April 29, 2008

VERSE OF THE DAY

“And without faith it is impossible to please God, because anyone who comes to him must believe that he exists and that he rewards those who earnestly seek him.”- Hebrews 11:6

KP

We kipanya we ni chiboko aisee!!

Neno la wiki

Gaurding Your Ways In Psalm 39:1, we are given an important warning,I said, "I will guard my ways, lest I sin with my tongue; I will restrain my mouth with a muzzle, while the wicked are before me." The Hebrew word translated ways in this passage literally means a well-trodden path. It paints the picture of a pathway that has been walked down so many times that a groove has been worn in that path. The psalmist is drawing our attention to something that has been repeated again and again, a response that has been so often repeated that it has become engrained in our behavior—a habit.You have probably heard the saying, "He's set in his way," meaning it is not likely you are going to change the way a person acts in certain instances. The "ways" are habits, attitudes, and responses that aren't likely to change without a very powerful motivation or without some sort of an encounter with God. I think virtually every habit we have initially began with a thought. Sow a thought; reap an action. Sow an action; reap a habit. Sow a habit; reap a character. Sow a character; reap a destiny. It all goes back to a thought that perhaps should have been dealt with, but wasn't.Take some time to consider your thoughts. Are you giving way to thoughts that will lead to ungodly habits? If so, give those thoughts to God and ask Him to help you think the thoughts that will lead to godly habits.

JK uso kwa uso Morgan Tsvangirai

Mtoto Salome Yohana azikwa

Mtoto Salome Yohana (3) aliyechinjwa kimazingara amezikwa leo huko Tabata Segerea na umati wa watu ambao walionyesha kusikitishwa sana na jinsi mtoto huyo alivyouwawa kinyama.

April 28, 2008

KIJANA ADAI ANA VICHWA 50 ZAIDI!!!!

Aliyekutwa akitafuna kichwa cha mtoto atoa madai mazito.
Kijana Ramadhani Seleman Mussa (18), anayedaiwa kukutwa akitafuna kichwa cha mtoto Salome Yohana (3), amedai kumiliki vichwa vingine 50. Mbali ya kumiliki vichwa hivyo, pia kijana huyo amedai kwamba, amekuwa `akitengeneza` ajali barabarani kwa njia za kishirikina kwa lengo la kujipatia damu ya kunywa.
Alitoa madai hayo jana katika kituo kidogo cha polisi cha Stakishari, Ukonga jijini Dar es Salaam ambako anashikiliwa pamoja na mama yake mzazi, Khadija Ally na baba yake wa kufikia, Lucas Kibaya.
Akiwa kituoni hapo, kijana huyo alionekana akitoa maelezo hayo kwa ujasiri na pasipo wasiwasi wowote. Hata hivyo, kutokana na maneno mazito na yakutisha aliyokuwa akiyatoa, polisi walilazimika kuwaondoa baadhi ya watu katika chumba cha mahojiano. Watu walioshuhudia mahojiano hayo , waliiambia Nipashe kuwa, Ramadhani aliwaeleza polisi kwamba, anamiliki vichwa hivyo 50 kwenye maeneo tofauti hapa jijini Dar es Salaam na mkoani Mtwara alikodai alikuwa akiishi na baba yake mzazi.
Aidha, alidai kuwa ametega`kombora` la kichawi la kusababisha ajali katika barabara ya Morogoro pembezoni mwa daraja la Manzese ambalo hutumiwa na watembea kwa miguu. Madai hayo yaliungwa mkono na majirani wa sehemu aliyokuwa akiishi kijana huyo, eneo la Segerea kwa Bibi. Mmoja wa majirani hao, Bw. Sadi Marando, alidai kuwa, kijana huyo alimweleza kwamba, kila baada ya miezi mitatu, hupata kiu ya kunywa damu ya mtu.
Bw. Marando, amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kumshikilia mama wa kijana huyo kwa madai kwamba, Ramadhani alikuwa akisema siku zote kwamba, kazi zote za ushirikina hushirikiana na mama yake Khadija Ally. ``Kijana yule ni hatari ukisikiliza masimulizi yake unaweza kukimbia, hapa mtaani alikuwa na maisha ambayo kwa kweli yalikuwa ya kutisha, si mtu wa kawaida,`` alidai Bw. Marando.
Bw. Marando, alisema kutokana na kijana huyo kutoonekana kama binadamu wa kawaida, majirani walikuwa wakimhoji kila mara na kuna siku alisema kwamba wanacho kikundi chao chenye watu 10 akiwemo mama yake na kwamba yeye ndiye kiongozi.
Alisema katika mfululizo wa vituko vya kijana huyo, Alhamis iliyopita alitaka kumchinja mdogo wake, Pascal Lucas. ``Alikuwa ameshamkanyaga chini kama kuku na kuanza kumchinja, bahati nzuri majirani wakafanikiwa kumkamata, nadhani kiu ya damu iliendelea ndiyo maana alimteka na baadaye kumuua Salome,`` alisema Bw. Marando.
Ramadhani amenukuliwa akisema kwamba `makao makuu` ya kundi hilo yako mkoani Mtwara na wameweka `matawi` maeneo ya Manzese Darajani na Buguruni, jijini Dar es Salaam. Polisi mmoja wa kituo cha Stakishari aliyeomba jina lake lisitajwe, alisema Ramadhani bila woga amesisitiza kwamba, si mara yake ya kwanza kula nyama ya mtu na kwamba ataendelea kwa vile nyama za watu ndizo humpa nguvu katika mambo ya kishirikina.
Hata hivyo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Bw. Charles Mkumbo, alisema upelelezi na maneno yaliyozungumzwa na kijana huyo ni siri yao kwa ajili ya kutengeneza kesi. Alisema hata kama kijana huyo anadaiwa kutoa maneno hayo, polisi hawatishiki na watamfungulia kesi kama muuaji wa kawaida. ``Tunachopeleleza sasa ni siri yetu, tunatafuta ushahidi na kujua mazingira ya tukio hilo na sisi tutamshughulikia kama muuaji mwingine yeyote na kamwe suala la uchawi kwetu halipo,`` alisema Kamanda Mkumbo. Alipoulizwa kwamba kama polisi hawasadiki taarifa za uchawi ni kwanini wanawashikilia wazazi wa kijana huyo, Kamanda Mkumbo alijibu kwamba, wanawashikilia kwa kutambua kuwa, huenda wanajua mengi juu ya mtoto wao kutokana na kuishi naye kwa muda wote. Kuhusu mazishi ya marehemu mtoto Salome, Kamanda huyo alisema polisi haina neno juu ya hilo bali inasubiri taratibu za maziko zitangazwe na familia. Hata hivyo, alisisitiza kwamba, kabla ya maziko, lazima mwili wa marehemu ufanyiwe uchunguzi ambapo polisi wameomba ndugu wapeleke mwakilishi atakeyeshuhudia. ``Ndugu wakiwa tayari, muda wowote waje tuwakabidhi mwili, lakini kwaza tutaufanyia auchunguzi,`` alisisitiza Kamanda. Nipashe ilitembelea familia ya marehemu huyo huku mama na baba wa mtoto aliyeuawa kwa kuchinjwa, wakiwa wamegubikwa kwa majonzi. Mama wa mtoto huyo, Bi. Pendo Dunstan, alisema majonzi aliyo nayo hawezi kuyaelezea. ``Ni Mungu tu anayejua moyo wangu unaugua kwa jinsi gani,`` alisema kwa masitiko makubwa. Naye baba wa marehemu, Bw. Yohane Majana, aliwataka polisi wamuachie huru kijana huyo anayedai kuwa ni mchawi ili na yeye amwonyeshe uchawi wa kisayansi. ``Wamwachie! Mimi naomba aachiwe huru ili nikutane naye ana kwa ana tuone,`` alisema.
Kuhusu mazishi, Bw. Majana alisema bado wanajikusanya ili kupata fedha hasa ikizingatiwa kwamba familia yao ni maskini. Alisema ndugu na jamaa walitarajiwa kukutana jana kwa ajili ya michango na kwamba wanatarajia mazishi yafanyike leo eneo la Segerea. Wakati huo huo, Godfrey Monyo na Karama Kenyunko wanaripoti kuwa, polisi jijini Dar es Salaam, inawashikilia wazazi wa mtoto aliyekutwa na kichwa cha mtoto katika mfuko wa rambo. Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Bw. Charles Mkumbo, alisema polisi wanaendelea na uchunguzi wa sakata hilo na kwa kuanzia wameanza kwa kuwashikilia wazazi wa mtoto huyo. ``Tumewashikilia wazazi wa mtoto aliyesababisha mauaji hayo na mtoto mwenyewe pia tunaye kwa hiyo tunaangalia nini kifanyike ili kubaini chanzo cha tatizo hilo,`` alisema. Kamanda Mkumbo alisemapolisi hawaamini kama suala hilo ni la uchawi bali ni tukio la uhalifu kama mengine na kuwataka wananchi kuwapa muda ili kulifanyia uchunguzi kwa kina.
Alisema uchunguzi utakapokamilika, watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara moja kujibu tuhuma hizo.
Jumamosi ya wiki iliyopita, kijana Mussa (18) anayedaiwa kuingia jijini Dar es Salaam akitokea Mtwara, alinaswa akiwa na kichwa cha mtoto. Mtoto huyo wa kike, Salome Yohana, alipotea nyumbani kwao Tabata Segerea, wiki iliyopita na baadaye kiwiliwili chake kilikutwa katika choo cha nyumba ya jirani kabla ya kupata taarifa za kuonekana kwa kichwa chake hospitali ya Taifa Muhimbili. source Nipashe

Neno la Leo

“Your attitude should be the same as that of Christ Jesus: Who, being in very nature God, did not consider equality with God something to be grasped, but made himself nothing, taking the very nature of a servant, being made in human likeness. And being found in appearance as a man, he humbled himself and became obedient to death— even death on a cross!”- Philippians 2:5-8

Precision yaja na BOEING 737-300

Abiria wakiwasili ktk jiji la Mwanza au Rock city. Captain Kalero Mkandawile na First Officer Owen Mshiu wakiwa tayari kuluka ktk Boeing 737-300 Kampuni ya Precision air leo imezindua ndege yake mpya ya Boeing 737-300 yenye uwezo wa kuchukua abiria 116, hii ni ndege ya kwanza kubwa na yenye uwezo wa kuchukua abiria wengi kwa kampuni hii

April 27, 2008

Hii inasikitisha sana jamani. ni KALI YA KARNE.

Huyu ni mmoja kati ya wale vijana waliodaiwa kuanguka kimiujiza pale Mikochen B Assemblies of God kwa Mchungaji Dr Getrude Lwakatare, ila mamlaka zilidai kuwa ni matapeli na hivyo kuonekana kana kwamba Mch. Dr Lwakatare alikuwa amepanga nao, lakini Mungu kadhiirisha ukuu wake.
Hii ni kali ya karne.
Kijana akamatwa na kichwa akifyonza damu
Ramadhani Musa (18) anayedaiwa kuingia Dar es Salaam juzi akitokea Mtwara, amenaswa akiwa na kichwa cha mtoto mdogo. Mtuhumiwa alikamatwa na walinzi wa Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili (MUHAS) jijini Dar es Salaam jana asubuhi akijaribu kukipitisha kwa staili.
Akiwa na kifurushi aliwahadaa walinzi kuwa anakwenda kumuona shangazi yake, hata hivyo walimshtukia baada ya kuona damu zimetapakaa mdomoni.
Walipokagua kifurushi walikuta kichwa cha mtoto wa kike aliyekuwa amesukwa mtindo wa `twende kilioni` kikichuruizika damu. ``Kijana huyo alikichukua mbele ya walinzi hao na kuanza kufyonza damu na kujilamba midomo, `` alidai mlinzi na kuongeza kuwa aliwauliza kwa ujasiri mnashangaa nini? ``Kwetu ni kitu cha kawaida kula nyama za watu.`` Ofisa Upelelezi wa Mkoa wa Ilala wa Bw. Charles Chambo, alithibitisha kutokea kwa mkasa huo na kueleza kuwa kichwa hicho ni cha Salome Yohana (3).
Kwa mujibu wa mama Salome, Bi. Pendo Dutsan, binti yake alitoweka juzi usiku nyumbani kwa shangazi yake anayeishi Segerea na kwamba kabla ya kuishia alikuwa akicheza nje ya nyumba yao.
Waligundua kuwa hayupo wakati wa chakula cha jioni na kuanza kumtafuta lakini bila ya mafanikio hadi jana asubuhi, mgeni wa jirani yao aliyetajwa kwa jina la Lucas Kibaya, alipogundua kiwiliwili chake chooni. Alidai Kibaya aliingia chooni na kukuta tofali limefunika tundu na alipoliondoa aliona kanga iliyokuwa na damu na kugundua kiwiliwili cha mtoto kilichonasa kwenye tundu hilo.
Baada ya kutoa taarifa, polisi wa kituo cha Stakishari Ukonga walifika na kuopoa kiwiliwili hicho na kutafuta gari ili kunyonya uchafu ili kutafuta kichwa ambacho kilikuwa hakionekani. ``Wakati tunaendelea kukisaka kichwa polisi walitueleza kuwa walipokea taarifa za kukamatwa kwa Musa akiwa na kichwa Muhimbili,`` alisema mwanamke huyo akilia kwa uchungu. Aliongeza kuwa polisi walikichukua kiwiliwili pamoja kuwakamata watuhumiwa ambapo mwili huo ulikuwa chooni kwao hadi kituo cha Stakishari.
Baada ya taarifa za kupatikana kichwa hicho, watuhumiwa ambao kiwiliwili kilikuwa nyumbani kwao walipelekwa Muhimbili hospitali walikoonyeshwa kichwa pamoja na `miliki.` Watuhumiwa hao Kibaya na mkewe Hadija Ali walimtambua kijana wao na kueleza kuwa alikuja Dar es Salaam Ijumaa, siku moja kabla ya tukio, akitokea Mtwara.
Hadija alidai walitengana na mzazi mwenzake (baba wa mtoto huyo) kwa miaka mingi na muda wote alikuwa akiishi Mtwara. Alisema Ramadhan alitoweka juzi jioni na alipigwa na butwaa baada ya kuona kuwa aliyekamatwa na kichwa cha Salome ni mwanae.
Mhudumu wa chumba cha maiti Muhimbili Bw. Mizome Gogo, alisema kichwa hicho kilifikishwa jana asubuhi na polisi na muda mfupi baadaye askari wa Stakishari waliwaletea kiwiliwili.

April 25, 2008

TICTS NA KARAMAGI

Karamagi akili bungeni kumiliki asilimia 35% ya hisa za TICTS na kuwa yeye ndo mwenyekiti huku waheshimiwa akiwemo Mh Chenge aka "Vijisenti" na Rostam Azizi wakifuatilia kwa makini.

Mrs Pinda

Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda (kushoto) akitoka kwenye ukumbi wa bunge mjini Dodoma jana baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu.

Mambo ya Mswati hayooo

Mambo ya mila na utamaduni wa Bondeni kwa Mfalme Mswati, kila mwaka jamaa anakazi ya kuchagua mwali mpya kabisa wa kuoa. King Mswati alianza kutawala Swaziland mwaka 1986 ana umri wa miaka 40 na mpaka sasa ana wake 13 na anauhakika wa kuoa mke 1 kila mwaka, je akifanikiwa kufikisha miaka 100 atakuwa na wake wangapi?

TABATA DAMPO-Mshiko WAKARIBIA

Wakazi wa Tabata Dampo waliovunjiwa nyumba zao kinyume cha sheria na kinyama watalipwa mshiko wao hivi karibuni baada ya zoezi la kutambua wamiliki halali wa nyumba na wenye leseni za makazi kufanyika leo hii.

Wesley Snipes afungwa

Wesley Snipes amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu kwenye gereza la serikali (federal). Kisa hakulipa kodi aliyostahili kulipa! Denzel Washington alikuwa mahakamani akitoa shuhuda kuhusu jinsi Snipes alivyo mtu mwema. Pia Woody Harrelson alitoa shuhuda. Snipes mwenyewe alimwomba hakimu amwonee huruma! Lakini wapi! Jaji kampa kifungo cha juu kabisa miaka mitatu. Alisema awe mfano kwa wengine!
Kwa hisani ya Dada Chemi.

Neno la Leo

“To them God has chosen to make known among the Gentiles the glorious riches of this mystery, which is Christ in you, the hope of glory. We proclaim him, admonishing and teaching everyone with all wisdom, so that we may present everyone perfect in Christ.”- Colossians 1:27-28

April 24, 2008

mashujaa JWTZ warudi

Baadhi ya askari na maafisa wa jeshi waliokuwa wakishiriki katika oparesheni ya kumuondoa muasi wa kisiwa cha Anjouani Kanali Mohamed Bacar wakipita mbele ya mgeni Rasmi Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa, Dk Hussein Mwinyi (hayupo pichani) wakati ya mapokezi ya askari hao jana jijini Dar es Salaam.

Mkonga wa MAWASILIANO

ULE MKONGA WA MAWASILIANO WA CHINI YA BAHARI KWA NCHI ZA AFRICA UTAKAMILIKA KABLA YA 2010 NA HIVYO KUTUWEZESHA KULIONA KOMBE LA DUNIA KWA URAISI ZAIDI KULIKO SASA AMBAPO MAWASILIANO YANATUMIA SATELAITE. Wataalamu wa mambo hayo Bw Simon na John Sihra juu.

WE KP WEWE, WE HAYA TU!!!

Enzi zetu

Nini kilikuwa chajadiliwa hapa?

Guu la Kibongo Ohh

April 23, 2008

JK, JENS na Uzazi Salama

uzinduzi wa kampeni ya mkakati wa kupunguza vifo vya akina mama na watoto wa chini ya umri wa miaka mitano kuanzia mwaka 2008-2015.
( National Road Map Strategic Plan to Accelerate Reduction of Maternal, Newborn and Child Deaths in Tanzania 2008-2015 ) mkakati huo unaoendwshwa na Wizara ya afya na ustawi wa jamii ulizinduliwa jana jijini dar na rais jakaya kikwete kwa kushirikiana na waziri mkuu wa norway Jens Stoltenberg jijini ambae alikuwa katika ziara ya siku mbili nchini.

TBL NA WAJANE

Ofisa Tarafa ya Ilala, Bw. Suleiman Mwenda. akimkabidhi mmoja wa wanachama wa kikundi cha Wanawake Wajane cha The Good News Social Welfare Organisation (GOSOWO), Bibi Haruna Shamte cheti cha kuhitimu mafunzo ya kudarizi nguo pamoja na kutengeneza batiki yaliyogharamiwa hivi karibuni na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Wanaoshuhudia hafla hiyo iliyofanyika Vingunguti, Dar es Salaam jana, ambapo pia TBL iliwakabidhi msaada wa vyerehani vyenye thamani ya sh. milioni 4 ni Ofisa Uhusiano wa TBL, Bi. Dorris Malulu (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa GOSOWO, Bw. Frank Mshahara.
Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bi. Dorris Malulu akifurahia kuona kitenge cha batiki chenye jina la kampuni hiyo baada ya kukabidhiwa zawadi na Kikundi cha Wanawake Wajane cha The Good News Social Welfare Organisation (GOSOWO), baada ya kukipatia msaada wa vyerehani vya thamani ya sh. milioni 4 pamoja na kuwagharamia sh. milioni 1.5 za mafunzo ya kudarizi na kutengeneza nguo za batiki. Kulia ni Ofisa Tarafa ya Ilala, Bw. Suleiman Mwenda

April 21, 2008

Washika Kalamu Mjengoni

Baadhi ya washika kalamu wanaoripoti yanayojili mjengoni.

KWA KINA BABA TUUUU!

Kina baba mmeipata hii? najua wengine leo au jana baada ya kusoma habari hii mmeanza kuwaangalia wanenu au mlioambiwa wanenu kwa macho mawilimawili, hayo ndo mambo ya tekonologia ya kisasa au kipimo kinachoitwa DNA kinavyosema kwa ndoa zilizopimwa au walokuwa na mashaka na wenza wao.

Atimaye Chenge abwaga manyanga.

Rais akubali kujiuzulu kwa Chenge Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo April 20, 2008, amepokea barua kutoka kwa Waziri wa Miundo Mbinu, Mheshimiwa Andrew Chenge ya kujiuzulu wadhifa wake na Rais amekubali ombi hilo la kujiuzulu. Rais ameuelezea uamuzi huo wa Mhe Chenge kama uamuzi wa busara kwa kutilia maanani mazingira ya sasa. Katika barua yake kwa Rais, Mhe Chenge amesema kuwa pamoja na kwamba shutuma dhidi yake bado zinachunguzwa, mapenzi yake kwa nchi na chama chake, yamemsukuma kujiweka pembeni. Mhe Chenge ni Mbunge wa Bariadi Magharibi. Mwisho Imetolewa na Ikulu, 20th April, 2008

Buriani Braza Dito

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ukiwaona Ramadhani Ditopile au Braza Dito anatarajiwa kuzikwa leo mchana huko Kinyerezi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, Marehemu Dito alifariki saa 2:30 asubui jana ktk hoteli ya Hilux mji kasoro bahari alikofikia na mke mdogo.

April 19, 2008

NENO LA LEO

“But Christ has indeed been raised from the dead, the firstfruits of those who have fallen asleep. For since death came through a man, the resurrection of the dead comes also through a man. For as in Adam all die, so in Christ all will be made alive.”- 1 Corinthians 15:20-22

kipanya leo

WAWAZA NINI HAWA????

SIKU YA KUAPISHA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI KENYA KILA MTU AONESHA YUKO MBALI NA SHUGHURI YENYEWE. WHY??????

ALA KUMBE!!!!! 3G

Mambo ya 3G na voda hayo, wamwona live unayeongea naye kwenye simu, Onyo wale jamaa zangu mlozoea kucheat au kuongopa hii haikufai kwani utaonekana pale ulipo na unayeongea naye. so please take care. Mambo ya VODACOM HAYO.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...