June 13, 2012

MINDSET

Tumeona katika post iliyopita tafsiri mbalimbali za neno hili MINDSET, kwa tafsiri ya kibantu isiyo rasmi naweza kusema ni "Mitazamo ama tabia za watu katika kufikili ama kukabiliana na jambo fulani", hii ni tafsiri yangu. 


Mwandishi wa vitabu Carol Dweck amejaribu kuelezea katika kitabu chake cha Mindset sababu mbalimbali za kwanini- 
  • Akili na Kipawa amam kipaji pekee haviwezi kumletea mtu mafanikio, 
  • au ni jinsi vinaweza kusababisha mtu kutokufanikiwa, 
  • na je ni kwanini kupongeza hivyo tu hakuleti utashi wa ndani ama mafanikio bali kuyahatarisha tu, 
  • na je ni jinsi gani kwa kumfundisha mtu ama kuifunza akili wazo dogo tu kwaweza kupandisha kiwango cha ufanisi wa akili na kuleta uzalishaji zaidi. 
  •  
Watu wengi wanafungwa kusonga mbele kimaisha, mafanikio ama masomo kutokana na mitazamo yao, ni mitazamo ambayo yaweza kubadilishwa na mtu kupiga hatua fulani lakini kutokana na ama mapokeo ama mazoea inakuwa vigumu mmno kwa mtu kubadili mtazamo wake kuhusu jambo hili ama lile.Hii inaitwa Fixed Mindset. Mawazo mgando (tafsiri ni ya kwangu)


Mwandshi Dweck anatanabaisha kuwa kuna  mawazo mgando fixed mindset na mawazo endelevu ama Growth Mindset, "In a fixed mindset, people believe their basic qualities, like their intelligence or talent, are simply fixed traits. They spend their time documenting their intelligence or talent instead of developing them. They also believe that talent alone creates success—without effort. They’re wrong."

Mfano wa picha hapo juu ni sawa na watu wenye Fikra ama mawazo mgando, Tembo hawa wa India wakiwa wadogo ufungwa na mnyororo huo na kigingi hicho, kwa sababu wanakuwa wadogo wanakuwa hawawezi kujinasua katika kigingi hicho, watajaribu mara kadhaa wakishindwa wanaacha, wanakata tamaa, wanaamini kuwa hawawezi, kwa wakati huo kwao kinakuwa ni kikubwa na hakiwezekani. 

Kuna msemo kuwa "Tembo uwa hasahau" hivyo ata anakupokuwa mkubwa kama nyumba anafungwa katika kigingi kile kile na kwa sababu hasau, Tembo huyo hatofanya juhudi yoyote kujinasua hapo japo hakika anaweza akiamua kwa sababu angali anakumbuka kwamba alipokuwa mdogo kilimshinda, hivyo tembo huyu atatulia hapo hapo muda wote mpaka mtu aje amfungue.

Dale Canergie anasema,
"Develop success from failures. Discouragement and failure are two of the surest stepping stones to success."

Kwa maana nyingine ni kwamba kushindwa jambo fulani, iwe masomo, biashara, fursa au mahusiano mara moja au mbili hata tatu si kushindwa bali ni kujifunza, kwamba kushindwa huko ndio ngazi ya wewe kuelekea mafanikio, mgunduzi wa taa hizi za umeme Thomas Edson alijaribu mara zaidi ya 999 kabla ya kufanikiwa kugundua taa hizi tutumiazo sasa, lakini yeye anasema, "I have not failed. I've just found 10,000 ways that won't work."

Kama Tembo Je ni wangapi wameendelea kushikiria mapokeo ama mtazamo kwamba hili haliwezekani ama siliwezi, kwa sababu tu ama walijaribu wakashindwa tena mara moja au mbili tu?  au kujaribu jambo ama fursa mpya tofauti na mazoea ama mapokea au mitazamo mgando, huku wakijinadi kuwa wanaishi katika karne ya Sayansi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ama Information Age?. Jibu utakuwa nalo msomaji.

Katika mawazo endelevu anasema "In a growth mindset, people believe that their most basic abilities can be developed through dedication and hard work—brains and talent are just the starting point. This view creates a love of learning and a resilience that is essential for great accomplishment. Virtually all great people have had these qualities."

Hawa si watu waliokubali kuwa kigingi hiki hawakiwezi, wamejaribu tena na tena, wamejifunza na hawakukata tamaa na hatimaye ndio kundi la watu wenye mafanikio duniani. 

Wengi wetu wa umri kama wangu na zaidi tunaweza kukumbuka zamani kulikuwa na kampuni hii ya mafuta ya Shell, hii ni kampuni kubwa sana ya mafuta duniani inaajiri wafanyakazi wapatao 25,000/-,(takwimu za 2008)  vituo vingi vya mafuta mpaka hii leo vinaitwa Shell hapa nchini, sijui ni wangapi hasa vijana leo hii wanajua kwanini vituo hivyo vinaitwa kwa jina hilo, sijui, lakini sijui ni wangapi wanafahamu historia ama sababu ya kampuni hii ya kubwa ya mafuta kuitwa jina hilo, iko siri kubwa na ya kutia moyo kuhusu kubadili mtazamo au MINDSET CHANGE, fuatana nami hapa hapa kujua zaidi juu ya hilo. 


Nakutakia usomaji mwema na mafanikio, Kwa maoni na ushauri waweza kunipigia 0784475576, 0716927070 au email: brwebangira@gmail.com

 


Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...