April 22, 2009

UMATI WAFURIKA KUNG'OA MBEGU ZAO

Sehemu ya UMATI uliojitokeza kijiandikisha ili kung'oa mbegu.
Kulingana na mkataba au sheria waliojiwekea DECI na washiriki wao ilikuwa na hatua tatu, yaani
  1. Kupanda
  2. Kuvuna
  3. Kupanda Milleleeee au kurejesha mbegu shambani.

Sasa kuna ama kung'oa au mbegu kuoza mileleeeeee

MAMA MKUTANONI

Mama amependeza jamani!
Mama Salma Kikwete akiwa na Mke wa Waziri Mkuu wa UK Sarah Brown ktk mkutano wa wake za marais huko USA.

DENSI LA DECI MAELEZO

ilibidi mkutano ufanyike nje.
" Sasa nitafikishia wapi ujumbe wangu?"
"kweli bora tutoke"
"Hatunyamazi bora tutoke"
Afisa mwingine aingilia kati kumtuliza mmoja wa washiriki Mch Temba.
Mabishano kidogo,
Afisa Habari akimtaka kufuta kauli na kufuata press release yake.
a
Alianza vyema akiwa na mwenyekiti wa wastaafu wa EAC
Leo ilikuwa ni patashika pale MAELEZO baada ya anayejiita mwenyekiti wa kamati ya dharura ya washiriki DECI Isaac Kalenge kusema kuwa Pinda karopoka, alitakiwa na uongozi TIS kufuta kauli yake lakini hakuwa tayari ilibidi mkutano uishie hapo na kuamia nje ya ofisi za idarahiyo.

MREMA ANACHEZA RAFU?

Mgombea uenyekigoda wa TLP Joram Kinanda akiwa na mwenyekiti wa Kamati ya Wanachama wa Kunusuru TLP Macmillan Lymo akiwaonesha orodha ya wajumbe feki 42 kati ya 80 wa NEC ambao walishiriki ktk kikao ambacho pia kilimtimua Mutungirei hivi karibuni. WAH. hawa wanadai kuwa Mrema huwa anachukua wasukuma mikokoteni pale Manzese wakti wowote na kuwaita ni wajumbe wa NEC au mkutano na pia ni kuwa hata katiba anatengeneza yeye mwenyewe.
Ktk uchaguzi huu unaokaribia inadaiwa kaarika wajumbe 163 tu kati ya 1200 wa mkutano mkuu na kuandaa morani wapatao 300 kudhibiti atakaye taka kujipeleka huko mkutanoni pasi kuitwa.
Habari ndo hiyo

CRDB KUUZA HISA MIL 125

Mwenyekiti wa Board Martin Mmari (kati) akizindua uuzaji hisa Mil 125 huku Mkurugenzi Dr Charles Kimei na Naibu Mkurugenzi Jens Ole Pedersen wakishuhudia.
Benki ya CRDB PLC imeanza kuuza hisa zake zipatazo Milioni 125 kwa dhamani ya au bei ya kutupwa ya Shs 150 kwa kila hisa moja kuanzia Trh 20 mpaka 8 Mei kabla ya kujiandikisha rasmi DSE hapo Mwezi Juni.

ZAIN NA KENGERE NYEUSI

Zain imezindua huduma ya Blackberry (Kengere Nyeusi) kwa wateja wake wa malipo kabla pia,
Pichani Kaimu Mkurugenzi wa Masoko Kelvin Twissa na Meneja Uhusiano Beatrice Malya Singano wakionesha aina hizo za simu zenye huduma zote za kisasa bila kukosa mtandao wa nguvu na zaidi waweza kuimiliki bure ikiwa unaweza kuwa walipia au watumia muda wa maongezi usiopungua TZS 35, 000/- tu.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...