January 26, 2009

Ujumbe kila kona..

Huwa nina kawaida au tabia ya kusoma kila kilichombele yangu kilichoandikwa, sijui kama kawaida/tabia hii ni mzuri au la kila mtu aweza sema lake.

Lakini jambo moja nilijualo ni kuwa kila nisomapo chochote kile sikosi kupata ujumbe au kujifunza jambo,

Ni wangapi wetu uwa twapoteza japo sekunde ka si dakika kusoma hivi vitiketi vya daladala? hebu soma kwa makini tiketi hii alafu niambie kile ulichogundua au kujifunza hapo. Jibu unalo.

Leo nimebahatika kupanda magari mawili ambalo kila moja lilikuwa na jumbe toka pande mbili za imani zetu kuu au kielelezo cha ustaarabu na utamaduni wetu watanzania wa kuweza kujichanganya pasipo kuwa na mikwaruzano na kila mtu akashika hamsini zake.

Moja wapo ni hili lililonipa tiketi hiyo, na la pili lilikuwa na kila namna ya ujumbe ndani ya basi wa Qorani takatifu kuanzia ule wa "Allah is One" N.K Lakini muziki uliokuwa ukitutumbuiza na kutusahaulisha machungu ya foleni za jiji la Bongo ulikuwa toka kwa Dada Upendo Nkone, kwa wale wapenzi wa nyimbo za Gospel mwajua ni nyimbo za aina gani dada huyu aimba au za milindimo ya namna ipi. Basi ilikuwa ni burudani kwetu sote, na hii ndio Tanzania kisiwa cha amani na ustaamilivu wa imani.

Na kwa wale wasiotaka kuokoka someni ujumbe huo.

Mpiganaji Athumani aendelea vyema.

Mpiganaji Athumani Khamis akijuliwa khari na Maofisa toka TSN, Mkumbwa Ali Naibu Mhariri Mkuu na Emmanuel Makene Katibu wa shirika katika Hospital ya Millpark huko Afrika Kusini katika jiji la Jo'burg hivi karibuni.

Khali ya Athumani inaendelea vizuri na inatia matumaini, kwani hivi sasa angalau ameanza kupata hisia miguuni na kuweza kuinua mikono ni jambo la kumshukuru Mungu sana na hakika kwa mapenzi yake Mwenyezi Mungu muumba wa vitu vyote nina imani kubwa kuwa siku moja Mpiganaji huyu atakuja tembea tena kwa miguu yake kwani hakuna neno gumu lakumshinda MUNGU.

Blogu hii inakuombea sana Mpiganaji upone haraka na upate kurudia maisha yako kama zamani na hali hii iwe kwako sehemu ya historia tu.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...