November 9, 2011

Mbeya kunani? Mlevi amuua polisi kwa kumtwanga vichwa baa



ASKARI Polisi wa Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya , amekufa baada ya kushambuliwa kwa kupigwa vichwa viwili na mmoja wa wateja wa baa ya Uzunguni wilayani humo juzi usiku.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Anacleti Malindisa alimtaja askari aliyeuawa ni Konstebo Ambros aliyekuwa na askari wenzake katika baa hiyo, kabla ya kushambuliwa na mtuhumiwa Nurdin Juma.

Akizungumzia tukio hilo, Malindisa alidai Juma aliwasili katika baa hiyo saa nne usiku ambapo alivua nguo zake zote, kubaki uchi wa mnyama na kuanza kupiga mateke viti vilivyokuwamo katika baa hiyo.

Alisema wakati akiendelea na shughuli ya kupiga viti mateke, ghafla alimvamia Ambros na kumshambulia kwa kumpiga vichwa viwili ambapo alianguka chini na kwamba askari wenzake walimchukua na kumkimbiza katika Hospitali ya Wilaya ambako alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.

Kaimu Kamanda alisema, wanamshikiliwa Juma na kwamba uchunguzi wa awali unaonesha kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa amelewa na kwamba uchunguzi zaidi unaendelea kuhusu tukio hilo.

Kadhalika alisema mipango ya kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda kwao mkoani Morogoro kwa ajili ya maziko inaendelea.

Source: Habari Leo.

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...