September 16, 2011

Mv Spice Islanders 1, Nahodha anasakwa.


JESHI la Polisi nchini limeanza kumtafuta nahodha wa meli ya mv Spice Islander iliyozama baharini katika eneo la Nungwi, Kaskazini Unguja usiku wa kuamkia Jumamosi. 

Taarifa ya Jeshi hilo iliyotolewa jana na Mkuu wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, ilimtaja nahodha huyo kwa jina la Said Kinyanyite, ambaye ni mkazi wa Nzasa Mbagala, Charambe, Temeke, Dar es Salaam. 

Mussa alisema nahodha huyo, ambaye hakuonekana baada ya ajali hiyo ni mzaliwa wa kijiji cha Mbwemkuru, Pande, Kilwa mkoani Lindi. 

Kamishna Mussa aliwaomba wananchi kupitia mpango wa Polisi Shirikishi Jamii, kutoa taarifa kituo chochote cha Polisi endapo watapata taarifa za alikojificha, ili akamatwe na kutoa maelezo ya jinsi ajali hiyo ilivyotokea. 

Taarifa hiyo ilisema tangu kuzama kwa mv Spice Islander, hajapatikana hali ambayo imewalazimu polisi kutafuta picha yake kwa lengo la kurahisisha utambuzi kwa watu wasiomfahamu wamwonapo. 

Katika hatua nyingine, kazi ya kuopoa miili ya walionasa kwenye mabaki ya meli hiyo iliyokuwa ikifanywa kwa ushirikiano wa wapiga mbizi wa Afrika Kusini na majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini, imeshindikana. 

Ofisa Habari wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Inspekta Mohammed Mhina, alisema kushindikana huko kumesababishwa na hali mbaya ya bahari na kina iliko meli hiyo tofauti na uwezo wa wazamiaji hao. 

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...