Na kwa wale wasiotaka kuokoka someni ujumbe huo.Huwa nina kawaida au tabia ya kusoma kila kilichombele yangu kilichoandikwa, sijui kama kawaida/tabia hii ni mzuri au la kila mtu aweza sema lake.
Lakini jambo moja nilijualo ni kuwa kila nisomapo chochote kile sikosi kupata ujumbe au kujifunza jambo,
Ni wangapi wetu uwa twapoteza japo sekunde ka si dakika kusoma hivi vitiketi vya daladala? hebu soma kwa makini tiketi hii alafu niambie kile ulichogundua au kujifunza hapo. Jibu unalo.
Leo nimebahatika kupanda magari mawili ambalo kila moja lilikuwa na jumbe toka pande mbili za imani zetu kuu au kielelezo cha ustaarabu na utamaduni wetu watanzania wa kuweza kujichanganya pasipo kuwa na mikwaruzano na kila mtu akashika hamsini zake.
Moja wapo ni hili lililonipa tiketi hiyo, na la pili lilikuwa na kila namna ya ujumbe ndani ya basi wa Qorani takatifu kuanzia ule wa "Allah is One" N.K Lakini muziki uliokuwa ukitutumbuiza na kutusahaulisha machungu ya foleni za jiji la Bongo ulikuwa toka kwa Dada Upendo Nkone, kwa wale wapenzi wa nyimbo za Gospel mwajua ni nyimbo za aina gani dada huyu aimba au za milindimo ya namna ipi. Basi ilikuwa ni burudani kwetu sote, na hii ndio Tanzania kisiwa cha amani na ustaamilivu wa imani.
January 26, 2009
Ujumbe kila kona..
Mpiganaji Athumani aendelea vyema.
Mpiganaji Athumani Khamis akijuliwa khari na Maofisa toka TSN, Mkumbwa Ali Naibu Mhariri Mkuu na Emmanuel Makene Katibu wa shirika katika Hospital ya Millpark huko Afrika Kusini katika jiji la Jo'burg hivi karibuni.
Khali ya Athumani inaendelea vizuri na inatia matumaini, kwani hivi sasa angalau ameanza kupata hisia miguuni na kuweza kuinua mikono ni jambo la kumshukuru Mungu sana na hakika kwa mapenzi yake Mwenyezi Mungu muumba wa vitu vyote nina imani kubwa kuwa siku moja Mpiganaji huyu atakuja tembea tena kwa miguu yake kwani hakuna neno gumu lakumshinda MUNGU.
Blogu hii inakuombea sana Mpiganaji upone haraka na upate kurudia maisha yako kama zamani na hali hii iwe kwako sehemu ya historia tu.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
The Himba are an ethnic group of about 20,000 to 50,000 people living in northern Namibia, in the Kunene region (formerly K...
-
Mineral occurrence in Tanzania by TMAA UONGEZAJI WA PATO LA MTANZANIA Mheshimiwa Spika, 46. Lengo la Dir...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...