November 19, 2011

JK - "NITASAINI SHERIA YA MCHAKATO WA KATIBA"



RAIS Jakaya Kikwete emesema licha ya kelele za wanasiasa, atasaini Sheria ya mchakato wa kuunda Katiba Mpya.

Alitoa kauli jana na kupangua hoja zote kupinga mchakato huo zilizotolewa na Chadema kwamba muswada huo haukuzingatia kanuni zitakazowezesha demokrasia.Kauli hiyo ya Rais imekuja saa chache baada ya Bunge kupitisha Muswada wa Mabadiliko ya Katiba ambao ulisusiwa na Wabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi kwa madai kuwa mchakato mzima una kasoro.

 Akizungumza na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa PTA, Sabasaba juu ya hali ya uchumi nchini na mchakato wa Katiba, Rais Kikwete alisema atatia saini sheria ya mchakato wa kuunda katiba mpya ambayo inatokana na muswada uliopitishwa na Bunge jana.

 Alikibebesha lawama nyingi Chadema kwa kile alichosema ni upotoshaji wa mchakato huo kwa lengo la kuuvuruga wakati unaendeshwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.
 

Alimtupia shutuma za waziwazi Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akisema amekuwa kigeugeu kwa sababu mwanzo alimsifu (Rais Kikwete), kwa kukubali Katiba kubadilishwa lakini baadaye akageuka na kuanza kumponda.

 “Mbowe ni miongoni mwa watu walionimwagia sifa baada ya kutangaza nia yangu ya kuanza kwa mchakato wa Katiba Mpya, nakumbuka ilikuwa Februari 11, mwaka huu wakati akichangia hotuba yangu katika Kikao cha Bunge alisema: ‘Tunampongeza Rais katika suala hili.’ Ila muda mfupi baadaye chama chake kikaja na mtizamo tofauti wa kunyang’anywa hoja yao… na kwamba Rais asiunde tume wala kuhusika katika mchakato.”

 Alisema alishangazwa na kauli za Chadema na kusema: “Hii si mara ya kwanza kwa nchi yetu kufanya zoezi la marekebisho ya Katiba na hata kuandika Katiba Mpya.”

 Alisema kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi, katika suala la upatikanaji wa Katiba anayeunda tume ni Rais na akisema hata katika utawala wa Awamu ya Kwanza na ya Pili, ilibadilishwa mara tatu na Rais ndiye aliyeunda tume.

 “Mwaka 1977 yalifanyika mabadiliko mengine ya Katiba ambayo yalitengeneza Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ilikuja kufanyiwa marekebisho makubwa mwaka 1984,” alisema Rais Kikwete.

 Mwaka 1991 na 1992, alisema iliundwa tume nyingine iliyoongozwa na Jaji Francis Nyalali ya kukusanya maoni ya Katiba ya kutoka mfumo wa chama kimoja kwenda vyama vingi.

 “Tume hii ilipendekeza sheria 40 zifutwe, zilifutwa na nyingine zinaendelea kufutwa ikiwemo sheria ya kumweka mtu kizuizini,” alisema.

 Alisema mwaka 1997 katika utawala wa Rais Benjamin Mkapa aliundwa Tume ya Jaji Kisanga ambayo ilikusanya maoni ya mabadiliko ya 13 na 14 ya Katiba.

 “Siku zote katika mchakato wa Katiba, tume huundwa na Rais, sasa iweje sasa?... Rais amepungukiwa sifa kikatiba?” alisema na kusisitiza kwamba ndiye mwenye mamlaka kikatiba kuunda kamati hiyo.

Alisema iwapo Chadema kitaandaa mchakato wake wa kuunda katiba itabidi mawazo yao wayakabidhi kwa kamati atakayoiunda.

 Alisema tayari CUF iliwasilisha rasimu yake ya Katiba na kuikabidhi serikalini na kwamba nayo itapelekwa kwenye kamati kama sehemu ya maoni yaliyotolewa na makundi ya Watanzania.
 Rais alisema uteuzi wa wajumbe katika tume utazingatia sifa na kwa mujibu wa kanuni akisema hana mamlaka ya kuichagua kwa kuzingatia vigezo vya urafiki.


SOURCE: Mwananchi

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...