October 19, 2011

JK, LOWASSA MTEGONI1


DHANA ya kujivua gamba iliyoasisiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, na ambayo hivi karibuni ilimng’oa aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, imeingia katika hatua ngumu ya utekelezaji wake, Tanzania Daima Jumatano, limebaini.


 Ugumu wa hatua ya sasa unatajwa na wafuatiliaji wa siasa za ndani za CCM kuwa unasababishwa na mwelekeo wa dhana hiyo kuonekana ukielekea kumlenga Waziri Mkuu wa zamani ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa.

 Kuibuka upya kwa siasa zenye mwelekeo wa uhasama mkali kati ya kundi moja la viongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na Katibu wa Uenezi na Itikadi wa chama hicho, Nape Nnauye, kunaelezwa kuwa ni matokeo ya mwelekeo wa sasa wa dhana hiyo.

 Viongozi hao wa vijana wanaoongozwa na Kaimu Mwenyekiti wao wa Taifa, Benno Malisa, anayeungwa mkono na Mwenyekiti wa UVCCM wa Mkoa wa Arusha, James Millya, wanatajwa kuwa watu ambao wamekuwa wakipinga harakati zinazopigiwa chapuo na Nape za kuendelea kwa utekelezaji wa dhana hiyo ya kujivua gamba.

 Wakati Nape na wana CCM wengine wenye msimamo kama wake wakiitaja hatua ya Benno, Millya na vijana wenzao wa Arusha kuwa inayolenga kukwamisha utekelezaji wa dhana hiyo, kundi hilo linalompinga linamtuhumu kwa kukivuruga chama chao kwa maslahi yake binafsi.
 Sakata hili jipya liliibuka baada ya Benno kuliongoza kundi kubwa la vijana wa chama hicho kufanya maandamano katika jiji la Arusha hivi karibuni yaliyomalizika kwa kauli nzito kutoka kwao ambao mbali ya kuelekezwa kwa Nape zilimtuhumu pasipo kumtaja kwa jina mtoto mmoja wa kigogo kuwa alikuwa nyuma ya mpango wa kuwazuia kutekeleza ajenda yao.

 Hatua hiyo ya Benno ambayo baadhi ya wadadisi wa mambo wanaifananisha kuwa ni kubadili mwelekeo wa mapambano ya kisiasa inamweka mwanasiasa huyo kijana katika kundi la watu wanaopinga hatua zozote za kujaribu kumng’oa Lowassa katika uongozi wa chama hicho.

source Tanzania Daima. 

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...