March 10, 2011

Pinda ashangaa wanafunzi kukosa viatu.

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amesikitishwa na maisha wanayoishi wanafunzi wa Shule ya Msingi Mulusagamba iloyopo wilayani Ngara, Mkoa wa Kagera.

Pinda alionyesha masikitiko hayo jana baada ya kufika shuleni hapo na kuwaona wanafunzi wa shule hiyo wakitembea bila viatu huku sare zao za shule zikiwa chafu.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Waziri Mkuu huyo ambaye yuko katika ziara ya kiserikali katika Mkoa wa Kagera, alifika katika shule hiyo kwa ajili ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Wilaya ya Ngara iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Salumu Nyakonji.

”Hali walionayo wanafunzi hawa ni mbaya sana kwani inaonekana kuchangiwa na umaskini unaowakabili wazazi wao.

“Ili kuondokana na hali hii lazima sasa viongozi wa wilaya muwe wabunifu, mbuni fursa mbalimbali zitakazowaongezea wananchi wastani wa kipato chao.

“Viongozi lazima mhakikishe wananchi wanaboresha kilimo ili kiwe na tija kwani kwa kufanya hivyo wataweza kukabiliana na umaskini wa kipato unaowakabili,” Alisema Pinda

Ili kuimarisha Kilimo Kwanza, aliwataka viongozi wilayani hapa wawahamasishe wananachi juu na manufaa ya kilimo cha kisasa kwa kufuata kanuni za kilimo.

Kwa mujibu wa Mtanzania

Ahadi zaanza kutekelezwa, Bajaj za wajawazito vijijini hizoooo

Moja ya Pikipiki 400 zitakazo tumika kubebea wagonjwa "Ambulance"

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...