June 11, 2010

Comments/maoni mbalimbali ya wadau

Wadau nimeona niwashirikishe comments za wadau mbalimbali juu ya picha hii ambazo ziko kule kwenye facebook. haya ni maoni yao na si BP

John Badi
John Badi
Duuuuuuuuuuuuuuuuuuuu.............!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!?
Tuesday at 2:58pm ·
Subi Nukta
Subi Nukta
this is absurd, to say the least. I am trying to think through but I there is nothing whatsoever that answer the questions I have. That we are expecting to see teachers working to their utmost ability in delivering the best in education? aren't we even ashamed of asking any result(s) from this teacher - who apparently is a representative sample of many - who doesn't have a life to begin with? Stupidity comes in many forms, and some of our decision makers are stupid, I really do not care how many schools they've attended or degrees they have, if it doesn't help alleviate the problem, it's plain useless, ignorant and stupid. What good does it do having education but not be able to convert and apply it into real life situations? Plain stupid! blame it on poor and unrealistic planning = stupid. And unless we come out of this stupidity, we are bound to seeing the same thing over and over.
Tuesday at 6:04pm ·
Richard Mulonga
Richard Mulonga
This is a good shot, telling a good story about the plight of a teacher! But I wonder what society expects from a service provider like this one who is ill-motivated and living in a sham of a house?
Tuesday at 6:10pm ·
Fadhy Mtanga
Fadhy Mtanga
Hivi zile bilioni tatu sijui saba zilizoileta Brazil zisingeweza kuiokoa hii? Mtaniona mie mshamba sijui michezo, potelea mbali....lakini tunatumia pesa nyingi ktk mambo yasiyo na ulazima na kuyadharau yale yenye ulazima...unadhani mwananchi huyu mtumishi wa umma anaitafsirije serikali yake inapofuja pesa pasipo kumjali yeye? Unadhani ataipenda nchi yake kwa moyo wote...hivi kuna mtu na akili zake atamwambia mwananchi huyo aimbe 'Tanzania nakupenda kwa moyo wote, nilalapo nakuota wewe."?
Tuesday at 6:18pm ·
Beda Msimbe
Beda Msimbe
Nukta 77 naweza kabisa kutokukubaliana nawe na naweza kabisa kukubaliana nawe.Sisi binadamu ni wavivu mno wa kufikiri.Dunia iliyojaa tope la Mungu, huyu mwalimu lazima awe na kasoro za kufikiria kukaa katika sebule hii ili iweje hasa? Kamchezo gani haka yaani mimi bwana huweza kusema fyuu huu ni upuuzi.Unaweza kutengeneza nyumba nzuri ya tope yakuishi kama tembele la wagogo, lakini pia unaweza kuwauliza wananchi wasiotaka kuwapa mazingira mazuri walimu wao wanaofundishia watoto wao?Huu uvivu wa madiwani au wananchi wenyewe., Hivi unasubiri mtu akuletee maisha nyumbani kwako? Mbona wachaga hawana nyumba za walimu za kijinga kama hizi. Tupeane heshima jamani mwingine ni umbumbu wa fikira na ujinga wa mawazoi. Hii ama hakika hotuba
Tuesday at 8:04pm ·
Subi Nukta
Subi Nukta
kwa hivyo unamhamisha mwalimu ukampa nyumba mbovu ili aijenge na kuiboresha aishi humo, kwa mshahara upi? marupurupu tu ya uhamisho anazungushwa miaka miwili, seuze kudai malipo ya kukarabati nyumba? huo muda wa kukarabati nyumba mwanafunzi anafundishwa na nani? au atakarabati siku za wikiendi, kwa hivyo familia yake haihitaji? hao viongozi wakihamishwa mbona huwa wanapewa fedha ya kukarabati nyumba (hadi kufikia Bilioni ngapi sijui, rejea nyumba ya gavana na Spika na Mawaziri wengine) au kwa kuwa wao kazi zao za maana zaidi ya hii ya ualimu ambayo wamepitia? Askari je? Wafanyakazi wa sekta ya afya? wao wote wakaanza kukimbizana na mafundi muda wa kazi? Hebu tufike mahali tuheshimu makazi na malazi ya watu kwani huchangia sana kwa mtu kuweza kufanikisha (au kutokufanikisha) jukumu lake. Nina hakika mwalimu huyu angejua kuwa atalipwa fedha atakayoitumia kukarabati nyumba aliyohamia, asingekuwa na uvivu wa kuagiza mafundi wafanye hivyo, shida iliyoko, hatalipwa na hilo ndilo lililowakatisha tamaa waalimu wengi, nazungumza hivi kwa mfano hai wa ndugu zangu waalimu 6 walioahmishwa na kukumbwa na adha hii, mmoja amehamishwa mwaka 1992 hadi leo hajarejeshewa fedha zake pamoja na kuwakilisha risiti zote halali za ukarabati wa pango.
Tuesday at 8:14pm ·
Beda Msimbe
Beda Msimbe
Usiwe na jazba Nukta 77 ni ukweli wa kupima, kwamba hatutumii akili zetu kulinda afya zetu.Sisemi walafi waliopo serikalini wanaofanya maisha ya wengine kuwa magumu. Lakini nataka kusema yapo makosa mengi yamefanywa na hila za mwanadamu wala si serikali! Waliuza nyumba za mpaka majaji sasa majaji wanalazimika kuishi katika mahoteli waliuza nyumba za mpaka wakuu wa polisi sasa wanahaha. Yapo makosa ya msingi kabisa yamefanywa na hili siwezi kulibishia. Ninachobishia ni matumizi ya akili. Tazama hiyo nyumba, tazama wanavijiji tazama na mwalimu mwenyewe hili ndilo ninalotaka kusema Bibi wa Calcutta, thereza, alisema kwamba tusitegemee serikali kwa kila kitu namimi naweza kusema wazi kabisa tusitegemee. Ukienda vijijini, natembea sana huko pity! kweli nakuambia pity manake mtu anachotaka ni serikali hili serikali lile hata kufukua mfereji anataka serikali mradi mkubwa unaharibika serikali haina bolti ya kufungia bati la kwenye mfereji. Mimi nabishia ukweli hivi tukoje hasa
Wednesday at 10:14am ·
Subi Nukta
Subi Nukta
@ Beda, iko haja ya kubwa ya kuhakikisha kila mtu katika nchi hii anatimiza wajibu wake, Mwananchi na Kiongozi, ilivyo sasa, kila mmoja anaona yeye hastahili kuambiwa na mwingine la kufanya; na huu uzembe unaosababisha na kuoneana haya, heshima na adabu za woga, upendeleo, rushwa na tuhuma za ngono/uzinzi/uasherati vitaendelea kututafuna natutabaki kwenye dimbwi la umaamuma hadi siku tutakapojua kutia adabu katika kazi na kila mtu kujituma na kuwajibika kwa mujibu ya misingi ya kazi. Nimekusoma vyema. Ninauchukia uvivu. Ninauchukia uzembe. Inakera kiongozi anaposhindwa kumwajibisha mwananchi il hali amepewa dhamana ya kufanya hivyo, inakera zaidi kiongozi anapozembea na kutokutoa haki kwa Mwananchi. Hii nchi hii?! we ngoja.
Wednesday at 10:22am ·
Bernard Rwebangira
Bernard Rwebangira
@ Beda, Subi and all, ukweli hali inatisha, hii ni picha moja tu kati ya photo story kuhusu makazi ya walimu vijijini, hiyo nyumba ni ya tope si ya kulekebisha labda kuvunja na kujenga upya, hawa ni wanataaluma ambao huduma yao sote tumeipitia, simjui ambaye leo hii anadaia amesoma ama alienda shule lakini hakuwai kupitia chini ya mikono ya mwalimu, nasema tena simjui mtu huyo kama yupo. Natambua fika jazba zako Da Subi, una kila sababu ya kuwa na jazba, sijui ingekuwaje kama ungeonana nao walimu hawa walokata tamaa ya maisha uso kwa uso, ungelia sana labda, nathani ifike wakati kama taifa tutambue vipaumbele vyetu ni nini, mi sijui ni vipi ata sasa, anayejua atujulishe wadau.
Wednesday at 1:17pm ·
Beda Msimbe
Beda Msimbe
ni sawa na kusema kwamba daktari lazima apewe kipaumbele,polisi je? tumezoea sana kulialia lakini hatuonyeshi nini dawa ya tatizo letu.Wakati fulani nilimwambia mtu mmoja haya turejeshe fedha zote zilizoporwa.Tujenge majengo si ndio tunachotaka? ndio si ndio! lakini nambie je ndio tutakuwa tumemaliza tatizo? Mimi ninachosema ambacho nabishia ni kweli kwamba kila kitu lazima kifanywe na serikali?Sisi tunafanya nini? Tunazungumzia wabunge kuwa na mishahara mikubwa, sawa kabisa wanayo mikubwa so! manake wakati fulani tunatafuta kubebesha lawama tu kwanini hatufanyi mambo yanayoeleweka bali kulalamika tu? hata huyu mwalimu naye amekaa hapa miaka mitano anashindwa kushawishi watu kuwa na eneo zuri la kuishi? moja ya dhambi kubwa ya mauti ni kukata tamaa padri wangu mmoja aliyenisaidia kufika hapa na kufikiria alisema. Kukata tamaa ni dhambi kubwa inamfanya mtu kufa kabla hajastahili kufa . haya tuache hayo ukifikoa vijijini si walimu pekee wenye hali inayotia hasira wapo watu wa ugtaniw anaiosaidia wakulima kulima vizuri. msiseme etui nania mbaye hajapityia kwa mwalimu! nambie nani ambaye hajala chakula,hajaenda mhhh manake vyote hivyo vipo kwa sababu watu wanafanya wajibu wao. je dawa n i kuonyesha nyumba zinazofanana na feki. Mimi nasema si lazima serikali kufanya yote lakini kama tuna utaratibu tunaweza kufanya yote na serikasli ikabaki wimbo tu by the way nani ni serikali
Wednesday at 4:08pm ·
Abel Ngapemba
Abel Ngapemba
Beda nakuunga mkono. Jana nilikuwa ktk mkutano wa mashauriano pale Movenpick, mtu mmoja akasema ”in Japan everybody is a think tank...in Tz viongozi ndo think tank, like Director Generals even if they don't have direction. Kila kitu tunasubiri kuambiwa, kupewa n.k. Jeshini tumejenga nyumba za makamanda na hata mahanga yetu, tumefyatua matofali, tumechoma moto. Gharama ya serikali ilikuwa kidogo sana. Shule niliyosoma almost 80% ya chakula tulikuwa tunalima wenyewe. Problem yetu we are not creative, hatuoni vitu muhimu exposed to us till they are gone. It is through stadi za kazi that poor teacher can have good house and ofcourse furniture. Awafundishe watoto kufyatua tofali, kujenga...he has manpower though pupils
Yesterday at 7:49am ·
John Badi
John Badi
Weee Ngapemba acha 'ufisadi' weweee! hivi unajua mshahara wa mwalimu? halafu ni muda gani afundishe na muda upi afyatue matofari na ni muda upi ajenge? Au unataka watoto wetu ndo watumike kufanya hizo shughuli je watasoma saa ngapi? Ukizungumzia Jeshini ni sawa kwani JKT ukienda zaidi ya kwata shughuli kubwa ndio hiyo wala hakuna concetration yamasomo acheni hizo jamani kwani wanaoathirika na hali hiyo ni watoto wetu wenyewe...... Sina maana tuilaumu serikali la hasha bali na wadau mbalimbali wajitokeze ku-support kama ambavyo baadhi wanafanya hivyo.
Yesterday at 8:15am ·
John Badi
John Badi
Zamani wakati sisi twasoma P/school tulikuwa tunafyatua matofali, tunalima na nk. na ukikosa unatandikwa bakora hadi matako yanakuwa ya BLUE lakini sasa hivi ni tofauti, ukimwambia mtoto afyatue matofali au kumchapa viboko ni nongwa wazazi wanakuja juu.
Yesterday at 8:21am ·
Abel Ngapemba
Abel Ngapemba
Badi, nikiwa shule ya msingi nimefuga nguruwe, nimefanya bustani, uselemala nk. Sekondari nimejenga mifongo [mifereji], bustani nk kupitia what was called clubs na ilikuwa only two hrs a week. Tulikuwa tunalima na kufuga, chakula pekee kilichokuwa kinanunuliwa na mchele na maharagwe na kazi hizi tulikuwa tunafanya saa moja kila kitu, yet Maua wasalways among the first five performer kimasomo. Leo hii I don't buy vegetables kwa sababu ninabustani, ninamahindi ambayo anytime I want navuna, ninakuku wa kienyeji mayai siyo kwa ajili ya biashara bali matumizi ya home. Hizo kazi ni practise of what you are taught theoritically
Yesterday at 8:43am ·
John Badi
John Badi
Ni kweli... Nipo pamoja nawe mjomba hizo zilikuwa ni salamu tu mjomba...
Yesterday at 9:02am ·
Abel Ngapemba
Abel Ngapemba
Nataka mtoto wangu ajifunze, siyo darasani tu bali kwa vitendo. Mambo ya wadau kusupport hayana msingi tunawafundisha watoto kuwa tegemezi. Yes huna nyumba bora kama huyo mwl, basi unakaa na kupoteza nguvu kuomba msaada! Pse do sthing, THINK on how to remove the barrier. Matatizo yapo kutupa changamoto tuweze kufikiri na kuendelea. Tuwe na malengo kwamba kila siku nitafyatua tofali 10 badala ya kunywa pombe "kupoteza mawazo“ kumbe tunapoteza akili
Yesterday at 9:03am ·
John Badi
John Badi
Kweli kabisaaaaaaa... kwanza huyu mwalimu anaonekana cha pombe huyuuu... jamani hata kukanda tope tu asilibe chini yaani sakafu iwe levo anashindwa? Hapana! mimi nahisi hapa hapakuwa maskani yake labda walimkuta kilabuni... mimi nikiwa mtumishi wa serikali enzi hizo niliwahi kuhamishiwa na kufanya kazi ktk wilaya ya Newala takribani kwa mwaka mmoja na nilibahatika kutembelea katika vijiji karibia vyote kwa kuwa mwisho wa mwezi tulikuwa tukipeleka mishahara ya walimu sikuwahi kuona 'makazi ya walimu ya aina hii' ni kweli tulikuta wakiishi ktk nyumba zenye hadhi sawa na wanakijiji wengine lakini hii kiboko!
Yesterday at 9:13am ·
Emertus Chibuga
Emertus Chibuga
Hali mbaya sana hii. Kuna mabilioni ya uchaguzi lakini kuna vijisenti katika kuendeleza elimu. Ndiyo Bongo hiyoooo
Yesterday at 10:26am ·
Beda Msimbe
Beda Msimbe
kuna gharama ya demokrasia kaka wacha masikhara! gharama yake ni kubwa kama kichwa chako kinavyokuwa kikubwa katika kutatua matatizo ambayo kimsingi hayapo lakini mwenyewe unayaendekeza. Mtu unakaa kwenye udongo bomba wa kufanyia kazi na hata kama ukiamua kufyatua tofali 100 kwa wiki bado katikia nusu mwaka unaweza kuwa na tofali za kutosha kwakufanyia kazi lakini sisi tumekuwa watu wa kusubiri ndio maana nchi hii imejikita katika kuombaomba tu afadhali ya matonya anayefanya kitu cha maana kwa kuomba. Tunaombaomba tu, lakini cha msingi hakuna kabisa. Swala la kuharibikiwa hata hatulifikirii zaidi ya wapi mdako upo tukacheze, wapi bibo lkipo tukalinywe na halafu matangazo mengi walimu wana shida ya nyumba? ha ha ha kama kweli nilivuna shairi usiku kwa kutumia taa za scania pale mafinga, tukjaokoa msitu wa mabilioni bila kuwa na vifaa vya zima moto kwa kutambua kwamba katika mita zaidi ya 50 tukioa viunganisha upander wa pili hautafikiwa na moto na sao hili mwaka huo ukapona.Tukawa katika elimu ya maarifa ya nyumbani nikajifunza kupika chapati na vitumbua. Mimi mluguru bwana lakini nilijua mivyakula ambayo kwetu haiko kupitia maarifa ya nyumbani. Hivi mara moja kwa wiki watu wakajifunza kutengeneza tofali na kuzichoma hatujapa kwelikweli tofali za nyumba ya mwalimu na maktaba. acheni hizo. Kwanza tusilinagnishe gharama za demokrasia na ukweli halisi tutachanganyikiwa.
Yesterday at 12:40pm ·
Subi Nukta
Subi Nukta
Hii nchi hii, hii nchi upuuzi mwingi sana, tangu ngazi ya viongozi hadi ngazi ya wananchi. Ukiwaona wananchi wanaofanya mambo ya kipuuzi viongozi wao wanatoka mumo humo, usitegemee watakuwa hawana upuuzi kiasi cha kuwatosha. Huyu mwalimu (na wengine wa staili hii) wameshindwa vipi kuwajibishwa na viongozi wao? tatizo tunapozungumzia viongozi, kila mtu ana-shoot kwenye viongozi wakubwa wa Serikali, tunasahau kuwa huyu mwalimu kama akili yake haijamwongoza kufanya mabadiliko, ndiyo sababu akawepo Mwalimu Mkuu atakayeuliza kulikoni mwalimu Massawe unaishi kwenye hali hii. Mwalimu Mkuu naye akiwa mzembe, yupo anayemfuatia, sijui kama ni Afisa elimu wa Kata, Tarafa, Mkoa au vipi. Hao nao wakizembea, wapo Wakaguzi wa elimu, sijui kuanzia ngazi gani hadi ngazi ya Kanda. Hao wote wanafanya kazi gani? kuendeshwa hadi maofisini mwao kutundika makoti kusoma magazeti, kusubiri kipindi cha mitihani na kuona matokeo? Hawatembelei walimu wao kuzungumza nao na kugundua matatizo na kuyatafutia ufumbuzi? Kumbe walipewa uongozi wa kazi gani? Ni yapi hasa wanayoshughulikia huku kila mwaka takwimu za matokeo ya shule zinazidi kudidimia? Who really cares? Who gives a damn about pupils/students if nobody gives a damn about the teaching environment? Unsatisfied teachers will result in unsatisfactory results unless we expect magic which unfortunately, never exist. We are moving just like a failed nation with majority of it's people demoralized and a lot looting from every corner like there is no tomorrow. Siyaoni haya yakitendeka enzi za Babu. Walimu walikuwa wakifanya kazi zao na kuwajibika, ukiona gari la Elimu Ualimu unajua iko namna na si njema, kulikuwepo Elimu Ualimu Kikosi cha Mafundi, vimeishia wapi? Mafundi wamehamia kwenye kujifunza namna ya kufanya ufundi wao kwenye makaratasi wakishapata wanakwenda kushinda baa na kuoa wake wa pili na wengine kukalikiti nywele kisha wanapeleka ripoti za kutunga na kazi hazionekani. Hii nchi hii?! Our kids will dig our skulls out of the grave to examine if we really were human beings or some other form of creatures that happened to inhabit this place.
Yesterday at 6:54pm ·
Abel Ngapemba
Abel Ngapemba
Subi, genuine observation na tafakuri. Mwalimu anamwandaa mwanafunzi wake si kujua hesabu tu bali kuwa na maadili, usafi na kuwa presentable. What's the use of having a student with high grades but misbehaves. As a nation we have a long way to go, as citizen we are obliged to shorten the way
Yesterday at 7:49pm ·
Beda Msimbe
Beda Msimbe
Subi would you please cool down, youare damn angry and that is not good for a decent girl. By the way nilikaa nyumbani morogoro, nikaona walimu wanavyoongoza lakini siku hizi walimu ndio wanaongozwa i dont think kama tupo correct. ha ha ha yapo mambo bwana, yapo mambo wengine wameyaua kwa sababu zao binafsi na kisha tumeanza kuwafunza watoto wetu kuajiriwa na kuwa na hiki(tunatengenea wezi) na kisha uwe na hiki lakini hatufunzi watu kutatua matatizo yanayowazunguka. Sasa kama watanzania hawawezi kujifunza kwa hili basi ni ma-mbambalioto kwani watakiona cha mwaka bajeti ya mwaka huu tegemeo ni la watanzania wacha waanze kuwasha mdomo kama pilpili badala ya kujifungia na kujifungwa mkwiji kuvuka.Yule mwanahara,mu wa rhodesia alionyesha njia alipopewa kibano na mjomba wake, afrika ya kusini wakatengeneza nyukilia na vifaru kiama walipobanwa. Hivi sisi tumerogwa nini?
Yesterday at 8:11pm ·
Subi Nukta
Subi Nukta
siwezi kuwa na amani katika hali kama hii, viongozi vululu vululu, wananchi vululu vululu, tupo alimradi bora liende kutwa kuchwa ikawa asubuhi ikawa jioni siku ya pili. Taifa la ombaomba, yeah, we can as well change the name and be The United Republic of Ombaomba. Hii nchi hii?! I guess we have to hit the rock bottom before we really know where we are, where we came from and where we ought to go. Sasa hivi bado naona mshahara wa pesa tatu na matumizi ya shilingi sita unatosha, tusubiri matumizi yatakapofika shilingi tisa na mshahara ule ule pengine tutasema lugha ya tafauti na heshima ya kazi itarudi.
Yesterday at 8:27pm ·
Beda Msimbe
Beda Msimbe
once again you are sawasawa
5 hours ago ·

Vuvuzela kuanza rasmi kuzizima leo.

Leo ndio leo, ilikuwa miaka, miezi, wiki, siku na hatimaye ni masaa tu kuanza rasmi kwa fainali za Kombe la Dunia huko Bondeni ikiwa ni mara ya kwanza toka kuumbwa ulimwengu kwa fainali hizi kufanyika Afrika.
Dimba hili la Soccer City ndipo ufunguzi utakapofanyikia na pia ndipo mechi ya mwisho itafanyikia.
Japo nchi yaongoza kwa uhalifu na bahati mbaya tayari kuna taarifa ya waandishi kuvamiwa na kuporwa kwa mtutu wa bunduki, (nami pia yaliwai kunikuta ktk SAA) lakini tnatumaini kuwa patakuwa na udhibiti mzuri wa usalama hili pasiwepo vitendo hivi tena.
\
Kila la kheri WOZA.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...