October 19, 2011

Mwezi wa 11 twaambia hakuna sababu kuondoa noti za "zamani"- BOT


Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imesema haujafika wakati wa kutangaza muda wa mwisho wa matumizi ya noti za zamani, kwa vile watu wanaozimiliki kwenye mzunguko bado ni wengi.
Mkurugenzi wa Huduma za Kibenki na Mambo ya Sarafu wa BoT, Emmanuel Boaz, alisema hayo jijini Dar es Saalam jana alipozungumza na NIPASHE kwa niaba ya Gavana wa Benki hiyo, Profesa Benno Ndulu.

Alisema watautangazia umma utaratibu wa kurudisha noti hizo ili kuziharibu wakati zitakapobaki chache kwenye mzunguko.

Hata hivyo, hakuwa tayari kueleza kiasi cha noti hizo zilizoko mikononi mwa watu kwenye mzunguko kwa maelezo kwamba, suala hilo ni la ndani ya BoT.

“Tunajua hela yote iliyopo kwenye mzunguko na iliyopo Benki Kuu. Ikifika muda tutatangaza utaratibu wa kuzirudisha zikibaki chache bila kuwaletea wananchi usumbufu,” alisema Boaz.
Alisema baada ya kutoa noti mpya, hawakuona sababu ya kuutangazia umma kuwataka kurejesha zile za zamani kwa kuepuka msongamano wa watu, ambao ungejitokeza kwenye mabenki, hali ambayo ingewaletea wananchi usumbufu mkubwa.

Kutokana na hali hiyo, alisema noti hizo, ambazo ni za thamani ya Sh. 500, 1,000, 5,000 na 10,000, bado ni fedha halali kama walivyokwisha kutangaza huko nyuma, ambapo alisema hawakuwahi kutangaza muda wa mwisho wa kukoma matumizi yake.
source: Nipashe

Hivi sasa unaposema noti za zamani mtu anachanganyikiwa, maana zilizotolewa kabla ya hizi za Mwezi january ni mpya zaidi ya hizi zinazoitwa mpya, kwa msimammo huu Tanzania tutaendela kuwa na noti mbili mbili, lakini ambazo hazikai mifukoni mwetu, bila shaka haya ni maendeleo, na pengine ndiyo tunayoyataka. 


Mungu Ibariki Bongo Yetu.  

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...