM ni matokeo ya “kushiriki siasa za uzeeni”."Sasa hili Mukama hawezi akajua kwa sababu yeye anafanya siasa za uzeeni. ..Yeye (Mukama) hajawahi kugombea udiwani, uenyekiti wa mtaa, ubunge au nafasi yoyote ndani ya chama chake zaidi ya huu ukatibu mkuu ambao alipewa tu.. atayajuaje hayo?" Alihoji na kuendelea:

Source: Mwnanchi

September 22, 2011

Tuzo zaidi kwsa JK New York.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihudhuria mkutano wa 'Social Good Summit' anapokea tuzo kutoka United Nations Foundartion for his work in Martenal Health and Social Media Commitment kutoka kwa Makamu wa Rais wa Public Policy of United Nations Foundation Mr. Peter Yeo katika sherehe fupi iliyofanyika jijini New York jana.
 

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mheshimiwa Ban Ki- Moon kwenye Makao Makuu ya Umoja Mataifa jijini New York nchini Marekani.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amepokea Tuzo Mbili Maalum kwa mchango wake mkubwa katika Afya ya Mama Mjamzito na Watoto kwa ujumla kutoka taasisi mbili tofauti mjini New York.

Tuzo ya kwanza imetolewa na Taasisi ya Kijamii ya Umoja wa Mataifa (UN Foundation) na kukabidhiwa kwa Rais na Makamu wa Rais wake anayeshughulikia sera ya Umma Bw. Peter Yeo.

Rais amepokea Tuzo ya pili katika makao makuu ya Soko la Hisa la Marekani (National Association of Securities Dealers Automated Quotations) kwa kifupi NASDAQ ambalo ni soko la pili kwa ukubwa duniani baada ya lile la New York.  Rais amekabidhiwa tuzo hiyo na Makamu wa Rais wa NASDAQ Bw. David Wicks.

 Mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo Rais amepewa heshima maalum ya kugonga kengele kuashiria mwisho wa biashara kwa siku hiyo.

Akipokea tuzo hizo mbili maalum, Rais ameelezea changamoto zinazoikabili sekta ya Afya nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla na kuzishukuru nchi na taasisi mbalimbali ambazo zinaunga mkono juhudi za kupunguza matatizo ya afya ya mama mjamzito.

“Si sahihi kwa mama mjamzito kufariki wakati anampa uhai binadamu mwingine, uzazi unatakiwa kuwa shughuli ya furaha na sio huzuni na ndiyo maana tumetoa kipaumbele kwenye afya ya mama mjamzito kwenye ajenda yetu ya Afya” Rais amesema.

Rais amewaeleza wageni waalikwa ambao katika hadhara zote mbili wametoka katika nchi na taasisi mbalimbali kuwa kati ya vitu ambavyo serikali ya Awamu ya Nne imeamua kutoa kipaumbele katika kuongeza huduma za afya ya uzazi kwa kujenga zahanati na kuzipandisha daraja zilizokuwepo.

Serikali pia inaajiri wakunga na wataalamu zaidi wa Afya na kuongeza mafunzo katika sekta hiyo.

Juhudi zingine ni pamoja na kutoa huduma za Mpango wa Uzazi bure na kutoa vifaa vya kujifungulia kwa akina mama wanaohudhuria kliniki.

“Vifaa hivi ni maalum kwa ajili ya kuwasaidia akina mama wakati wa kujifungua, na tuna amini kuwa kwa kufanya hivi wanawake wengi zaidi watahudhuria kliniki na kuwapa motisha wa kujifungulia katika taasisi zetu za afya”. Rais ameeleza.

Kutokana na juhudi hizo takwimu zinaonyesha kupungua kwa vifo vya akina mama wajawazito na  wakati wa kujifungua  kutoka 8,000 kwa mwaka 2005 hadi 6,000 mwaka jana.

“Upungufu wa vifo 2,000 ni hatua nzuri katika muda mfupi lakini bado hairidhishi sana, tunaweza kupunguza zaidi na hilo ndiyo lengo letu kwani hatutaki kuona mwanamke yeyote anakufa kutokana na ujauzito au wakati wa kujifungua”. Rais amesema.

Mbali na shughuli hizo, Rais amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Slovenia Dr. Danilo Turk, Makamu Waziri Mkuu wa Luxembourg Bw. Jean Asselborn na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki Moon na Waziri wa Maendeleo wa Uingereza Bw. Andrew Mitchell.

Leo tarehe 22 Septemba, 2011, Rais anatarajiwa kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
MWISHO.
 
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
New York.
Marekani.
22 Septemba, 2011


Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...