August 19, 2009

Hili la CCM na UFISADI Limekaaje wadau?

HALMASHAURI Kuu ya CCM juzi ilifikia uamuzi wa aina yake baada ya kuunda kamati maalumu ya kuwashughulikia wabunge wake wanaoikosoa serikali ya chama hicho tawala, huku ikimwekea kinga rais wa serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.
“Bunge limeanza kuwa kama mchezo wa (kikundi cha televisheni cha vichekesho) The Comedy,” alisema katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, John Chiligati wakati akizungumza na waandishi wa habari jana.
“Yaani kila mtu anafanya mambo yake mwenyewe, hali ambayo inaweza kusababisha watu kurushiana hata viatu ndani ya Ukumbi wa Bunge, sasa hali hii maana yake nini? “Kwa hiyo tumesema inatosha, hapo tulipofikia tusiendelee mbele.
Wanaoropoka ovyo ni walevi na tumeona kuna kundi dogo ambalo limejiona kama ni wateule wa kuzungumzia sakata hilo (la ufisadi) bila ya kujua wabunge wote wana haki ya kuzungumzia suala hilo, lakini kwa utaratibu tena kwa kupitia katika vikao vya kamati za wabunge.”
source: mwananchi

ASKOFU MAYALA AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia kutoka Rock City zinasema kuwa Askofu Mkuu Anthony Mayala( 69) wa Kanisa Katoliki Mwanza amefariki dunia leo mchana katika Hospitali ya Bugando alikopokelewa baada ya kuugua ghafla.
Taarifa kutoka Mwanza kwa Msaidizi wake, Padri Renatus Nkwande zilieleza kuwa Askofu Mkuu Mayala aliugua ghafla saa mbili asubuhi baada ya kuishiwa nguvu na alikimbizwa katika hospitali hiyo kabla mauti hayajamkuta saa 8:30 mchana.
“Hatutajua ni nini zaidi maana alikuwa mzima na asubuhi ali-collapse ghafla tukamkimbiza hospitali,” alisema Padri Nkwande ambaye alifafanua kuwa awali Askofu Mayala alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo mara kwa mara.
Alisema Jimbo hilo limepokea kwa masikitiko taarifa za madaktari kuhusu kifo hicho na kuongeza kuwa Jimbo limempoteza msimamizi aliyekuwa wakati wote msikivu wa shida za watu bila kujali imani zao, mcha Mungu, mpole na mnyenyekevu wa kuigwa na kwamba daima hakupenda kupigizana kelele na watu hata kama nafasi yake ingemruhusu kufanya hivyo.
Alisema utaratibu wa mazishi utafanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) kwa kushirikiana na Jimbo hilo na kwamba taarifa zaidi zitapatikana kesho.Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa TEC, Anthony Makunde alithibitisha taarifa za kifo cha Askofu Mayala na kueleza kuwa taarifa nyingine za maziko ya Askofu Mayala zitaelezwa baadaye.Askofu Mkuu Mayala alipata daraja la Upadri mwaka 1970 na mwaka 1979 aliteuliwa kuwa Askofu wa Jimbo la Musoma kabla ya kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza mwaka 1988.
Sisi tunasema Bwana Alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana lihimidiwe.

Chandimu!!

Wengi tumepitia hapa, hata baadhi ya mastaa wamepita pia hapa, na hawa ni kina Ronaldo au Etoo wa kesho wakijaribu huko Sumbawanga kama mdau Peti Siyame alivyowashuhudia leo hii.

Mama Salma na Malkia wa Uswazi

Mama salma kikwete akigonganisha glasi na mke wa Mfalme Mswati III wa Swaziland Malkia Nomsa Matsebula wakati wa chakula cha usiku ambacho mama kikwete alimwandalia malkia huyo,ikulu

Hashim Thabeet alipomtembelea JK Ikulu

JK and HT
Hasheem Thabit and his mother Rukia Presents a basketball Tshirt number one to Presisent Jakaya Mrisho Kikwete at Dar es Salaam State house yesterday afternoon when the president hosted a lunch in honor of the professional basketballer currently an NBA member.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...