JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
Agosti16, 2008
PRESS RELEASE
Mkuu wa Chuo cha Kijeshi (TMA), Monduli Arusha, Brigedia Jenerali January Nyambibo amefariki Dunia katika Hospitali Kuu ya Kijeshi Lugalo Agosti 15, 2008 kwa ugonjwa.
Mipango ya mazishi inafanywa na Makao Makuu ya Jeshi kwa kushirikiana na familia yake. Msiba uko nyumbani kwa kaka yake Luteni Kanali Mstaafu Jackton Nyambibo, Gongo la Mboto Ukonga jijini Dar es Salaam karibu na hospitali ya Mather Care.
Marehemu atazikwa kwa heshima zote za kijeshi Jumatatu, Agosti 18, 2008 saa kumi alasiri katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Wakati wa uhai wake, Brigedia Jenerali Nyambibo alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo, Msaidizi wa Mnadhimu Mkuu, Mkufunzi Mkuu TMA na Shule ya Mafunzo ya Infantria (SMI) Mgulani, Mwambata Jeshi nchini Msumbiji na Mkuu wa Chuo TMA wadhifa aliokuwa nao hadi alipofariki dunia.
Marehemu Nyambibo alizaliwa mkoani Mara mwaka 1953 na kupata elimu yake ya msingi na Sekondari mkoani Mara hadi mwaka 1971 alipojiunga na Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Wakati wa utumishi wake jeshini, marehemu alipandishwa vyeo katika ngazi mbalimbali na kupata cheo cha Brigedia Jenerali Agosti 30, 2006 cheo alichofariki nacho.
Brigedia Jenerali Nyambibo atakumbukwa kwa mchango wake alioutoa wakati wa ukombozi Kusini mwa Afrika pale alipokuwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha Mgagao mkoani Iringa kilichokuwa na jukumu la kuwafundisha wapigania uhuru wa Chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini.
Imetolewa na Kitengo cha Habari
Makao Makuu ya Jeshi
Upanga, Dar es Salaam
RIP.
August 17, 2008
Brig General Nyambibo atunaye tena
JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
Agosti16, 2008
PRESS RELEASE
Mkuu wa Chuo cha Kijeshi (TMA), Monduli Arusha, Brigedia Jenerali January Nyambibo amefariki Dunia katika Hospitali Kuu ya Kijeshi Lugalo Agosti 15, 2008 kwa ugonjwa.
Mipango ya mazishi inafanywa na Makao Makuu ya Jeshi kwa kushirikiana na familia yake. Msiba uko nyumbani kwa kaka yake Luteni Kanali Mstaafu Jackton Nyambibo, Gongo la Mboto Ukonga jijini Dar es Salaam karibu na hospitali ya Mather Care.
Marehemu atazikwa kwa heshima zote za kijeshi Jumatatu, Agosti 18, 2008 saa kumi alasiri katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Wakati wa uhai wake, Brigedia Jenerali Nyambibo alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo, Msaidizi wa Mnadhimu Mkuu, Mkufunzi Mkuu TMA na Shule ya Mafunzo ya Infantria (SMI) Mgulani, Mwambata Jeshi nchini Msumbiji na Mkuu wa Chuo TMA wadhifa aliokuwa nao hadi alipofariki dunia.
Marehemu Nyambibo alizaliwa mkoani Mara mwaka 1953 na kupata elimu yake ya msingi na Sekondari mkoani Mara hadi mwaka 1971 alipojiunga na Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Wakati wa utumishi wake jeshini, marehemu alipandishwa vyeo katika ngazi mbalimbali na kupata cheo cha Brigedia Jenerali Agosti 30, 2006 cheo alichofariki nacho.
Brigedia Jenerali Nyambibo atakumbukwa kwa mchango wake alioutoa wakati wa ukombozi Kusini mwa Afrika pale alipokuwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha Mgagao mkoani Iringa kilichokuwa na jukumu la kuwafundisha wapigania uhuru wa Chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini.
Imetolewa na Kitengo cha Habari
Makao Makuu ya Jeshi
Upanga, Dar es Salaam
RIP.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
There has been resurgence in the number of registered divorces in the country in the past two years after declining between 2005 and 2006. ...
-
Tarime — FELISTA Laurent (15) had not been admitted to hospital in her life, until November 4, this year, when she was attacked by his fath...
-
But while the suspect was being attended to in one of the wards at Leratong Hospital in Krugersdorp, west of Johannesburg, the on-...
-
TRA YA NCHI JIRANI YAPONDA PONDA MAGARI YALOSHINDWA KUKOMBOLEWA BANDARINI, MAGARI YAPATAYO 200 KUPONDWA DESEMBA HII, JE HUKU NI KUWA NA AK...
-
Archbisop of Australia Philip Aspinall briefs journalists on The Primates 2007 meeeting just ended yesterday at one of the Beach Hotel in D...
-
Tuna kila sababu kumshukuru Mungu kwa kutufikisha hapa tulipo, miaka mitano si mingi sana lakini kwa taasisi takatifu ni miaka mingi sana,...
-
Shirika la habari la Uholanzi Radio Netherlands Worldwide limeipa shavu picha hii na kushika nafasi ya tano katika shindano lake la hivi kar...
No comments:
Post a Comment