September 21, 2011

Obama akutana Kiongozi wa waasi Libya


President Barack Obama (R) meets with Libyan National Transitional Council (NTC) Chairman Mustafa Abdul Jalil at the beginning of the UN General Assembly, in New York City, New York, USA, 20 September 2011. World leaders are gathering this week in New York for the annual meeting of the UN General Assembly, which will focus on post-Gaddafi Libya and the Palestinians’ bid for statehood, amongst other issues.


Credit: EPA

Baada ya kushutumiwa na Pinda, polisi waibuka na kujichimbia mkwara,


IGP Saidi Mwema akiwa na DCI Robert Manumba. 

Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Robert Manumba amesema kuwa jeshi la polisi litawachukulia hatua kali askari wote wanaojiususha na magendo ya sukari, hii ni baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuwashutumu hadharani kuwa kuna polisi wanahusika katika sakata zima la utoroshwaji wa sukari nje ya nchi na hivyo kusababisha uhaba usio na lazima. 


JWTZ Kuridhi polisi sakata la sukari 
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amewatuhumu polisi, kwamba wanahusika na utoroshaji wa sukari nje ya nchi na kulitaka Jeshi hilo kukomesha vitendo hivyo mara moja, vinginevyo Serikali italiagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuingilia kati ili kudhibiti vitendo hivyo.

 Akiwahutubia mamia ya wakazi wa hapa akiwa katika ziara ya Mkoa wa Mara, Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kulikalia kimya suala hilo huku wananchi wakiteseka.
 Alisema viwanda vya sukari vya Mtibwa na Kilombero vilivyopo mkoani Morogoro, Kagera na TPC cha Moshi, vinafanya kazi nzuri ya kuzalisha wastani mzuri wa sukari ambayoinatosha kwa matumizi ya wananchi, lakini sukari hiyo haipatikani nchini.

 “Viwanda hivi vinazalisha tani 41,000 hadi 44,000 wakati matumizi yetu ni wastani wa tani 30,000 na 31,000; hii inaonesha kwamba kuna karibu tani zaidi ya 10,000 za ziada. Lakini jambo la ajabu sukari haipatikani nchini na kuifanya kupanda bei na kuumiza wananchi,” alisema Pinda.

 Alisema amepewa taarifa za siri, kwamba baadhi ya polisi wanashiriki katika utoroshaji huo wa sukari kwenda nchi jirani na husindikiza magari ya wafanyabiashara yenye sukari ili kupita kwenye vizuizi vya barabarani kirahisi.

 “Wanapigiana hadi simu kutaarifiana, kwamba jamani eee kuna gari lenye namba fulani linakuja na mzigo, likifika hapo lipite bila matatizo.

 Wanafanya hivi kwa maslahi yao binafsi na si kuwasaidia Watanzania. “Nimemwagiza RPC (Kamanda wa Polisi wa Mkoa) na kundi lake, lakini pia nimemwagiza Kaimu Mkuu wa Mkoa (Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Geofrey Ngatuni) kukomesha suala hili haraka.

 Kama itaonekana wanashindwa, basi tutawaagiza Jeshi (JWTZ) kuingia kati ili kudhibiti. “Hatutaki kufika huko, nawaomba polisi wafanye kazi yao ipasavyo ili kukomesha hali hiyo mara moja,” alisema Pinda.
source Habari Leo

Hatimaye Muhubiri Gilbert Deya kurejeshwa Kenya kushtakiwa


Mhubiri ambaye aliyedai kuwa ana uwezo wa kuwatungisha mimba kina mama kimiujiza kupitia maombi atarudishwa nchini Kenya kukabiliana na mashtaka ya utekaji watoto.
 Gilbert Deya, ambaye huongoza misa katika eneo la Peckham London Kusini, amekuwa akikabiliana kisheria asirejeshwe Kenya tangu mwaka 2007, akidai kuwa hatua yeyote ile itakayochukuliwa dhidi yake itakiuka haki zake za kibinadamu.
 Kwa sasa Waziri wa Mashauri ya Ndani Theresa May ameamua mpango wa kumrejesha mhubiri huyo Kenya uendelee.
 Serikali ya Kenya inadai kuwa aliwaiba watoto watano kati ya mwaka 1999 na mwaka 2004.
 Wasiwasi ulizuka 2004 mara tu baada ya kipindi kimoja cha BBC radio 4 cha udadisi kwa Jina Face the Facts kupeperusha hewani shughuli zinazofanywa na Deya.
 Wanawake ambao hawangeweza kutunga mimba ama waliokuwa wamepita umri wa kuzaa, waumini katika kanisa lake la Peckham Kusini mwa London waliahidiwa wataweza kupata watoto kimiujiza.
 Lakini watoto hao walikuwa wanazaliwa katika zahanati bandia mjini Nairobi nchini Kenya.
 Watu hawa walikwenda Afrika na kurejea Uingereza na mtoto ambaye vyombo vya utawala viligundua hakuwa mtoto wao kupitia upimaji wa asidi nasaba.
Mbunge David Lammy
 Mke mmoja na mumewe ambao walipitia miujiza hiyo walirejea London na kwenda katika hospitali moja ya eneo la Tottenham eneo la mbunge David Lammy.
 "kilichojitokeza hapa ni kuwa kulikuwa na wizi wa watoto, ambao hukuwahusisha tu watu katika eneo langu la uwakilishi bali pia wanawake kadhaa waliokwenda Kenya na kurudi nyumbani wakidhani watoto waliorudi nao ni wao" alisema David Lammy.
 Gilbert Deya akihojiwa na Radio 4 mwaka 2004, alipoulizwa anajieleza vipi kuhusu kuwepo na tofauti kubwa kati ya asidi nasaba ya watoto na wazazi wao , alijibu " Watoto wanaozaliwa kimiujiza katika Kanisa letu wanazaliwa kwa miujiza ambayo binadamu hawezi kuitafakari"
 Mwaka 2007, Waziri wa Mashauri ya Ndani wa Uingereza wakati huo Jacqui Smith aliamua Deya arudishwe hadi Kenya.
 Deya alikataa rufaa dhidi ya uamuzi huo aliyoiwasilisha katika Mahakama kuu, rufaa hiyo haikufaulu na pia alikataliwa kuwasilisha malalamishi yake katika bunge la malodi.

Source: BBC

HUDUMA YAKE IPO HAPA 

Kulikuwa na sababu shauri hili kufika hapa????

Mahita alipa mil. 12/- fidia ya mtoto

MKUU wa Jeshi la Polisi mstaafu (IGP), Omar Mahita, amesalimu amri ya mahakama ya Kinondoni baada ya jana kutoa sh milioni 9 kati ya milioni 12 alizoamriwa kulipa kwa ajili ya fidia ya malezi ya mtoto aliyezaa na msichana wake wa kazi ambaye awali alimkana mahakamani.

 Mahita alilipa fedha hizo jana kupitia kwa wakili Charles Semgalawe na kutoa ahadi ya kumalizia kiasi cha sh milioni 3 zilizosalia ndani ya siku 30. Malipo hayo yanafuatiliwa na kampuni ya udalali ya Nasm Auction Mart.

 Awali kabla ya Mahita kulipa fedha hizo, alipewa siku 14 zilizomalizika jana baada ya mlalamikaji Rehema Shabani ambaye ni mama mzazi wa mtoto Juma Omar Mahita kwenda kudai mahakamani fidia kutokana na mdaiwa huyo kuchelewesha malipo aliyoamriwa na mahakama.

 Katika kesi ya msingi, mahakama ilimpa ushindi mlalamikaji Rehema kwa kumtambua mtoto Juma kuwa ni mtoto halali IGP Mahita.

 Katika hukumu hiyo mahakama ilimtaka Mahita mbali na kumtambua mtoto huyo kuwa ni wake pia ilimuagiza kulipa sh 100,000 kila mwezi kwa ajili ya matunzo.

 Mara baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Mahita alipinga na kuamua kukata rufaa mahakamani akidai hukumu iliyotolewa na mahakama ya Kinondoni si halali, lakini mahakama hiyo iliyatupilia mbali maombi hayo.

 Kwa sasa mtoto wa Mahita Juma Omar anasoma kidato cha kwanza katika sekondari ya Hananasif iliyoko Kinondoni.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...