November 25, 2011

Mvua zaleta maafa!



WATU wawili wamekufa na wengine watatu kunusurika baada ya lori walilokuwa wakisafiria kusombwa na maji katika daraja la Mto Loobuko kati ya Makuyuni na Mto wa Mbu wilayani Monduli.


Ajali hiyo ilitokea jana saa 12 alfajiri wakati lori hilo namba T190 AKW likiwa limebeba mitambo ya kutengeneza barabara likitoka Engaruka kwenda Arusha, kukumbwa na dhahama hiyo.

Maafa hayo yametokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika milima ya Monduli.

Mfanyakazi wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), Augustino Masige, akiendesha gari namba T573 AHW, akitoka Arusha kwenda Musoma ni miongoni mwa watu walionusurika katika maafa hayo baada ya gari lake aina ya Toyota kusombwa na maji eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Jowika Kasunga, aliwataja watu waliokufa kuwa ni dereva wa lori hilo aliyetambuliwa kwa jina moja tu la Shekman (38) na msaidizi wa mitambo ya kutengeza barabara, Samwel Julius (28).

Kasunga alisema watu hao walisombwa na maji umbali wa kilometa moja huku msaidizi wa opareta wa mitambo, alikutwa amenasa kwenye miti huku amekufa.

Dereva alikutwa amekufa umbali wa kilometa moja baada ya kugunduliwa na wanafunzi wa shule za msingi waliokuwa wakirejea nyumbani kutoka shuleni.


Kwa hisani ya Father Kidevu blog

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...