September 20, 2011

CHADEMA YAPETA DHIDI Ya MADIWANI WALOTIMULIWA


MAHAKAMA ya hakimu mkazi Arusha imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa na madiwani watano waliofukuzwa kwenye Chama Cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ambapo imedaiwa kuwa madiwani hao wanatakiwa kulipa garama mbalimbali ambazo zimetumika katika kesi hiyo.

Hapo awali Madiwani hao waliwasilisha pingamizi ambapo pingamizi hilo lilidai kuwa madiwani hao hawakutendewa haki na chama hicho ambapo chama hicho kiliwafukuza .
hayo yamedhibitika leo,(JANA) katika mahakama ya hakimu mkazi ya jiji la arusha ambapo kesi hiyo ilikuwa ikisikilizwa na Hakimu Hawa Mguruta ambapo alisema kuwa alifikia uamuzi huo baada ya kupitia hoja nne za pingamizi zilizowasilishwa mahakamani hapo na mawakili wadaiwa , Method Kimomogoro na Albert Msando na majibu ya wakili wa wadai ,, Severine Lawena .

Katika shauri hilo la madai namba 17 la mwaka 2011 washitakiwa walikuwa ni Chama Cha Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA) na Freeman Mbowe huku wadai wakiwa ni madiwani waliofukuzwa kwenye chama hicho na kata zao kwenye mabano ni Naibu Meya , Estomii Mallah ( Kimandolu) , John Bayo (Elerai), Ruben Ngowi ( Themi), Rehema Mohamed (Viti Maalum) na Charles Mpanda (Kaloleni).

Aidha Hakimu Mguruta alisema kuwa anakubaliana na hoja za mawakili wa wadai kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kuchunguza maamuzi ya chombo binafsi kama ilivyo kamati kuu ya Chadema ambapo walibainisha kuwa chombo chenye mamlaka hayo ni mahakama kuu .

"ni kwamba nakubaliana na hoja kuwa Chadema haiwezi kushitakiwa kwa jina lake kwani jina hilo halina uhai kisheria hivyo haiwezi kushitaki wala kushitakiwa kwa mujibu wa sheria'alieleza Hakimu Mguruta.

Hakimu Mguruta alisema kuwa anakubaliana na hoja ya mawakili hao kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho (Mbowe) hawezi kushitakiwa binafsi alipaswa kushitakiwa kwa nafasi yake ua Uenyekiti wa Taifa vinginevyo hataweza kutekeleza maelekezo ya mahakama hiyo ndani ya Chadema

“Mbowe alipaswa kushtakiwa kwa nafasi yake ya uenyekiti wa Taifa kwani endapo ataondolewa kwenye nafasi hiyo au kujiuzulu hataweza kutekeleza maamuzi ya mahakama kwani hataweza kuendesha na kusimamia maamuzi ya vikao ndani ya chadema” alisema hakimu mguruta .

Katika hatua nyingine Hakimu huyo alikubaliana na hoja kuwa kesi hiyo imefika mahakamani hapo ikiwa imepitwa na wakati kwani tayari madiwani hao walishakata rufaa kwenye baraza kuu la Chadema hivyo kesi hiyo imepoteza maana huku akiongeza kuwa mahakama kuu ndiyo yenye uwezo wa kupitia maamuzi yaliyofanywa na na vikao ndani ya taasisi lakini haiwezi kuhoji au kuamua juu ya taratibu za ndani za chama husika .

Wakati maamuzi hayo yakitolewa madiwani watatu kati ya watano waliofungua kesi hiyo walikuwa mahakamani hapo ambao ni Diwani wa kata ya Elerai Bw John Bayo , Naibu Meya wa jiji la Arusha ambaye pia ni diwani wa a kata ya Kimandolu, Bw Estomih Mallah ambapo walipotakiwa kutoa maoni yao mara baada ya kikao cha mahakama kumalizika walisema kuwa hawana maoni ya kuongea na vyombo vya habari. .

Aidha iliwabidi madiwani hao waliofungua kesi hiyo kusubiri ndani ya chumba cha mahakama mpaka mashabiki hao wa Chadema walipotoka nje ndipo nao wakatoka ingawa waliendelea kukaa kwenye maeneo hayo ya mahakama mpaka wanachama hao walipoondoka kwa maandamano na mbunge wa Arusha Mjini , Godbless lema .

Hata hivyo katika hatua nyingine polisi wenye silaha na mabomu ya machozi wakiwa kwenye magari mawili ya Polisi yenye namba za usajili PT 1844 na PT 0746 walifika na kuwaamuru wanachama hao kutawanyika mbele ya jengo la ofisi za mkuu wa wilaya ya Arusha zilipo ofisi za mbunge huyo ambapo walitii na kuondoka .

Story kwa hisani ya Full Shangwe Blog

JK APEWA TUZO.

Rais Jakaya Kikwete akipewa tuzo na Waziri Mkuu wa Antigua and Barbuda Mh. Winston Baldwin Spencer  kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya afya, teknolojia na maendeleo kwenye hafla ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na taasisi ya South-South katika hoteli ya Waldorf Astoria jijini New York.

Vimbwanga Igunga - Mbunge CCM: Tukishindwa nakunywa sumu



KAMPENI za uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga, zimezidi kupamba moto baada ya Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), kujiapiza mbele ya wananchi kuwa atakunywa sumu iwapo chama hicho kitashindwa kwenye uchaguzi huo.

 Akizungumza na wanakijiji wa Ugaka kwenye kata ya Nkinga wilayani hapa wakati akimwombea kura mgombea wa CCM, Dk. Peter Kafumu, Lusinde alisema kutokana na mwenendo mzuri wa kampeni za CCM na jinsi wanavyowafikia wananchi, haoni sababu za kushindwa kwenye uchaguzi huo.

 “Hapa nimewaona waandishi wa gazeti la Mbowe (Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA); nataka mkaandike kwa namna ambavyo tumezunguka, CCM tukishindwa nakunywa sumu,” alisema na kuongeza:

 “Nataka tuwaambie, tutawapiga bao la mbali kabisa na huyo Dk. Slaa sisi tunammudu ndiyo maana tukamwambia Mzee Kikwete, endelea kuongoza nchi atuache vijana tumkabe koo maana yule mzee ni mnafiki mkubwa,” alisema Lusinde.

 “Kale kazee kagonjwa kale, ndiyo maana nimekuja kuwaambia inawezekana viongozi wa CHADEMA wanavuta bangi, zile bangi zile, haiwezekani unatembea nchi nzima unahamasisha vurugu, unatangaza vita,” alisema Lusinde Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM.

 Kwa upande wake mratibu wa kampeni hizo, Mwigulu Mchemba, aliwataka wananchi hao kumchagua Dk. Kafumu na kusema wanasiasa wa upinzani wanasema tangu uhuru serikali ya CCM haijafanya kitu kabisa, Igunga haijapata maendeleo wakati si kweli.
 

“Wenzetu wanapandikiza chuki kwa vijana wa vyuo vikuu nao wanakubali kupotoshwa na wanasema serikali ya CCM haijafanya kitu si kweli. Kwanza idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu imeongezeka halafu wanasema Rais huyu hajafanya kitu, kama si kulaaniwa ni nini?” alihoji.

 Alisema wapinzani wanatumia umaskini wa wananchi kama mtaji wa kisiasa, wamelalamikia kupandishwa kwa bei ya pamba ili watu wakasirike na kutoichagua CCM.

 “Wacha niwaambie wakati wa ukame serikali ya CCM iligawa chakula jimbo lilipokuwa wazi wakasema tusigawe chakula eti hiyo ni rushwa sasa tusipogawa chakula mtatuchagua? Hivi njaa ina likizo? Kwa nini serikali ipeleke chakula mpaka Somalia lakini Igunga ibaki na njaa hivi mtapiga kura mkiwa na njaa?” alihoji Mwigulu.

Source: Tanzania Daima.

Nani wanahujumu Sukari???


 Kampuni Kilombero yashangaa uhaba wa sukari


KAMPUNI ya Sukari Kilombero imeshangazwa na nchi kukumbwa na uhaba wa sukari, ikisema kuna hujuma kwenye usafirishaji nje ya nchi bidhaa hiyo, kwani kwa miezi mitatu Tanzania imekuwa ikilisha sukari Kenya.

 Imesema yenyewe huzalisha sukari ya kutosha kwa wastani wa tani 500 kwa siku na kuwapa mawakala wake, lakini kuna watu wanauza nje ya nchi ambako sukari ina bei maradufu ya bei ya ndani ya nchi hali hiyo inachangia uhaba huo.

 Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni hiyo, Bashir Harun, alimweleza hayo Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe alipotembelea kampuni hiyo Dar es Salaam kufahamu hali ya uzalishaji na usambazaji wa sukari.

 Harun katika kuthibitisha hujuma katika usambazaji wa sukari, alisema wapo wafanyabiashara wanaoingiza fedha katika akaunti ya kampuni hiyo kwa lazima wakitaka sukari.

 Alisema kitendo hicho kiliwalazimu kuandikia benki zote barua kuzizuia kupokea fedha ili kuhakikisha mikoa yote inapata sukari kupitia mawakala wake.

 Alisema muda kama huu, kiwanda chake huwa na sukari ya ziada, lakini mwaka huu hakina kutokana na kuwa yote inauzwa, akitolea mfano wa mwaka jana ambapo mwezi kama huu walikuwa na ziada ya tani 18,500.

 “Kinachotakiwa Waziri ni kufanya kazi kwa ushirikiano na kuanzia leo nitakupa kiasi kilichozalishwa na kila wakala amechukua kiasi gani cha sukari ili kumfuatilia anaipeleka wapi na anaigawa vipi,” alisema na kuahidi kumpa Waziri orodha ya wasambazaji na mawasiliano yao.

 Aliwataja baadhi ya wasambazaji anaowapa sukari kwa kila mkoa kuwa ni Iringa (Kaundama Store), Morogoro (MA Traders,Thabit Islam, Alnaeem na Mohamed Enterprises).

 Wengine ni Mtwara (MA Abdurazack), Mwanza (VA Shah), Mbeya (Tugimbane), Shinyanga (Alneeem na Mohamed Enterprises) na Dodoma (Mnary na Anthony Alex) na Dar es Salaam (RTC, Mohamed Enterprises na wengineo).

 Harun alisema huwauzia kilo 50 za sukari mawakala hao hadi Dar es Salaam kwa kati ya Sh 82,600 na Sh 85,000 huku bei ya kiwanda ikiwa Sh 80,004.

 Waziri Maghembe alisema kuanzia leo watafuatilia magari yote kutoka kiwandani mpaka yanakokwenda kwa kutumia watu maalumu na atakayegundulika sukari aliyotoa kiwandani haijawafikia wananchi, atafutiwa leseni.

 “Baada ya kuwafutia leseni nitawapa taarifa viwanda vyote kutomwuzia sukari tena kwani haiwezekani kuzalisha sukari kwa ajili ya nchi jirani huku wakisafirisha bila leseni, kwani Serikali haijapata kutoa leseni ya kuuza sukari nje,” alisema Maghembe.

 Alisema ni lazima kufahamu sukari inakwenda wapi na nani anaipeleka, kwani Serikali haitaki sukari ya nje kuingia nchini, ili kulinda viwanda visife, kwani hali hiyo itakuwa haiwatendei haki Watanzania.

 Alisema kwa msambazaji ye yote atakayepakia mzigo na akashindwa kusema anakoupeleka, sukari hiyo itachukuliwa na Serikali lengo likiwa ni kuifikisha kwa mlaji.

 Aliwataka wananchi kupiga simu namba 0754-387928 kutoa taarifa za watu wanaohodhi sukari kwenye maghala au kuuza nje ya nchi na watoa taarifa watapewa zawadi.

source: Habari Leo,
Picha na Leonald Magomba

ARV zaotesha matiti wanaume?????

TANZANIA: Man on ARV develops abnormal breasts



Some Tanzania men on anti-retroviral (ARV) drugs have experienced abnormal breast enlargement similar to that of women. There are even cases where women taking the life prolonging drug against HIV complaining of queer side effects including becoming disabled.

 Joseph Mkanda, 43, one of the victims, said he developed strange symptoms plus growing breasts after taking the drugs. Initially, he suspected the cause to be lack of a balanced diet. But he soon realised that the main problem was the type of drugs he was taking.  

“I feel very much ashamed to go out of my house, because I have developed breasts like a woman. …I fear that other people would laugh at me,” he said from his Mtwara-base.  



“I went to one of the medical doctors in my village, who told me that such signs were normal for people suffering from AIDS who have been taking the drugs for a long time. At the moment, I don’t know what to do or where to go,” said Mkanda.  

Salima Omar, 36, from Mtwara said she developed strange symptoms after taking the drugs. Salima, a mother of seven, said one of her daughters died shortly after birth in 2006 when she had undergone the HIV test.

 Changes in body  One of her sons is also HIV positive and has been taking ARV drugs since October 2007. She explained they had both been taking the drugs, but due to unknown reasons, she started noticing changes in her body.  

But she believes the changes were caused by the fact that she has been unable to follow the instructions of taking the ARVs. She said the drugs were very strong and required the users to get a balanced diet. But Salima was unable to follow the instructions and at times stopped taking the medicine.  “These drugs are very strong; if you take them without enough food you become very weak.

But there are days when I'm forced to take them without eating anything, especially when I get seriously sick.

In other words, I take the medication irregularly,” she explains. The family lives off the earnings of her husband who repairs bicycles.  After spending on alcohol, which Salima admits she likes very much, there is little left to support a big family like theirs, especially for buying food. Actually, she has been forced to sell all the family goats in order to keep the family alive. 

 Like many families in Mtwara District, Salima’s has been experiencing food shortage since 2007, a situation complicated by the recent long drought in the district, forcing many people to survive on only one meal a day.  She feels very weak on days she does not take the medication.

“I have even started developing some complications …I believe it is due to my inconsistency in taking the drugs. My left side is developing rashes, and I suffer much pain," she says.  Despite her HIV-positive status, Salima had until recently insisted on having more children. Three months ago she gave birth to twins. One died, and the other is very weak.

While pregnant, Salima’s doctors gave her treatment to prevent transmission of the virus to her babies.  Hassan has agreed they will not have more children, although Salima is not convinced. She particularly dislikes his refusal to use a condom when having sex.  There is no alternative to taking ARVs by HIV positive persons, even though it is challenging to adhere to the treatment because of lack of resources to get proper diet.



Dr Kawambwa awakejeli walimu Nchini


SERIKALI imesema walimu nchini wangekuwa wanatumia nguvu kubwa wanayotumia hivi sasa kudai posho na malimbikizo yao, wangeitumia madarasani matokeo mabaya yangekuwa ni historia.

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya uUfundi, Dk Shukuru Kawambwa, alisema hali ya ufundishaji madarasani hivi sasa hairidhishi kutokana na baadhi ya walimu wamekuwa hawatilii mkazo kanuni, taratibu na sheria ya maelekezo ya ajira zao. 

Alisema kutokana na hali hiyo, hivi sasa Serikali hairidhishwi na utendaji kazi wa baadhi ya walimu, kwani licha ya jitihada za kuhamasishana bado wanatumia nguvu kubwa kudai posho na malimbikizo mbalimbali na kwamba, wangetumia kasi hiyo madarasani matokeo mabaya yangekuwa ni historia. 

Dk Kawambwa, ambaye pia ni Mbunge wa Bagamoyo, alisema hayo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza Shule ya Msingi Milo huku akionyesha kutoridhishwa na hali aliyoshuhudia, kwani licha ya kuwapo wanafunzi 151, hakuna vitabu na miundombinu ni mibovu. 

Kitu kingine kilichomshangazwa, ni zaidi ya mwaka mmoja hakuna mahala panapoonyesha kuna maofisa wa elimu wa wilaya au wakaguzi waliowahi kutembelea shule hiyo hata mara moja.

 “Kwa kweli sijaridhishwa kabisa na hali hii niliyoikuta hapa, wanafunzi wapo 151 hawana vitabu, shule ina hali mbaya na zaidi kinachochefua hakuna kumbukumbu ya maofisa elimu au wakaguzi waliowahi kutembelea hapa hata mara moja,” alisema Dk Kawambwa na kuongeza: 

“Pia, nimepata picha halisi kuwa ni dhahiri kuna pengo kubwa la mawasiliano baina ya maofisa elimu, wakaguzi wa elimu na hata maofisa elimu wa mkoa siyo kwa Bagamoyo tu, inawezekana hali ni hii nchi nzima  kwa walimu wa shule za pembezoni mwa wilaya.”

 
Alikitaka Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kuongeza kasi ya kuhamasisha wanachama wake kutimiza wajibu wao, kwani kazi ya ualimu ni ngumu na inahitaji mtu ambaye ana wito wa pekee, hivi sasa wengi wao hawatimizi majukumu yao ipasavyo.

 Pia, kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Milo, Dk Kawambwa aliwataka kuwa na moyo wa kujitolea kujenga nyumba za walimu na kuahidi Serikali kuwaunga mkono, ili kupunguza tatizo la walimu kukaa mbali na vituo vya kazi.

Source Mwananchi

Burundi please do start it again!

Agathon Rwasa FNL and President Pierre Nkurunziza hugs after signing peace agreement in Dar es Salaam in 2006. Photo by Bernard Rwebangira


AN OFFICIAL in Burundi says attackers from neighbouring Congo have killed 36 people at a pub in the central African nation.


Bujumbura province governor Jacques Minami said the attackers descended on the pub west of Burundi's capital last night.


He says the attackers had crossed the river from Congo.Survivor Jackson Kabura, who was wounded in the stomach, said the men entered wearing fatigues.

He says: "One of them said, 'kill them all, kill them all. Make sure there's no survivors'."
President Pierre Nkurunziza has declared three days of mourning.


Burundi suffered a 16-year civil war that only ended in 2009 when its remaining rebel groups demobilised.
Source: Daily Record

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...