January 30, 2009
BREAKING NEEEEEWS... MGONJA AFARIKI
AJARI ZAZIDI KUTUMALIZA BONGO.
Kilio cha Mtu mzima.......
Akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed, ambaye ni Mbunge wa Wawi (CUF), kwa uchungu, Pinda alisema kauli aliyoitumia ni katika kuwahakikishia wauaji hao kuwa Serikali sasa imechoshwa na unyama wanaoufanya na wasidhani Taifa na Watanzania watawavumilia.
“Pengine kuna mtu ambaye hajapata nafasi ya kuonana ana kwa ana na kuzungumza na watu hawa (albino), mimi nimekutana nao nimeona jinsi wanavyoumia (analia), mimi nilisema kuwa wauaji hawa hawawezi kuvumiliwa,” alisema Waziri Mkuu huyo na kukatisha kidogo hotuba yake na kulia.
Huku akifuta machozi, aliendelea kusema iwapo kuna Mtanzania ambaye anaona kuwa ametenda uovu kuliko maovu yote katika suala hilo la albino na iwe hivyo, lakini nia yake ilikuwa nzuri. Alisema alianza ziara yake katika Mkoa wa Tabora, baada ya kupewa kiundani historia ya mauaji hayo ambayo yalianzia kwa vikongwe ambao kwa takwimu alizopewa, waliouawa kwa mapanga walifikia 2,000 kwa sababu za kishirikina.
Alisema wakati mauaji hayo yakiendelea kukemewa, mwaka 2006 yalianza mauaji ya albino kwa kasi ndogo, lakini hadi juzi akiwa katika ziara hiyo, alipewa takwimu kuwa walifikia 28 na wengine watatu wakauawa akiwa bado katika ziara hiyo.
Aliongeza kuwa kwa watu ambao wameyashuhudia mauaji hayo, si mazuri na ni ya kutisha kwa kuwa wauaji wanachotaka ni viungo. “Tukio la Januari 22 wenyewe mliona yule baba wa watu alipokatwa mguu wa kulia na kisha kutelekezwa hapo, damu ilimwagika hadi akafa.” Alisema pamoja na Tanzania kusifika ndani na nje ya nchi kuwa ni nchi yenye amani na utulivu, mauaji hayo sasa yameitia doa nchi.
“Kutokana na mazingira haya, niliamua kufanya ziara na katika ziara yangu nilisisitiza umuhimu wa vyombo vya Dola katika kudhibiti mauaji haya, elimu kusambazwa kwa wananchi, kuongezwa kwa huduma za afya, madhehebu ya dini kukemea mauaji hayo na vyama vya siasa kuungana katika kupambana na tatizo hilo,” alisema.
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
The Himba are an ethnic group of about 20,000 to 50,000 people living in northern Namibia, in the Kunene region (formerly K...
-
Mineral occurrence in Tanzania by TMAA UONGEZAJI WA PATO LA MTANZANIA Mheshimiwa Spika, 46. Lengo la Dir...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...