January 30, 2009

BREAKING NEEEEEWS... MGONJA AFARIKI

CHEDIEL MGONJA ALIYEWAI KUWA WAZIRI KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA KWANZA AMEFARIKI DUNIA LEO HII MUDA WA SAA KUMI NA MOJA JIONI KULINGANA NA TAARIFA ZILIZOTUFIKIA MUDA SI MREFU.

AJARI ZAZIDI KUTUMALIZA BONGO.

Leo hii alfajili.
WATU 15 wamefariki dunia kutokana na ajali ya magari na gari moshi zilizotokea alfajiri ya kuamkia jana katika mikoa ya Dar es Salaam na Morogoro, huku zikiacha majeruhi zaidi ya 20.
Mkoani Dar es Salaam, watu tisa walikufa papo hapo na wengine 10 kujeruhiwa katika eneo la Jet Club Kipawa katika Barabara ya Nyerere wakati mkoani Morogoro, watu sita wamekufa papo hapo na wengine 10 kujeruhiwa katika ajali ya gari moshi mali ya Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) iliyotokea katika maeneo ya Stesheni ya Mzaganza na Kidete katika Wilaya ya Kilosa.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema ajali ya Kipawa ilitokea saa 10 alfajiri ambako gari lenye namba za usajili T700 AFT aina ya Toyota Hiace ‘Kipanya’ lililokuwa likitokea Airport kwenda Tazara, liligonga gari lenye namba za usajili T452 ACP aina ya Scania lililokuwa limeanguka katikati ya barabara na kusababisha kifo cha abiria tisa papo hapo.
Aliwataja baadhi ya waliokufa kuwa ni Ally Issa (37); Michael Maujiro; Augustino Yohana; Elly Athumani; Alfonsi Golesh; Machel Msagira (33); na John Steven.
Alisema maiti zote zimehifadhiwa katika Hospitali ya Amana wakati majeruhi 10 wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Alisema chanzo cha ajali hiyo, Kova alisema ni mwendo kasi wa dereva wa Hiace ambayo ilikuwa imebeba abiria ikitokea Machinjioni Pugu. Alidai imebainika gari hilo lilikuwa linafanya kazi usiku tu kutokana na muda wa leseni yake kumalizika.
Naye Ofisa Habari Msaidizi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI), Mary Ochieng, alisema hali za majeruhi hao zinaendelea vizuri kiasi.
“Tunaendelea kuwapa matibabu…mmoja bado yupo ICU (chumba cha uangalizi maalumu) na tayari tumeshawaruhusu wawili,” alisema Ochieng jana mchana.
Waliolazwa ni Simon Silvesta (27); Eva Joseph (28); Karunde Osambi (32); Zamoyoni Mongera (36); Joshua Jumanne (29), Alex Msuya (65); Emilly Steven (40); Ratibu Abdallah (21).
Katika ajali ya Morogoro, ilitokea saa saba usiku wa kuamkia jana ikihusisha gari moshi lenye namba 8828 likiendeshwa na Richard Mkude (38) kwa kushirikiana na Msaidizi wake Lucas Isaya, wote ni wakazi wa Mkoa wa Morogoro.
Gari moshi hiyo iliyokuwa na mabehewa manne, ilikuwa ikitokea mikoa ya Bara kwenda Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Reli, Yessaya Msigwa, alithibitisha ajali hiyo na akizungumza kwa simu akiwa eneo la tukio, alisema katika mabehewa hayo manne, moja lilikuwa la abiria, jingine lilikuwa tupu wakati jingine lilibeba mataluma yakitokea Wilaya ya Mpanda mkoani Rukwa.
Alisema gari moshi hilo lilipofika Kijiji cha Msaganza, behewa la moja la nyuma liliyumba na kufuatia behewa lililowabeba abiria na baadaye yote kupinduka na kusababisha vifo vya watu hao na majeruhi hao walikuwa wakitoka mnadani.
Kamanda Msigwa aliwataja waliokufa katika ajali hiyo ni wafanyabiashara Said Pindupindu, Seif Bakari, Nassoro Mohamed, Jonas Lukanda, Abbas Kandaro; wote kutoka Wilaya ya Kilosa na mwingine mmoja ambaye jina lake halijatambuliwa.
Aliwataja waliojeruhiwa katika ajali hiyo na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa ni Hamisi Chamwitu; Seleman Mohamed, Sadic Monera, Esta Mbwambo na Asha Hamis ambao ni wakazi wa Mkoa wa Morogoro.
Wengine waliolazwa katika hospitali hiyo ni Edward Athanas, Aziz Seleman ambao ni wakazi wa Dar es Salaam; Hamis Manyeleta, Hamis Selemani, Mecha Jackson ambao ni wakazi wa Wilaya ya Kilosa.
Kamanda huyo alisema miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Kilosa.
Alisema kazi ya kutambua miili hiyo ikikuwa ikiendelea na hadi kufikia jana mchana, miili ya watu watano kati ya sita ilikuwa imeshatambuliwa na ndugu zao na majeruhi wanaendelea vizuri.

Kilio cha Mtu mzima.......

Ukiona mtu mzima analia basi ujue kuna makubwa yamemkuta, hapana shaka aliyokutana nayo au kuyasikia toka kwa waathirika wenyewe yaani Maalbino maalufu kama "kinywa cha farasi" alishindwa kuzuia chozi lake akifafanua kwa waheshimiwa hasa waliomshutuma kuwa alikuwa ameenda kinyume na katiba.

Akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed, ambaye ni Mbunge wa Wawi (CUF), kwa uchungu, Pinda alisema kauli aliyoitumia ni katika kuwahakikishia wauaji hao kuwa Serikali sasa imechoshwa na unyama wanaoufanya na wasidhani Taifa na Watanzania watawavumilia.

“Pengine kuna mtu ambaye hajapata nafasi ya kuonana ana kwa ana na kuzungumza na watu hawa (albino), mimi nimekutana nao nimeona jinsi wanavyoumia (analia), mimi nilisema kuwa wauaji hawa hawawezi kuvumiliwa,” alisema Waziri Mkuu huyo na kukatisha kidogo hotuba yake na kulia.

Huku akifuta machozi, aliendelea kusema iwapo kuna Mtanzania ambaye anaona kuwa ametenda uovu kuliko maovu yote katika suala hilo la albino na iwe hivyo, lakini nia yake ilikuwa nzuri. Alisema alianza ziara yake katika Mkoa wa Tabora, baada ya kupewa kiundani historia ya mauaji hayo ambayo yalianzia kwa vikongwe ambao kwa takwimu alizopewa, waliouawa kwa mapanga walifikia 2,000 kwa sababu za kishirikina.

Alisema wakati mauaji hayo yakiendelea kukemewa, mwaka 2006 yalianza mauaji ya albino kwa kasi ndogo, lakini hadi juzi akiwa katika ziara hiyo, alipewa takwimu kuwa walifikia 28 na wengine watatu wakauawa akiwa bado katika ziara hiyo.

Aliongeza kuwa kwa watu ambao wameyashuhudia mauaji hayo, si mazuri na ni ya kutisha kwa kuwa wauaji wanachotaka ni viungo. “Tukio la Januari 22 wenyewe mliona yule baba wa watu alipokatwa mguu wa kulia na kisha kutelekezwa hapo, damu ilimwagika hadi akafa.” Alisema pamoja na Tanzania kusifika ndani na nje ya nchi kuwa ni nchi yenye amani na utulivu, mauaji hayo sasa yameitia doa nchi.

“Kutokana na mazingira haya, niliamua kufanya ziara na katika ziara yangu nilisisitiza umuhimu wa vyombo vya Dola katika kudhibiti mauaji haya, elimu kusambazwa kwa wananchi, kuongezwa kwa huduma za afya, madhehebu ya dini kukemea mauaji hayo na vyama vya siasa kuungana katika kupambana na tatizo hilo,” alisema.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...