January 21, 2011
Kisa cha Ngombe, Mzee na mtoto mwenye hekima
Niliwai kusoma hadithi hii mahali fulani, kwa bahati isiyo njema sikumbuki ni kitabu gani, anyway hadithi yenyewe iko hivi:-
Mzee mmoja mfugaji akiwa na mwanae mdogo alikwenda kuchunga mifugo yake wakiwamo Ng'ombe kadhaa, katika kundi lile ng'ombe mmoja alizaa kandama hukohuko polini, ilipofika jioni ilibidi kuwarudisha mifugo yake zizini, wote waliongoza njia isipokuwa yule ngombe na ndama wake, ndama yule baada ya miguu yake kupata nguvu alikuwa anarukaruka tu kule polini.
Mzee yule alikuwa akiangaika kumchapa ngombe mzazi ili aongoze njia ya zizini lakini ngombe yule hakuwa tayari kwani ndama alikuwa bado akivinjali polini kule, Mzee aliangaika kwa kitambo bila mafanikio huku mwanae akimwangalia tu.
Mwishoe mtoto akamshauri babaye, akamwambia- "Baba kwanini usimbebe yule ndama? kwani mamaye atakufuta tu"
Mzee akumwelewa kwanza mtoto wake aliendelea kidogo kumlazimisha ngombe wake, mwishoni akaamua kujaribu kufuata ushauri ule lakini kwa namna ya kujifanya yeye ndo kaamua, akambeba ndama na hatimaye ng'ombe naye akamfata mpaka zizini.
Jambo lile la kushauriwa na mtoto wake tena wa miaka kumi tu lilimkwaza sana mzee yule alifikiri saaana mwishowe akafanya kitendo cha kijinga, akaamua kujinyonga, kisa, kushauriwa na mtoto mdogo.
Sitarajii baba zetu nao watafanya kitendo cha kijinga kama cha mzee mfugaji yule, sitarajii, nina hakika baba zetu leo hii wanabusara sana, wataona ushauri wa mtoto ni changamoto ya kujitafakari na kuamua kwa busara zaidi sasa na wakati ujao pi.
Hongereni sana VIJANA kwa kukataa kukaa kimya.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
LONDON (Dow Jones)--U.K. defense giant BAE Systems PLC (BA.LN) Tuesday was fined GBP500,000 for improper accounting in relation to the award...
-
It’s not important to hold all the good cards in life. It`s important how well you play the cards which you hold. Often, when we lose...
-
On Tuesday, 7th July we witnessed the peak of the Saba Saba festivities. I never go to the Dar es Salaam International Trade Fair, these day...
-
Huwa nina kawaida au tabia ya kusoma kila kilichombele yangu kilichoandikwa, sijui kama kawaida/tabia hii ni mzuri au la kila mtu aweza sem...
-
The Himba are an ethnic group of about 20,000 to 50,000 people living in northern Namibia, in the Kunene region (formerly K...
-
WAPENDWA TWAIJUA NGUVU YA NENO NA UWEZA WAKE? JE TWAJUA KUWA ULIMI WAUMBA AU WABOMOA? The Power of a Word Proverbs 12:18 gives us some val...