July 2, 2007
"Halloo!! shikamoo kaka, habari za leo, samahani nakuomba uje leo saa tano na nusu pale Ilala Boma CCM kutakuwa na............."
Hii ilikuwa ni sauti nyororo ya kubembeleza ambayo haikuwa ikiitaji utambulisho wowote uisikiapo mara upokeapo simu hasa kwa wanahabari wenzangu, ni sauti ya aina yake ambayo huwezi ifananisha na ingine au kuikosea na kama vile aliyekuwa anaitoa alikuwa akijua hivyo kwani ni aghalabu sana kusikia akijitambulisha.
Leo hii eti naambiwa sintoiskia tena abadani sauti hii? siamini!! eti ya kwamba imezimika ghafla kama kibatali au mshumaa uzimwao kwa hata kwa upope hafifu? hapana haiwezekani!! ati sasa waitwa marehemu? no haiwezekani!! mbona hukutupigia? mbona husitujulishe wadau wako kwa ile sauti yako nyororo ya kuwa watutoka? mbona husituage wadau wako Amina? Mbona ni mapema mno? yaani ndo kwanza jua lachomoza nawe waondoka? hukututendea haki washikadau.
Wanasema Mungu alikupenda zaidi? nakataa kuamini,, je ni kweli alikupenda mno kuliko vijana ulioapa kuwatetea na wakakuchagua kuwawakilisha? ni kweli alikupenda kuliko mwanao unayemwacha bila mama ktk umri mdogo hivi? Akili yangu ya kawaida yakataa kuamini, niwieni radhi kwa kutokuamini kwangu, pia nafahamu kazi ya Mungu haina makosa, lakini haa! sawa tutafanyaje!!
Imenichukua mda mrefu kuandika tanzia hii kwa kutoamini kwangu, nikidhani labda niko ktk ndoto ndefu na kwamba uenda nikiamka nitasikia tena sauti ile tamu ikinialika kwa ili au lile, sauti toka ktk sura ya tabasamu isiyo jua kununa, Lakini wapi siku zimepita na bado nasoma tanzia toka sehemu mbali mbali nami nalazimika kuamini japo kwa shingo upande kwamba ni kweli umetutoka Amina, waudaku walikufanya mradi, mamilion mengi wametengeneza kwa kupitia sura yako, kiasi najiuliza wapi watapata tena A.C mwingine? je ni nini wamekulipa A.C?
Yako mengi mno ya kuandika juu yako lakini itoshe kusema tu kwamba ulikuwa Kijana jasiri NA SHUJAA.
KWANGU NAAMINI UJAFA BADO BALI WAISHI. KWANI SHUJAA HUWA HAFI BALI ANAPUMZIKA TU.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
LONDON (Dow Jones)--U.K. defense giant BAE Systems PLC (BA.LN) Tuesday was fined GBP500,000 for improper accounting in relation to the award...
-
On Tuesday, 7th July we witnessed the peak of the Saba Saba festivities. I never go to the Dar es Salaam International Trade Fair, these day...
-
SAKATA LA RADAR BADO BICHI KABISA......... BAE in spotlight over Tanzania radar deal BAE Systems faces fresh controversy over foreign ar...
-
HII NI HOSTEL YA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI WANAPOISHI WATAALAMU WETU WA AFYA WA KESHO.
No comments:
Post a Comment