September 12, 2011

Maafa zaida Afrika Mashariki - Moto wateketeza mamia Nairobi, Kenya

Wakati Zanzibar inaendesha sala maalumu kwa waathirika wa ajali ya Mv Spice Islanders ambapo watu zaidi ya 200 wamepoteza maisha na mamia hawajulikani walipo huku 620 wakiokolewa, jirani zetu Kenya nao wamepatikana na janga baya baada ya moto uliotokana na bomba la mafuta kulipuka na watu wapatao 120 kupoteza maisha. 

Hii si habari njema kwa upande huu wa Afrika Mashariki, hatuna budi kumuomba Mwenyezi Mungu atuondolee jinamizi hili. 


Zaidi ya watu mia moja wamekufa baada ya bomba la mafuta kupasuka na kulipuka katika katika mji mkuu wa Kenya Nairobi, polisi wamesema.
 
Mlipuko huo umetokea katika eneo la viwandani la Lunga Lunga na askari wa zima moto walipambana na moto mkali ambao ulikuwa ukitishia makazi ya watu mjini humo.
 
Bomba hilo la mafuta limepita katika makazi ya watu wengi kwenye mitaa ya mabanda katikati ya mji wa Nairobi na Uwanja wa ndege.
 
Zaidi ya majeruhi 100 wamepelekwa hospitali, maafisa wanasema.
 
Msemaji wa magari ya huduma za dharura alisema waathirika wengi waliungua kiasi cha kutokufatambulika.
 
Taarifa zinasema mlipuko huo huenda umesababishwa na kishungi cha sigara kilichotupwa katika mtaro wa maji ambao ulikuwa ukielea mafuta.
 
Mafuta hayo yalivuja kutoka kwenye tangi moja katika ghala linalomilikiwa na Kampuni ya Mafuta ya Kenya, msemaji wa polisi Charles Owino ameliambia shirika la habari la Reuters.







Sources: BBC, Daily National, NTV

Mv Spice Islander - Simulizi ya Baharia

  • Nahodha, Mabaharia 11 hawajulikani walipo,
  • Mamia bado hawajulikani walipo,
  • Wazamiaji 12 toka Afrika kusini wawasili na vifaa vya kisasa kusaidia uokoaji.
  • Leo ni siku ya mapumziko Visiwani
  • Dua maalumu yasomwa katika viwanja vya Maisara


Baharia Rashid Said Rashid wa meli ya Mv. Spice Islander, iliyozama na kuua takribani watu 240 huku wengine 619 wakinusurika visiwani Zanzibar juzi, amesema waligawa maboya ya kujiokoa kwa abiria na kuwavalisha watoto kisha kuwaondoa melini kupitia madirishani kabla ya kuzama.
Akizungumza na NIPASHE akiwa amelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar, jana, alisema kabla ya meli hiyo iliyokuwa na mabaharia 12 kuzama majira ya saa 7:00 usiku wa Ijumaa iliyopita eneo la Nungwi, waliomba msaada kwa meli nyingine iliyokuwa inapita lakini hawakufanikiwa.
Said ambaye ni mkazi wa Shangani, alisema baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya kabla ya meli kupinduka, abiria walimtaka nahodha atoe taarifa kwao kama meli inazama na alifanya hivyo.
“Tulijaribu kufanya kila jitihada ili kuokoa hali hiyo, lakini tulishindwa na tukaamua tuiache meli na kuanza kutoka, hapo tena kila mmoja alikwenda kwa upande wake,” alisema.
Hata hivyo, alisema hafahamu kama mabaharia wenzake na nahodha wapo salama au wamekufa kwa sababu mara ya mwisho aliwaona kabla ya chombo kupinduka na kuzama.
“Kwa kweli siwezi kusema kama ni uzembe au la umefanyika, lakini wakati inatokea hali hii tulipishana na meli ya MV Jitihada na kuwapa ishara ya kuzama, lakini hawakutusaidia,” alisema baharia huyo.
Alisimulia kuwa walichukua jitihada mbalimbali za kuwapa ishara, lakini hawakufanikiwa na hawezi kusema kama walidharau au hawakuwaelewa walichokuwa wakikitafuta kutoka kwao.
Source: Nipashe

Binti Gadhaf kantunuku, anataka kunipa Mahela!


Dear,
My names are Aisha Ghadafi. The daughter of Colonel Ghadafi the Libyan leader.as a Libyan mediator and military official, former UN Goodwill Ambassador, philanthropist, humanitarian. I want you to take charge of some deposit fund. Reply for more details. E-mail: aishaghadafi2@w.cn
Aisha Ghadafi. 

Bongo pix say, 
Wadau nimepata email hii asubui hii, si ndo kwaitwa kulala masikini kuamka tajiri huku? nimjibuje huyu Binti Gadhafi? anadai ana mahela meeengi na amenitunuku anataka miye ndo niyakamate, jaman si ni kismati hiki au mwasemaje wadau? naombeni mawazo yenu kabla hajabadili msimamo!


Ukweli kuhusu Mv Spice Islander 1

  • Imetengenezwa Ugiriki 1967 ikijulikana kama Marianna 
  • Ina uwezo wa kubeba tani 836 GRT (Mizigo na abiria)
  • Imeuzwa zaidi ya mara mbili
  • Ilinunuliwa kama mtumba mwaka 2007 na Makame Hasnuu akabadili jina kuwa Spice Islander 1
  • Ilishawai kupata tatizo la Inngine ikielekea Somalia, 
  • Ina uwezo wa kubeba abiria 645. 


Description
The ship was 60.00 metres (196 ft 10 in) long, with a beam of 11.40 metres (37 ft 5 in). She was assessed at 836 Gross Registered Tonnage, 663 NRT, 225 Deadweight Tonnage. The ship was propelled by two Poyaud 12VUD25 diesel engines, of 1,560 horsepower (1,160 kW).
 

Built in 1967 as Marianna for an unknown owner, she was later sold to Thelogos P Naftiliaki, Piraeus, Greece. In 1988, Marianna was sold to Apostolos Shipping and renamed Apostolos P. She was later sold to Saronikos Ferries and placed in service on the Piraeus - Aegina - Angistri route.
 

In 2005, Apostolos P was registered to Hellenic Seaways. In 2007, she was sold to Makame Hasnuu, Zanzibar, Tanzania. and renamed Spice Islander I. On 25 September 2007, Spice Islander I was off the coast of Somalia when she experienced engine problems due to contaminated fuel. After the alarm had been raised via Kenya, USS Stout from Combined Task Force 150 was sent to her aid. The ship was on a voyage from Oman to Tanzania and was not carrying any passengers. USS James E. Williams also responded. Stout provide the ship with 7,800 US gallons (30,000 l; 6,500 imp gal) of fuel and supplied the ten crew with food and water. After her engines were restarted, she resumed her voyage to Tanzania.
On 10 September 2011, she sank with large loss of life. 

 Read more here

'No one will be spared' after Zanzibar ferry disaster - SMZ


Tanzania's authorities promised to "not spare anyone" as they began investigations into how almost 200 people died, including 50 children, when an overloaded ferry capsized near Zanzibar.

 Helicopters, rescue boats and scuba divers continued to search for survivors in the waters off the island on Sunday, as three days of official mourning began.
Some 619 people had already been found alive. Many had hung on to floating wreckage through the night. But officials said that hopes of finding more survivors from what is Zanzibar's worst maritime accident were fading. At least 197 people died.

Mohamed Aboud Mohamed, the island's minister of state, said that investigations were focused on why a ship licensed to carry 600 people was allegedly carrying more than 800.

"The government will take stern measures against those found responsible for this tragedy, in accordance with the country's laws and regulations," he said. "We will not spare anyone."

Heavy loads, including vehicles, building materials and cement, were also taken aboard the MV Spice Islander before it left Tanzania's main city, Dar es Salaam, late on Friday, bound for Zanzibar.
The telegraph  

Zanzibar - Mamia bado hawajulikani walipo


  • Miili 240 yapatikana 
  • 39 wazikwa na serikali
  • Helcopter, Wazamiaji na Boti za uokozi zaendelea na juhudi za uokoaji



Add caption
MJI wa Zanzibar na viunga vyake, jana uliendelea kuwa katika taharuki na simanzi kubwa kutokana na baadhi ya familia kuwakosa ndugu zao waliokuwa wakisafiri kwa meli ya MV Spices  Islander ambayo ilipinduka, kisha kuzama katika eneo la Nungwi kati ya Visiwa vya Unguja na Pemba.Wakati familia kadhaa zikisubiri majaliwa ya ndugu zao wanaoaminika kwamba walikuwa kwenye meli hiyo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), jana ilitangaza kwamba waliopoteza maisha ni watu 197 na kwamba watu 619 wameokolewa wakiwa hai.

 Taarifa hiyo ya SMZ iliyotolewa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud Mohamed inathibitisha kwamba meli ya MV Spices Islander ilikuwa na zaidi ya abiria 610 ambao ni uwezo wake. Kwa takwimu za waziri huyo, imethibitika kwamba ilikuwa imebeba abiria 816.

 Rais Jakaya Kikwete jana aliwatembelea wakazi wa Nungwi kuwapa pole kwa msiba huo mkubwa kwa taifa na kwa mujibu wa Waziri Aboud, mkuu huyo wa nchi alitarajiwa pia kuongoza kikao cha Baraza la Taifa la Ulinzi na Usalama kujadili maafa hayo.

 Kadhalika, Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal pia aliwatembelea wakazi wa Nungwi na pia kuwapa pole wafiwa na walionusurika katika ajali hiyo mbaya.
 

Aboud alisema kati ya waliokufa, 158 walitambuliwa na kuzikwa na jamaa zao wakati maiti 39 hawakutambuliwa hivyo kuzikwa na Serikali katika eneo la Kama, nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

 Alisema Serikali pia imeandaa makaburi mengine 134 kusubiri maiti ambao wanaendelea kuokolewa kutoka baharini.
 

Alisema SMZ imewasiliana na wakuu wa Mikoa ya Tanga, Pemba na Mombasa ili wasaidie upatikanaji wa maiti ikiwa wataonekana katika fukwe za maeneo hayo. “Kesho jioni (leo) tutakuwa na swala ya pamoja kwa ajili ya kuwatakia heri ndugu zetu,” alisema Aboud.

source: Mwananchi 

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...