September 26, 2011

NEC WEBSITE KULIKONI?

Hii ni screen shot ya Wavuti ya Tume ya Uchaguzi iliyopigwa saa 12:03 jioni hii, nilitarajia kukuta updates zozote kuhusiana na yale yanayojiri yanayowahusu, lakini iki ndicho kilicho hapo.
]
Update pekee inayoonekana baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana ni sentensi hii yenye maneno yapatayo 19:- "Tume ya Taifa ya Uchaguzi Yatangaza Ratiba ya Uchaguzi wa JImbo la Igunga pamoja na Chaguzi Ndogo za Madiwani"



Hata kwa sentensi hii mtu alitarajia kupata hiyo ratiba inayosemwa, lakini sivyo ilivyo. Mtu anajiuliza kulikoni huko NEC? yaani toka mwaka jana hakuna lolote lililotokea kuhusiana nanyi litupasalo wanachi kuhabarishwa? mtu aliyeikumbuka website hii na kupost hako ka-update ka maneno 19 ilimchukua muda gani hata kushindwa kuweka taarifa kamili?

  Hii yasikitisha kwa kweli, karne hii ya 21 na Zama hizi za Taarifa (Information Age) bado asasi muhimu kama hii inashindwa kuitumia ipaswavyo, mtu alitarajia loe hii kuwe si tu na ratiba bali majina, picha za wagombea na vyama na pengine taarifa kuhusu idadi halisi ya wapiga kura, vituo, na mambo mengine kama hayo.

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...