September 10, 2009

JK-"Sina urafiki wala Undugu na Fisadi"

JK Live

Hizi ni baadhi ya nukuu muhimu

Richmond na Kagoda

“Kwenye kupambana na Ufisadi na rushwa sina urafiki wala ndugu”

Ni kweli Richmond ilikuwa ni Ghost Company au maruani, Nililiona tatizo toka mwanzo nikamwagiza waziri wa Fedha, usiwachukulie dhamana hawa”

Ni kweli Kuna matatizo katika kuwachukulia hatua maafisa waliohusika na sakata zima hili kikao cha bunge cha Novemba kitakuwa na majibu ya hili”

Nyalaka za dini

“Zimetustusha na kutusikitisha sana, lakini ofu yetu ni uchaguzi ujao wa 2010 kwamba kwa sasa watu watapiga kula kwa maelekezo ya viongozi wao wa dini, nathani hii si sahihi, tutakaa chini na viongozi hawa tuzungumze nao”

Mafisadi Papa

Mafisadi wakubwa wana maarifa makubwa pia ya kujificha, hataivyo tunafanya juhudi kubwa kupamba nao”

Uhasama wa Wabunge wa CCM

“Kumekuwa na chuki mza wazi kati ya wabunge wa CCM na serikali yao na hata wabunge kwa wabunge wenyewe kiasi cha mtu kutoaminiana

Kuacha kinywaji chako kwa ofu kuwa utawekewa kitu kibaya”

Tumeunda timu ya wazee watatu Mzee Mwinyi, Mkapa na Kinana ili kuangalia hilo

Mafuta Zenji

Hatuna sababu ya kulumbana juu ya hili, linajadilika na laweza kuondolewa kama lilivyoingizwa katika mambo ya muungano mwaka ule 1968”

Kesi ya Zombe

Sheria imechukiua mkondo wake, lakini sisi kama serikali hatukulidhika hivyo tumekata rufaa juu ya maamuzi ya kesi hile mahakama ya rufaa”

Mikoa ya pembezoni

Kwangu hakuna mikoa ya pembezoni, juhudi za makusudi zinafanywa kuwaunganisha mikoa yote kwa lami, hasa Kigoma, Kagera na Lindi, wamechelewa lakini si kwamba tumewatupa, hakuna tuliyempuuza”

Uhuru wa Vyomba vya habari

“Mfumo wenye uhuru wa kusema, watu kutoa maoni yao naupenda sana kuliko wa kuwabana watu, na sitofanya jitihada za kuzuia uhuru huo maadamu unafata maadili ya uhandishi”

Migomo

“Migomo ni haki ya wafanyakazi, hainisumbui”

Kuwaziba midomo wabunge wa CCM

“Hakuna jitihada zozote za kuwaziba wabunge midomo, tunataka waseme, waikoseo serikali yao.

Shule za kata

“Ni kweli kuna tatizo la utekelzaji wake lakini tunafanya jitihada za dhati kuondoa hilo, likiwemo la Walimu, Vifaa vya kufudishia, vitabu na vifaa vya maabara”.

Maisha Bora kwa kila Mtanzania

“Kwetu hii ni mambo mawili, kwanza huduma za kijamii na kiuchumi na pili kuongezeka kwa kipato, tunajitahidi katika huduma za jamii kama afya, elimu, maji na miundombinu na katika kuongeza kipato tatizo kubwa ni mfumuko wa bei, hili ni tatizo kubwa sana, na kiini chake ni bei za vyakula, tunapamba nalo hili tulikuwa na SDP na sasa tumeanzisah Kilimo Kwanza lengo likiwa kujaribu kupambana na hili.”

Safari za Nje.

“Nasafiri kwa manufaa ya Taifa, Misaada yote tuliyopata inatikana na safari hizi, ukijifungia ndani utapata wapi haya? Zinafaida nyingi sana hizi.

Muulize Rais

“Mfumo huu ni kitu kipya na kimekuwa na manufaa sana, na nadhani ni wazo zuri na nitaliemdeleza, huu ni mwanzo tu”

HAYA NI BAADHI YA YALE NILIYOWEZA KUYANASA NA KUNUKU.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...