October 18, 2011

Babu wa Loliondo aibuka tena!


  • Adai kutafurika tena kama mwanzo
  • pia adai kuwa anahujumiwa. 



Mchungaji Masapila alisema bado anaoneshwa kuna watu watafurika tena Samunge kama ilivyokuwa awali.

"Hata mwanzo nilikuwa nawaeleza watu hapa kuwa wataona magari na mamia ya watu Samunge hawakuamini na wakaona pia wataona tena,"alisema Masapila.Hata hivyo, hakufafanua ni lini watu hao watafurika Samunge na watakwenda kutibiwa magonjwa gani.


Anunua magari ya kusaidia tiba akamilisha ujenzi wa nyumba yake.Katika kuhakikisha tiba ambayo inatoa inaendelea kuwa endelevu, Mchungaji Masapila amenunua gari aina ya Isuzu na Toyota Landcrusser kwa ajili ya kufuata dawa porini."Ni kweli nimenunua magari mawili ili yatoe huduma kwa kuwa siku hizi dawa zinapatikana mbali,"alisema Masapila.



Mchungaji Masapila ameishukuru Serikali kwa kuendelea kumuunga mkono na kumpa ulinzi jambo ambalo linaendelea kumpa moyo."Naishukuru sana serikali wakati wote wamenipa ushirikiano mkubwa na bado wanaendelea,"alisema Masapila.

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...