"Halloo!! shikamoo kaka, habari za leo, samahani nakuomba uje leo saa tano na nusu pale Ilala Boma CCM kutakuwa na............."
Hii ilikuwa ni sauti nyororo ya kubembeleza ambayo haikuwa ikiitaji utambulisho wowote uisikiapo mara upokeapo simu hasa kwa wanahabari wenzangu, ni sauti ya aina yake ambayo huwezi ifananisha na ingine au kuikosea na kama vile aliyekuwa anaitoa alikuwa akijua hivyo kwani ni aghalabu sana kusikia akijitambulisha.
Leo hii eti naambiwa sintoiskia tena abadani sauti hii? siamini!! eti ya kwamba imezimika ghafla kama kibatali au mshumaa uzimwao kwa hata kwa upope hafifu? hapana haiwezekani!! ati sasa waitwa marehemu? no haiwezekani!! mbona hukutupigia? mbona husitujulishe wadau wako kwa ile sauti yako nyororo ya kuwa watutoka? mbona husituage wadau wako Amina? Mbona ni mapema mno? yaani ndo kwanza jua lachomoza nawe waondoka? hukututendea haki washikadau.
Wanasema Mungu alikupenda zaidi? nakataa kuamini,, je ni kweli alikupenda mno kuliko vijana ulioapa kuwatetea na wakakuchagua kuwawakilisha? ni kweli alikupenda kuliko mwanao unayemwacha bila mama ktk umri mdogo hivi? Akili yangu ya kawaida yakataa kuamini, niwieni radhi kwa kutokuamini kwangu, pia nafahamu kazi ya Mungu haina makosa, lakini haa! sawa tutafanyaje!!
Imenichukua mda mrefu kuandika tanzia hii kwa kutoamini kwangu, nikidhani labda niko ktk ndoto ndefu na kwamba uenda nikiamka nitasikia tena sauti ile tamu ikinialika kwa ili au lile, sauti toka ktk sura ya tabasamu isiyo jua kununa, Lakini wapi siku zimepita na bado nasoma tanzia toka sehemu mbali mbali nami nalazimika kuamini japo kwa shingo upande kwamba ni kweli umetutoka Amina, waudaku walikufanya mradi, mamilion mengi wametengeneza kwa kupitia sura yako, kiasi najiuliza wapi watapata tena A.C mwingine? je ni nini wamekulipa A.C?
Yako mengi mno ya kuandika juu yako lakini itoshe kusema tu kwamba ulikuwa Kijana jasiri NA SHUJAA.
KWANGU NAAMINI UJAFA BADO BALI WAISHI. KWANI SHUJAA HUWA HAFI BALI ANAPUMZIKA TU.
July 2, 2007
"Halloo!! shikamoo kaka, habari za leo, samahani nakuomba uje leo saa tano na nusu pale Ilala Boma CCM kutakuwa na............."
Hii ilikuwa ni sauti nyororo ya kubembeleza ambayo haikuwa ikiitaji utambulisho wowote uisikiapo mara upokeapo simu hasa kwa wanahabari wenzangu, ni sauti ya aina yake ambayo huwezi ifananisha na ingine au kuikosea na kama vile aliyekuwa anaitoa alikuwa akijua hivyo kwani ni aghalabu sana kusikia akijitambulisha.
Leo hii eti naambiwa sintoiskia tena abadani sauti hii? siamini!! eti ya kwamba imezimika ghafla kama kibatali au mshumaa uzimwao kwa hata kwa upope hafifu? hapana haiwezekani!! ati sasa waitwa marehemu? no haiwezekani!! mbona hukutupigia? mbona husitujulishe wadau wako kwa ile sauti yako nyororo ya kuwa watutoka? mbona husituage wadau wako Amina? Mbona ni mapema mno? yaani ndo kwanza jua lachomoza nawe waondoka? hukututendea haki washikadau.
Wanasema Mungu alikupenda zaidi? nakataa kuamini,, je ni kweli alikupenda mno kuliko vijana ulioapa kuwatetea na wakakuchagua kuwawakilisha? ni kweli alikupenda kuliko mwanao unayemwacha bila mama ktk umri mdogo hivi? Akili yangu ya kawaida yakataa kuamini, niwieni radhi kwa kutokuamini kwangu, pia nafahamu kazi ya Mungu haina makosa, lakini haa! sawa tutafanyaje!!
Imenichukua mda mrefu kuandika tanzia hii kwa kutoamini kwangu, nikidhani labda niko ktk ndoto ndefu na kwamba uenda nikiamka nitasikia tena sauti ile tamu ikinialika kwa ili au lile, sauti toka ktk sura ya tabasamu isiyo jua kununa, Lakini wapi siku zimepita na bado nasoma tanzia toka sehemu mbali mbali nami nalazimika kuamini japo kwa shingo upande kwamba ni kweli umetutoka Amina, waudaku walikufanya mradi, mamilion mengi wametengeneza kwa kupitia sura yako, kiasi najiuliza wapi watapata tena A.C mwingine? je ni nini wamekulipa A.C?
Yako mengi mno ya kuandika juu yako lakini itoshe kusema tu kwamba ulikuwa Kijana jasiri NA SHUJAA.
KWANGU NAAMINI UJAFA BADO BALI WAISHI. KWANI SHUJAA HUWA HAFI BALI ANAPUMZIKA TU.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
There has been resurgence in the number of registered divorces in the country in the past two years after declining between 2005 and 2006. ...
-
Tarime — FELISTA Laurent (15) had not been admitted to hospital in her life, until November 4, this year, when she was attacked by his fath...
-
TRA YA NCHI JIRANI YAPONDA PONDA MAGARI YALOSHINDWA KUKOMBOLEWA BANDARINI, MAGARI YAPATAYO 200 KUPONDWA DESEMBA HII, JE HUKU NI KUWA NA AK...
-
Shirika la habari la Uholanzi Radio Netherlands Worldwide limeipa shavu picha hii na kushika nafasi ya tano katika shindano lake la hivi kar...
-
Habari wadau, Mnaweza shangaa leo kuja na uzi huu wa Saratani ya Utumbo mpana, kifupi mi si tatbibu na wala sina fani yoyote ya namna hi...
-
Kwa mujibu wa ripoti za Shirika la Afya Duniani vifo vitokanavyo na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, kitaalumu Noncommunicable Dise...
-
Jessica is recognized internationally as an inspirational keynote speaker. Born without arms, Jessica now flies airplanes, drives c...
-
But while the suspect was being attended to in one of the wards at Leratong Hospital in Krugersdorp, west of Johannesburg, the on-...
No comments:
Post a Comment