|
Usahili wa nafasi ya Mkaguzi Msaidizi idara ya Uhamiaji. |
UKISTAAJABU YA UHAMIAJI UTAONA YA UTUMISHI..!!
Siku ya (ijumaa trh 13/06/2014) idara ya Uhamiaji ilifanya usaili kwa jumla
ya vijana 10,846 ili kupata vijana 70 tu watakaoajiriwa kama Maafisa Uhamiaji
wasaidizi. Hii ilikua ni wastani wa 1/156 yaani nafasi moja ya kazi
ilishindaniwa na watu 156. Uwezekano wa kupata nafasi kwa vijana waliojitokeza kufanya
usaili (probability) ilikua 0.0064.
Kwa lugha nyingine ni kwamba kila kijana aliyejitokeza
kwenye usaili ule uwezekano wa kupata kazi ni asilimia 0.64% na uwezekano wa
kukosa ni asilimia 99.36%. Kwa maneno mengine ni kuwa uwezekano wa kupata kazi ni chini
ya asilimia moja (possibility is less than 1%). Rekodi hii ni ya kwanza kutokea
duniani.
Kabla ya rekodi hii, nchi iliyokua ikishikilia rekodi ni
China. Mwaka jana kiwanda kikubwa zaidi cha nguo duniani kiitwacho China
Textile Industry, kilichopo mjini Keqiao, kwenye Kaunti ya Shaoxing jijini
Shanghai, kilifanya usaili kwa watu zaidi ya laki moja wakitafuta kuajiri watu
5,000 tu.
[Kiwanda hiki kina wafanyakazi zaidi ya elfu hamsini na
vibarua zaidi ya laki 2 wanaofanya kazi kiwandani hapo kila siku]. Kufanya usaili kwa watu laki moja ili kupata waajiriwa 5,000
inamaanisha uwezekano wa kupata kazi kwa kila mtahiniwa (probability) ilikua
0.05. Kwa lugha nyingine ni kuwa uwezekano wa kupata kazi kwa
watahiniwa ulikuwa 5% na uwezekano wa kukosa ulikua 95%. Jumuiya ya kimataifa ililaani kitendo hiki na usaili huu
ukaingia kwenye rekodi za dunia kuwa ni usaili wa hovyo zaidi kuwahi kutokea
duniani. (The world most ridiculous job interview ever happened). Taarifa zinasema kuwa haikua haki (it was unfair) kumdahili
mtu huku uwezekano wa kupata kazi hiyo ukiwa chini ya asilimia 5%. Ilionekana
ni uonevu.
Vyanzo vya habari vilivyopinga usaili huo vinasema, Shirika
la kazi duniani (ILO) linapendekeza usaili wa kazi uwape uhakika wa zaidi ya
50% wanaosailiwa.
Hii ina maana kuwa mtu anayefanyiwa usaili wa kazi anapaswa
kuwa na uhakika wa angalau 50% wa kupata kazi wakati anapofanyiwa usaili. Asilimia 50% maana yake ni kuwa idadi ya wasailiwa isizidi
mara mbili ya nafasi za kazi zilizopo. Kwa mfano kama nafasi ni 70 unapaswa
kufanya usaili kwa watu wasiozidi 140.
Katika nafasi 70, ukisaili watu 140 maana yake ni kwamba
kila aliyeitwa kwenye usaili ana uhakika wa kupata kazi wa 50%. Hivi ndivyo ILO
wanavyopendekeza. Yani uhakika uwe 50% au zaidi.
Na hivi ndivyo mashirika mengi ya kimataifa yanavyofanya.
Kama nafasi ni 3 hata mkiomba 100 uwezekano wa kuitwa kwenye usaili (interview)
ni watu 6 tu' ili katika hao 6 wapatikane watatu watakaoajiriwa (sawa na 50% ya
waliodahiliwa). Sasa Idara ya Uhamiaji wakaamua kwa makusudi kuvunja rekodi
ya China na kuiweka Tanzania kwenye kilele. Wakati China ikipigiwa kelele kwa
kuweka uwiano wa asilimia 5%, Uhamiaji wao wakaenda mbali zaidi kwa kuweka
uwiano wa asilimia 0.64% Hali hii iliwafanya Watanzania wengi kulaani mfumo huu wa
usaili uliotumiwa na idara ya UHAMIAJI kwa sababu kuu mbili.
Kwanza ni mfumo wa udhalilishaji. Huwezi kuwakusanya wasomi
kwenye uwanja wa mpira kama magunia ya vitunguu ili wafanye usaili wa kazi.
Aina hii ya usaili ilikiuka misingi ya utu (it was agaist human dignity). Pili usaili huu ulizidi kudhoofisha hali ngumu za kiuchumi
walizonazo vijana hawa. Gharama za nauli (kwa waliotoka mikoani), malazi na
chakula walizotumia ni wizi wa kusadikika uliofanywa na serikali (ya CCM).
Ikiwa kila kijana alitumia wastani wa 150,000/= kama gharama
za nauli, malazi na chakula kwa siku alizokaa Dar, ukizidisha kwa watu 10,000
utapata jumla ya shilingi Billion Moja na milioni mia tano (1.5 billlios). Fedha hizi ni nyingi kuliko fedha zote za miradi ya
maendeleo kwenye wizara ya Afrika Mashariki. Ni nyingi kuliko madai ya askari
Magereza wote nchini. Askari magereza wanadai jumla ya bilioni 1.2 ikiwa ni
malimbikizo ya posho zao mbalimbali, ghamama za uhamisho n.k. Hebu fikiria vijana wasio na kazi wala chanzo chochote cha
mapato unawapora Bilioni moja na milioni mia tano, kwa kisingizio cha kuwaita
kwenye usaili.!!! Tena usaili wenyewe uwezekano wa kupata kazi ni chini ya
asilimia moja (1%).!!! Huu mi uhuni na ukatili usioweza kuvumilika.
Mbaya zaidi
ukatili huu umefanywa kwa makusudi na serikali (ya CCM). Lakini wakati hayo yote yakiendelea kuna kioja kingine
kikubwa kimetokea. Lakini hakijasikika sana labda kwa kuwa kila mtu alikua
"busy" na kioja cha idara ya UHAMIAJI. Kioja chenyewe ni hiki. Menejimenti ya utumishi wa umma
ilitangaza nafasi za kazi. Vijana zaidi ya 4,000 wakaomba nafasi mbalimbali
zilizotangazwa.
Wote wakaitwa kwenye usaili. Usaili wenyewe ulikua juz
(jumamosi) pale chuo cha Mwl.Nyerere Kigamboni. Hakuna aliyedhani kama UTUMISHI wangeweza kurudia makosa ya
UHAMIAJI. Lakini kilichotokea ni kinyume chake. Idadi ya watu haikua kubwa sana
kama ile ya Uhamiaji lakini nafasi zilikua chache zaidi ya zile za Uhamiaji.
Kwa mfano nafasi ya maafisa maendeleo ya Jamii (Community
Dev.Officers) iliombwa na watu 716, walioshiriki usaili jana ni watu 564.
Lakini nafasi za kazi (vacancy) kwa maafisa maendeleo ya jamii zilikua mbili
tu. Hii inamaanisha kuwa vijana wote 564 waliofanya usaili jana
kwenye nafasi ya maafisa maendeleo ya jamii, walikua wanapigania nafasi mbili
tu za ajira. Huu ni uwiano wa 0.35% au 1/282. Yani kati ya watu 282
waliofanya usaili ataajiriwa mmoja, halafu mwingine mmoja atapatikana kati ya
282 waliosalia. Hii ni sawa na kusema vijana wote walioshiriki usaili huu
kwenye nafasi tajwa hapo juu wana uhakika wa kupata ajira kwa 0.35% na uhakika
wa kukosa ni 99.65%.
Hiki ni kiwango cha juu zaidi ukilinganisha na kile cha
UHAMIJAJI ambako uhakika wa kupata ajira ulikua angalau 0.64% na kukosa 99.36%. Hii inamaanisha kuwa UTUMISHI wamevunja rekodi ya dunia
iliyowekwa na idara Uhamiaji. Kwa lugha rahisi ni kuwa Uhamiaji walishikilia
rekodi kwa siku moja tu kisha Utumishi wakaivunja.
Hivyo basi napenda kuchukua fursa hii kutangaza kuwa
Menejimenti ya UTUMISHI WA UMMA nchini Tanzania kwa sasa ndiyo inayoshikilia
rekodi ya dunia ya kufanya usaili wa kazi wa hovyo kuliko usaili mwingine
wowote uliopata kutokea duniani (The world most ridiculous job interview). Hongera idara ya Utumushi kwa kupata nafasi hiyo. Pongezi
kwa mama Hawa Ghasia na serikali nzima (ya CCM) kwa kutekeleza vema Ilani ya
chama chenu. Ama kweli ukistaajabu ya UHAMIAJI utayaona ya UTUMISHI. Analysis from post by Blood Hurricane JF member
My Take.
Japo tatizo la AJIRA laweza kuonekana kubwa lakini ukubwa huu ukiangalia kwa mtazamo chanya ni FURSA pia, katika kila CHANGAMOTO kuna FURSA ndani yake, na CHANGAMOTO inapokuwa kubwa zaidi FURSA inakuwa kubwa zaidi na yeyote atakaye weza kutafuta na kupata ufumbuzi kwa tatizo hilo upata mafanikio makubwa zaidi.
Naamini hii ni FURSA kubwa sana inahitaji CREATIVE MIND kuunganisha mtandao huu na kufanya muujiza wa karne, WE CAN DO IT.
Nitafafanua kwa kina zaidi katika post zitakazo fuata.
LETS THINK POSITIVE NO MATTER WHAT!