Sonya Skin Care

Sonya Skin Care
Click the Advert for more info.

Top ten reason to Drink it

Get noticed

Advertise with us

Subscribe here to get blog updates directly in your inbox

March 2, 2012

Jishindie Pesa taslim 1, 000, 000/-

Time is money, make the most of your on-line time by making money, Share and win One Million  Tzs. 

Habari Wadau
Bongo Pix Blog imekuwa kimya kidogo kwa takribani miezi kadhaa, hii ni kutokana na maboresho ambayo yanaendelea kufanyika, kutokana na tathimini iliyofanyika mara ilipotimiza miaka mitano, BPP katika mtizamo mpya itazinduliwa upya hivi karibuni, hivyo kwa kuthamini mchango wako mpenzi msomaji wetu tumeamua kumzawadia msomaji mmoja Tsh Millioni Moja.


Ndio, msomaji au Mdau mmoja atazawadiwa kitita hicho kwa kufanya zoezi moja dogo sana, zoezi la kutuma ama kushirikisha watu wengine wengi zaidi link ya blog hii kwa kutumia kitufe cha EMAIL THIS (cha kwanza mwisho wa post) au njia nyngine yoyote ya kushirikisha ama kujulisha watu wengine, iwe in facebook, twitter nk.


Hii si bahati nasibu, bali Yule atakayekuwa ametuma ama kushirikisha watu wengi zaidi ndiye atakuwa mshindi, zoezi hili linaanza leo tarehe 02/03/2012 mpaka tarehe 30/04/2012 saa 5:59 usiku EAT.

   

Email this kwa watu wengi zaidi ujishindie kitita hicho.

NB: Kumbuka kutuma pia kwa brwebangira@gmail.com kwa urahisi wa ufuatiliaji.

Bongo Pix Blog

February 15, 2012

WINNERS Boulevard.: “Tell me what your wages should be.”

WINNERS Boulevard.: “Tell me what your wages should be.”: Je wajua kwamba waweza kulipwa kiasi chochote pesa upendacho kwa mwezi kwa kazi ya kushirikisha ama kujulisha watu wengine taarifa ama jam...

February 6, 2012

"KUNRADHI"

Kunradhi wadau woote wa Bongo Pix, kwa kitambo kidogo BP imekuwa haina habari mpya, hii ni kutokana na majukumu kuinguliana, Nimekuwa BUSY kama Nyuki katika kipindi cha karibuni. 



U-busy huu ni maboresho, si tu ya Blog lakini pia ya mada na vitu mbalimbali vipya ambavyo vitaanza kuonekana hapa, BPB itakuwa na maboresho makubwa hivyo endelea kutembelea Blog hii ujionee mwenyewe. 

Poleni na samahani sana kwa usumbufu wowote. 
Bongo Pix Blog.

December 8, 2011

POSHO -M, MKULO HAJUI KITU!


Finance Mustafa Mkulo has said he does not know whether sitting or any other allowances for Members of Parliament have been increased substantially as reported in the media and confirmed by National Assembly Speaker Anne Makinda on Tuesday.

While Makinda told journalists that the daily sitting allowance during House sessions had risen from 70,000/- to 200,000/-, chiefly owing to hikes in house rental charges in Dodoma, the minister told this paper in a telephone interview in Dar es Salaam yesterday that he knows “completely nothing” on the matter.


Pressed for elaboration, Mkulo recommended that the appropriate place to go for details was the Speaker’s Office.


“It is better you contact the Speaker for details on what she is reported to have said. As I speak, I know completely nothing about the increase being talked about,” he said.


Winding up debate on the 2011/2012 government Budget in July, the minister said the effect of personnel allowances on the national budget was “very minimal”.


He said the 2011/2012 Budget totalled 13.5trn/- but personnel allowances accounted for only 352.74bn/-, including 25.65bn/- in sitting allowances for public servants – out of which 4.92bn/- went to MPs.
Source: IPPMEDIA. 

November 29, 2011

HATIMAYE MUSWADA MABADIRIKO YA KATIBA WAWA SHERIA!





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Novemba 29, 2011, ametia saini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011.

Hatua hiyo ya Mheshimiwa Rais kutia saini Muswada huo inakamilisha safari ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge kuwa limepitisha Muswada huo uliowasilishwa na Serikali katika kikao kilichopita cha Bunge.

Aidha, kutiwa saini kwa Muswada huo ili uwe Sheria ni hatua kubwa na muhimu katika safari ya kutungwa kwa Katiba mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais Kikwete katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Desemba 31, mwaka jana, 2010.

Pamoja na kutiwa saini hiyo bado Serikali itaendelea kusikiliza maoni na mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.

Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yoyote mwenye maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

KATIBA MPYA - CHADEMA NA RAIS WAKUBALIANA



MAKUBALIANO YA RAIS NA CHADEMA YALIVYOLIPOTIWA:

HABARI LEO: JK, CHADEMA MWAFAKA.
MUSWADAwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 uliopitishwa na Bunge hivi
karibuni utasainiwa na Rais Jakaya Kikwete kama ilivyopangwa.

Hali hiyo inatokana na makubaliano yaliyofikiwa jana kati ya Rais na Kamati ndogo ya Chadema iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe.

Juzi na jana, pande hizo mbili zilikuwa na mazungumzo kuhusu Muswada huo ambao ulipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila ushiriki wa wabunge wa Chadema na wa NCCR-Mageuzi ambao walisusia.

Kususia mjadala wa Muswada huo kwa wabunge hao wa vyama hivyo, ulitokana na madai yao ya kutaka Muswada huo usomwe mara ya kwanza bungeni wakidai haukuwa umesomwa na wananchi na kuuelewa, hivyo kukosa kuuchangia, lakini walikataliwa na Spika Anne Makinda.

Kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa jana Ikulu Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi na Kaimu Katibu Mkuu Chadema, John Mnyika, kutakuwa na haja ya sheria hiyo baada ya kusainiwa kuendelea kuboreshwa, ili ikidhi mahitaji ya kujenga na kuaminiana na mwafaka wa kitaifa.

Pia kutakuwa na mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha mwafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba mpya.

Awali ilielezwa kuwa mazungumzo hayo yalifanyika katika mazingira ya uelewano ambapo Rais Kikwete aliwahakikishia Chadema kuwa yeye na Serikali yake wana dhamira ya kuhakikisha Tanzania inapata Katiba mpya.

Kulingana na hatua iliyofikiwa jana, Rais atasaini Muswada huo kuwa sheria ambayo inatarajia kuanza kutumika Desemba mosi, lakini wakati ikiendelea kutumika, kutakuwa na fursa ya kuifanyia marekebisho endapo haja itajitokeza.

Hili si jambo jipya kwa masuala ya uandishi wa Katiba mpya, kwani hata ya Kenya ilipitishwa na mpaka sasa zipo taarifa kuwa imeshafanyiwa marekebisho mara 11 kutokana na mahitaji yanayoibuka kwa kuzingatia mazingira na muktadha.

Makubaliano ya jana, yanamaliza sintofahamu iliyokuwa imeanza kuibuka kwa Chadema na makundi mengine kutaka kufanya maandamano nchi nzima, kupinga Muswada huo kusainiwa na kushinikiza urejeshwe bungeni kusomwa kwa mara ya kwanza.

Lakini pia kunatoa fursa pana kwa wawakilishi na wabunge kurudi kwa wananchi kuwahimiza kujitokeza kutoa maoni na mawazo yao kuhusu aina ya Katiba inayotakiwa na Watanzania wote.



MWANANCHI - JK, CHADEMA WAKUBALIANA KUBORESHA MUAFAKA.
RAIS Jakaya Kikwete na viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe wamekubaliana kwamba ipo haja ya kuendelea kuuboresha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 ili ukidhi mahitaji ya kuaminiana na mwafaka wa kitaifa.Pia, wamekubaliana yawepo mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha mwafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba Mpya.

 Makubaliano hayo yamefikiwa jana na kusainiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi baada ya kumalizika kwa mkutano wa siku mbili baina ya pande hizo mbili kuhusu muswada huo.

 Katika kikao cha jana Mbowe aliongozana na wajumbe wa kamati hiyo Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara) Said Arfi na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) Said Issa Mohamed, Mshauri wa Masuala ya Siasa wa chama hicho, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Tundu Lissu na John Mrema.

 Katibu Mkuu Dk Willibrod Slaa ambaye ni mjumbe hakuwapo katika kikao cha juzi na cha jana na taarifa zilizopatikana baadaye na kuthibitishwa na yeye mwenyewe ni kwamba alikuwa safarini kwenda kuhudhuria kesi yake mahakamani Arusha jana.

 Kabrasha lililokabidhiwa na ujumbe wa Chadema kwa Rais Kikwete lilikuwa lina waraka uliotoa mapendekezo mbalimbali ya kurekebisha muswada huo huku wakitaka sheria iweke wazi kwamba Rais hana mamlaka yoyote juu ya Bunge Maalum la Katiba zaidi ya mamlaka ya kuliitisha kwa mara ya kwanza na kwamba mamlaka ya Bunge hilo yataisha mara baada ya kupitishwa kwa Katiba Mpya katika Bunge Maalum la Katiba.

 Wametaka ifanyike hivyo kwa kuwa sheria hiyo inampa Rais mamlaka juu ya Bunge Maalum la Katiba wakati Bunge hilo linatakiwa kuwa chombo huru na chenye mamlaka ya juu kuliko mamlaka nyingine zozote katika nchi.

 Katika waraka wao, Chadema wameeleza kutaka vifungu vyote vinavyokiuka haki za kimsingi za kikatiba vifutwe na kuwapo na uhuru kamili wa kujadili, kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi juu ya utungaji wa Katiba Mpya hata kama itakuwa kinyume na matakwa ya Tume ya Katiba na masharti ya Sheria hiyo.

Katika ukusanyaji na uratibu wa maoni ya wananchi juu ya Katiba Mpya na masuala ya muungano wametaka ziundwe tume mbili za katiba, moja itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya kwa ajili ya masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanganyika na ya pili itakayokusanya na kuratibu maoni ya wananchi juu ya masuala ya Muungano.

THE CITIZEN – JK, CHADEMA Talks:  The Way forward
The government and the opposition Chadema party have agreed in principle that the newly passed Constitutional review Act 2011 bill needs major amendments.

A joint statement issued yesterday by the two sides at the end of two days  of consultations, said that the bill should be improved so as to bring  it to the requirements of building a national consensus as well as cohesion. The one page statement signed by the minister for Information, Youth, Culture and Sports, Dr Emmanuel Nchimbi, on behalf of the government and Chadema Director for Foreign Affairs and International relations, Mr John Mnyika, notes also that the talks were conducted in a cordial atmosphere.


The two sides also agreed in the closed door talks that there was a need  for the government and other stakeholders to hold constant  meetings and consultations, for the purpose of building and strengthening national consensus during the process of crafting a new Constitution.

The agreement has brought the two sides at the middle ground. The Chadema team, which was led by its national chairman, Mr Freeman Mbowe, went into the talks with  a strong proposal that President Kikwete should not sign the new Bill into law.

On the other hand, the government believed that the bill was perfect and President Kikwete indicated that he would  endorse it despite sentiments from Chadema and a number of activists under the banner of Tanzania Constitution Forum (TCF).

President Kikwete, his government and the Parliament, insisted that the Bill has no flaws as it followed all legal  processes and procedures during its processing before it was passed by the Parliament more than a week ago.

Chadema MPs boycotted the debate on the Bill in Parliament in protest over claims that the authorities did not give common Tanzanians an  opportunity to widely discuss one of “the most important pieces of legislation to have been drafted in the last 50 years.”

And the thrust of  the Chadema message to President Kikwete and his team during the talks centred on rejecting the Bill, asking that it should not be assented, and its processing start afresh.

In their letter to the President, a copy of which was seen by The Citizen, the opposition party pleaded with  the Head of State not to assent the Bill so as to give time for wananchi to air their views on it. They also argued that there is a need for wananchi to be educated about the Bill as experience has shown that most people believe that what was passed was a new Constitution. Chadema said there was a need to first amend the current constitution in order to align it with prevailing conditions, in order to have a level playing field between the two sides of the Union during the writing of a new Constitution.


DAILY NEWS - Kikwete, Chadema reach consensus
PRESIDENT Jakaya Kikwete will soon sign into law the Constitutional Review Bill following a two-day meeting with a delegation from the opposition Chadema that apparently held different views.

 This means that the review process will start anytime from now, putting to an end heated debate and forums on the same that recently dominated the country’s political scene.

 A press statement signed by the Minister for Information, Culture and Youth, Mr Emmanuel Nchimbi, and Chadema Acting Secretary General John Mnyika reiterated that the meeting was conducted in a friendly atmosphere.

 The five-hour long meeting that started from 10am at the State House in Dar es Salaam on Monday, concluded that despite the Bill being passed by Parliament, it would be amended if and when necessary for it to win public trust and national consensus.

 The two parties also underscored the need for frequent communications and cooperation between the government and other stakeholders on improving the law to maintain national consensus during the constitutional review process.

 The CHADEMA delegation was led by the party’s National Chairman, Mr Freeman Mbowe. On Sunday, President Kikwete received recommendations on constitution review from CHADEMA. Both parties agreed that the process should adhere to the interest of the nation much as it should also refrain from dividing the public according to their religion, tribe and region.
 Last week, CHADEMA sought the president’s audience over the constitutional review Bill after their bid to stop a second tabling of the constitutional review Bill in parliament by staging a walk-out failed.

 Demonstrations planned by activists scheduled for Saturday to press President Kikwete not to sign into law the constitutional review Act were banned by police for fear that they would escalate into chaos. 

My take: 
Hizo YELLOW, sijaelewa sawasawa, labda wataalamu wanaweza kunisaidia, mnisamehe kwa kutokuelewa kwangu muafaka huu hasa kutokana na nukuu hizo. 

November 28, 2011

Movie debut: How Canon's C300 camera was created - British Journal of Photography

Movie debut: How Canon's C300 camera was created - British Journal of Photography:



When Canon announced that it was developing a new concept digital SLR with 4K video recording capabilities, photographers wondered whether the new model would be the long-awaited EOS 5D Mark III.


And while the new concept camera has so far remained unnamed, Mike Owen, Canon's European professional communication manager, in an interview with BJP's news and online editor Olivier Laurent at the Cinema EOS launch event in Berlin, confirmed that the camera [pictured above] will not be part of the firm's EOS range of still cameras.

"The Cinema EOS system is a system," he tells BJP. "It will have multiple products as the EOS product line has, and the thing that will tie all of this together will be the lens mount, because we feel that our lenses are one of our key assets. But when it comes to the concept camera, that will be part of the Cinema system, and the still EOS range will continue to develop as it has been over the past few years."

The confirmation comes as Canon is heavily promoting its Cinema EOS C300 camera to the European market, which, despite its fragmentation, is home to the world's largest filmmaking community. "It's always difficult to address a fragmented market when launching a new product," says Owen, "but it's the same with every single product we launch. We always try to have, as much as possible, a unified European approach to launching products. But, in terms of the implementation of the message, it can very complicated. One message, for example, that might work in the UK might not work in the Middle East."

"KUPANDISHA POSHO ZA WABUNGE 154% NI UKICHAA"


Nimeshtushwa sana na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa Wabunge. Nimeshtushwa zaidi kwamba Posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua maana maslahi yote ya Wabunge huamuliwa na Rais Baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge.


Wabunge wote watambue kwamba kuamua kujipandishia posho zao bila kuzingatia Hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano. Mbunge yeyote ambaye anabariki Jambo hili au anaishi hewani haoni tabunza wananchi au ni mwizi tu na anaona Ubunge ni Kama nafasi ya kujitajirisha binafsi.


Kwa Wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni uamuzi wa chama na ni uamuzi wa kisera. Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi. Nimemwomba Katibu Mkuu wa chama kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hili.


Toka tarehe 8 juni mwaka 2011 nilikataa kupokea posho za vikao. Popote ninapohudhuria vikao huomba Risiti ya fedha ninazokataa. Baadhi ya Wabunge Kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho.


 Nampongeza kijana mwenzangu kwa uzalendo huu. Nawataka wabunge wengine wenye Moyo wa dhati kukataa sio tu ongezeko hili la posho Bali posho yote ya vikao. Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa?

Tazama nchi hii, juzi serikali ilipokea Msaada wa tshs 20bn kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa 28bn Kama posho za kukaa tu.

Tanzania inaagiza gesi ya matumizi ya nyumbani kutoka nje kwa kutumia mamilioni ya dola za kimarekani. Kuwanda cha kutengeneza LPG kinagharimu tshs 35bn tu, Wabunge peek Yao kwa mwaka wanatumia 28bn kwa posho za kukaa tu achilia mbali mishahara na marupurupu mengine.

Ipo siku Watanzania watatupiga mawe kwa usaliti huu dhidi yao.

Zitto Kabwe(MB)
Kigoma Kaskazini -Chadema

PRESS RELEASE - IKULU


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wa Serikali yake leo, Jumapili, Novemba 27, 2011, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

 Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, yamefanyika katika mazingira ya urafiki na ujumbe wa CHADEMA umewasilisha mapendekezo yake kuhusu mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya Tanzania. Serikali imepokea mapendekezo hayo.

 Hata hivyo, pande zote mbili zimekubaliana kukutana tena asubuhi ya kesho, Jumatatu, Novemba 28, 2011, ili kuipa nafasi Serikali iweze kutafakari mapendekezo hayo.
 

Lakini pande hizo mbili zimekubaliana kuwa Katiba ya sasa ni Katiba nzuri iliyolilea Taifa kwa miaka 50 iliyopita kwa sababu ni Katiba ya sasa iliyoliwezesha Taifa la Tanzania kuwa na amani, utulivu na kupata maendeleo makubwa ambayo nchi yetu imepata mpaka sasa.

 Pia pande zote mbili zimekubaliana kuhusu umuhimu wa kutunga Katibu Mpya kama Mheshimiwa Rais Kikwete alivyoliahidi taifa wakati wa salamu zake za mwaka mpya Desemba 31, mwaka jana, 2010, Katiba ambayo italiongoza Taifa la Tanzania kwa miaka mingine 50 ijayo.

 Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Rais aliwahakikishia wajumbe hao wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Mheshimiwa Freeman Mbowe kuwa ni dhamira yake na ya Serikali yake kuhakikisha kuwa Tanzania inapata Katiba mpya.

 Katika mkutano huo, pande zote mbili zimekubaliana kuwa ni jambo muhimu sana kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba Mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na umoja wa kitaifa.

 Aidha, pande zote mbili zimekubaliana kuwa mchakato huo uendeshwe kwa kuzingatia misingi ya mambo mengine muhimu kwa taifa la Tanzania kama vile kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, kuligawa Taifa kwa misingi ya udini na ukabila ama kutugawa kwa misingi ya maeneo.

 IMETOLEWA NA: KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU NOVEMBA 27, 2011
 DAR ES SALAAM
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Some of published work

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Arts n' Photo sildes

Popular Posts

Picasa Photostream

Flickr Photostream

Follow us on FACEBOOK

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576