November 24, 2011

GAMBA LAGOMA


UTEKELEZAJI wa mpango wa CCM uliolenga kuwashinikiza watuhumiwa wa ufisadi kuachia nafasi zao za uongozi ndani ya chama hicho, umechukua sura mpya na sasa Kamati Kuu (CC) inaomba ipewe kibali cha kuwachukulia hatua zaidi wale ambao wamegoma kujiuzulu.Juzi, katika kikao chake mjini hapa, CC iliazimia kuomba idhini ya Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM ili ifanye kazi hiyo baada ya kuwepo ukimya ambao unaashiria kutokuwepo viongozi na makada ambao wako tayari kujiuzulu nyadhifa zao kwa hiari.

Tangu kupitishwa kwa mpango huo maarufu kwa jina la kujivua gamba katika kikao cha NEC kilichopita cha Aprili mwaka huu, ni kada mmoja tu, Rostam Aziz aliyechukua hatua za kujiuzulu ubunge wa Jimbo la Igunga na ujumbe wa NEC, lakini wengine wamekuwa kimya hadi sasa.

Katika kikao cha Aprili NEC hiyo ya CCM ilipitisha maazimio 26 lakini kubwa ni lile lililokuwa likihimiza vita dhidi ya ufisadi kuendelea na kutoa mwito kwa watu wanaotajwa na jamii kuhusika na ufisadi ambao wako ndani ya chama kujitathmini kisha kuchukua hatua za kuachia madaraka waliyo nayo.

Sehemu ya mwisho ya azimio hilo inasomeka: “Wasipoachia madaraka chama kiwachukulie hatua mara moja.”

Mmoja wa wajumbe wa CC ambaye ameomba jina lake kuhifadhiwa alisema: “Tunawaomba NEC waturuhusu jambo hili tulifanyie kazi sisi (CC) na litafanyiwa kazi kupitia taratibu za kawaida za chama kwa kuzingatia kanuni na taratibu za maadili za chama hicho.”

Kubadilika kwa utaratibu wa kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi, kulipokewa kwa shangwe na wafuasi wa watuhumiwa hao ambao wanasema kulikuwa na ajenda ya siri, kubwa likiwa ni vita ya urais wa 2015.

Hata hivyo, kada mwingine ambaye yuko karibu wa vigogo wa chama hicho alisema: “Hivi sasa hali itakuwa mbaya zaidi kwa watuhumiwa, tunakokwenda si hiari tena itakuwa ni lazima ikiwa chama kitawapata na hatia.”

“Ujue azimio la kwanza lilikuwa na pande mbili, kwanza ni watuhumiwa hao kujipima wenyewe kisha kuchukua hatua, lakini pili ni upande wa chama, sasa ukomo wa upande wa kwanza ambao ni kuchukua hatua wenyewe umekwisha, sasa ni zamu ya upande wa pili ambao ni wa chama,” alisema kada huyo ambaye pia ni mshiriki wa vikao vya uamuzi ndani ya CCM.

SOURCE: Mwananchi

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...