September 13, 2011

CUF Yazindua Kampeni Igunga

Mwenyekiti wa CUF Prof Inrahim Lipumba akiteta na Mgombea Leopold Mahona


Chama cha Wanachi CUF kimezindua rasmi kampeni zake kuwania kitu cha ubunge katika jimbo la Igunga kilichoachwa wazi na Rostam Aziz wa CCM alipojiuzulu katika kile alichoeleza kuwa ni kuachana na "siasa uchwara" ndani ya chama chake.




CUF ni chama cha tatu kufanya uzinduzi kikitanguliwa na CHADEMA na CCM, kuna jumla ya wagombea nane katika jimbo hilo. 

Lundenga wa Miss Tanzania aomba radhi!




YAH: KUOMBA RADHI KWA NDUGU ZETU WALIOPATWA NA MAAFA YA AJALI YA MELI HUKO ZANZIBAR .



Usiku wa kuamkia jumamosi ya tarehe 10 / 09 2011 tukio kubwa na la huzuni lilitokea huko Zanzibar ambapo wananchi wengi walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa wakati walipopatwa na ajali ya kuzama kwa MELI iliyokuwa ikitoka Unguja kuelekea Pemba .


Kwa bahati mbaya siku hiyo ya Jumamosi taaasisi yetu ilikuwa inahitimisha Fainali za Taifa za Mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania 2011.



Kama waandaaji wa Mashindano haya na wenye Mamlaka kamili ya maamuzi juu ya ama kuendelea au la kuahirisha jambo hili, tulipatwa na mshituko mkubwa sana juu ya tukio hilo .
kamati yetu ilikaa na kutakafari katika tukio hilo kwa kuzingatia mambo yafuatayo:-




• Taarifa kamili ya maafa haya tuliipata rasmi saa tisa na nusu mchana ( 9:30 ) siku ya jumamosi ambayo ilikuwa ni masaa machache kabla ya Fainali za Miss Tanzania kuanza katika ukumbi wa Mlimani City .

• Wenzetu wa TFF waliendelea na mechi za ligi kuu ikiwemo ya Yanga na Ruvu Shooting.

• Katika kumbi za starehe ikiwemo mabaa na burudani za muziki wa bendi na kumbi za disco ziliendelea kama kawaida.

• Muda uliokuwa umebaki kuwakilisha jina la mshiriki wetu kwenye fainali za Miss World zilikuwa zimekwisha hivyo kulikuwa na hatari ya kupoteza nafasi hiyo

• Pia tamko rasmi la kusimamisha shughuli zote za burudani lilianza tarehe 11 septemba 2011 kuomboleza Kitaifa maafa hayo.



Hata hivyo kama waandaaji tulifanya shindano tukiwa katika maombolezo kwani kabla ya kuanza shindano Watu wote waliokuwepo ukumbini walisimama kimya kwa dakika moja na hata washiriki walipoingia kwenye jukwaa kwa mara ya kwanza walikuwa wamevaa vitambaa vyeusi katika mikono yao ikiashilia maombolezo.



Hali hii imetupa mkanganyiko na kujikuta tukiendelea na mashindano kitu ambacho tunaona tumewakosea Watanzania wenzetu.


Kama Waandaaji tunapenda kusistiza kwamba tunawajibika kwa hayo yaliyotokea na si Taasisi yeyote au Kampuni yeyote na tunaomba ichukuliwe kama ni makosa ya kibinaadamu hasa ukizingatia mazingira magumu tuliyokuwa nayo kwa wakati huo na mkanganyiko wa matukio na taarifa za tatizo hilo.


KUOMBA RADHI
Hata hivyo shughuli hiyo inawezekana imewakwaza watu wengi na kwa sababu hiyo na pia hali halisi ya janga hilo na kwa niaba ya viongozi wenzangu na wadau wa shughuli zetu tunatoa tamko la dhati kwa Familia za ndugu wote walikumbwa na maafa haya, wale wote walionusurika katika ajali hii na Watanzania wote kwa ujumla, kwamba TUNAWAOMBA RADHI KWA MKANGANYIKO ULIOTUTOKEA HADI KUFIKIA HALI HII. Hatuna neno zaidi ya kusema na kusisitiza “TUNAOMBA RADHI”


Mwenyezi MUNGU aziweke roho za marehemu mahali pema peponi,

Amina,

Hashim Lundenga
Mkurugenzi 

Hii inasikitisha sana, Familia nzima kuteketea na usijue waliko!!


Tulikuwa watu 36 wakubwa kwa watoto lakini walionusurika ni wanne tu, 32 wote wamefariki dunia katika ajali hiyo na kati ya watu waliofariki miili iliyoonekana ni saba waliobaki hawajaonekana mpaka sasa,” alisema Ally na kuongeza:
“Ingawa mimi ni mzima lakini mpaka hivi sasa sijui pakuanzia wala pa kutokea baada ya kutoka hospitali kwa sababu familia nzima imeteketea katika ajali hiyo.”



Tulikusanyika wote tukasali 
“Kwa kweli nilipoona hivyo nikajua sasa tumekwisha. Nikarudi tena chini nikakuta maji yameshajaa ndani ya meli ndipo tukakusanyika wanandugu wote tuliokuwa ndani ya meli pamoja na maharusi wetu tukaswali swala ya mwisho na kuambizana kuwa kila mtu ajiokoe mwenyewe na Mungu akipenda tutakutana popote pale iwe duniani ama peponi,” alisema Ally.
“Niliwakusanya watoto wote baada ya kuona wazazi wao wamechanganyikiwa na ukizingatia kwamba hawana uzoefu na masuala ya maji nikawapa godoro na kuwaambia kwamba walishikilie kwani ndilo itakalowaokoa.”
“Baada ya kuwapa watoto godoro, nikarudi kuwatafuta ndugu wengine lakini sikufanikiwa kuwaona tena ndipo nilipoamua kurudi juu kutafuta jaketi nikapata moja nikalivaa kisha nikarudi nilipowaacha watoto na kuungana nao. Wakati huo maji yalikuwa yameshajaa ndani ya meli."
“Kidogo nikaokota mbao ambayo baadaye ilinisaidia kuvunjia moja ya dirisha la meli hiyo kwani wakati huo hata mlango ulikuwa hauonekani nikawapitisha watoto pamoja na mimi mwenyewe nikapita.”
“Nilipofika nje ya meli, nikakuta watu wengi wanaelea na majaketi yao wengine wakiwa wameshafariki dunia, kwa sababu yale majaketi kama hujui kuogelea hayawezi kukusaidia, isipokuwa ukifa huwezi kuzama badala yake utakuwa ukielea juu ya maji. Kadri muda ulivyozidi niliona watoto wakizidiwa na kuishiwa nguvu na mwishoni wote wakafariki dunia mbele yangu.”
Muda wote akisimulia, Ally alikuwa akibubujikwa machozi... “Baada ya kuona ndugu zangu wote wameteketea, ndipo nilipoanza kujiokoa mwenyewe na ilipofika saa 5:00 asubuhi, nikaona helikopta ikipita nikaanza kupeperusha shati langu kila wakati mpaka waliponiona na kuja kuniokoa.”
“Walipofika wakashusha kamba nikajitahidi kujivisha kwa shida kwani wakati huo wote hakuna hata kiungo changu kimoja kilichokuwa kinafanya kazi mwili ulianza kuchanika kwa sababu ya chumvi na baridi kali.”
Miongoni mwa walionusika alikuwamo mtoto wa miaka sita akiwa na dada yake mwenye umri wa miaka 12. Mama mdogo wa mtoto huyo, Mariam Hemedi alisema Said anaendelea vizuri na dada yake amesharuhusiwa kutoka hospitali.

"Beautiful Desert Roses" by Mwanzo Millinga


Opening the 3rd Exhibition in Paris, The French Minister for Culture and Communication, Frederic Mitterrand, said, "Mwanzo, I am deeply touched by the subject you chose to deal with, albinism and the problems encountered by. I am amazed by your humanistic feeling about these people and the quality of your work is fantastic. Lets have a picture together." He dragged me and we posed for a picture





A BEAUTIFUL DESERT ROSE
By Mwanzo Millinga, Tanzania
My inspiration to photograph people with albinism is based on personal admiration of them as beautiful people.

Beauty, as a study in aesthetics, is an entity which is adored, or has characters that are refered to beauty. These can either be individual or in a civilization, that involve the interpretation of some entities as being in balance and harmony with nature. The interpretation may lead to fealings of attraction and emotional well-being. Therefore, beauty is a subjective experience, and it is always said that « beauty is in the eye of the beholder. »

Biologically, albinos are people who lack pigment in their skin, eyes and hair. According to biological findings, majority of albinos are dying at the age of 40 mainly due to skin cancer and sun burn. The genetic disorder causing albinism also results in abnormal vision and, nystagmus which is an involuntary eye movements.

Albinos in Tanzania face two major problems. The first problem is genetic disorder in relation in relation to the environment. This shortern their life as sun burn and skin cancer make them die earlier. The second major problem is the killing from fellow human beings.

There is a tendecy of some people to think of the power of witchcraft in realizing their success dreams. In connection of the albino killings, witchcraft is the main source of the killings. Unfaithful witchdoctors usually tell their clients about the use of albino body parts in making medicine for them to be rich and successful. This makes the demand of the albino body parts go up and increase the killings...
Read more here 
 

BPB say,
Congratulation Mwanzo, this is a fantastic work, the subject you chose and the way of portraying them is also touchy, I am sure, by shading lights through the powerful medium of photography to the plight of our fellow Tanzanians facing will be a wakeup call to lots of people in the world and eventually turn their attentions to this problem and hopeful take necessary measure.


Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...