August 17, 2008
Brig General Nyambibo atunaye tena
JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
Agosti16, 2008
PRESS RELEASE
Mkuu wa Chuo cha Kijeshi (TMA), Monduli Arusha, Brigedia Jenerali January Nyambibo amefariki Dunia katika Hospitali Kuu ya Kijeshi Lugalo Agosti 15, 2008 kwa ugonjwa.
Mipango ya mazishi inafanywa na Makao Makuu ya Jeshi kwa kushirikiana na familia yake. Msiba uko nyumbani kwa kaka yake Luteni Kanali Mstaafu Jackton Nyambibo, Gongo la Mboto Ukonga jijini Dar es Salaam karibu na hospitali ya Mather Care.
Marehemu atazikwa kwa heshima zote za kijeshi Jumatatu, Agosti 18, 2008 saa kumi alasiri katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Wakati wa uhai wake, Brigedia Jenerali Nyambibo alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo, Msaidizi wa Mnadhimu Mkuu, Mkufunzi Mkuu TMA na Shule ya Mafunzo ya Infantria (SMI) Mgulani, Mwambata Jeshi nchini Msumbiji na Mkuu wa Chuo TMA wadhifa aliokuwa nao hadi alipofariki dunia.
Marehemu Nyambibo alizaliwa mkoani Mara mwaka 1953 na kupata elimu yake ya msingi na Sekondari mkoani Mara hadi mwaka 1971 alipojiunga na Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Wakati wa utumishi wake jeshini, marehemu alipandishwa vyeo katika ngazi mbalimbali na kupata cheo cha Brigedia Jenerali Agosti 30, 2006 cheo alichofariki nacho.
Brigedia Jenerali Nyambibo atakumbukwa kwa mchango wake alioutoa wakati wa ukombozi Kusini mwa Afrika pale alipokuwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha Mgagao mkoani Iringa kilichokuwa na jukumu la kuwafundisha wapigania uhuru wa Chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini.
Imetolewa na Kitengo cha Habari
Makao Makuu ya Jeshi
Upanga, Dar es Salaam
RIP.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...
-
Dr H Mwakyembe akishushwa toka ktk ndege ya kukodi na kupelekwa moja kwa moja MOI kwa Matibabu zaidi, Dr Mwakyembe alipata ajali ya gari m...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
No comments:
Post a Comment