WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amesikitishwa na maisha wanayoishi wanafunzi wa Shule ya Msingi Mulusagamba iloyopo wilayani Ngara, Mkoa wa Kagera.
Pinda alionyesha masikitiko hayo jana baada ya kufika shuleni hapo na kuwaona wanafunzi wa shule hiyo wakitembea bila viatu huku sare zao za shule zikiwa chafu.
Waziri Mkuu huyo ambaye yuko katika ziara ya kiserikali katika Mkoa wa Kagera, alifika katika shule hiyo kwa ajili ya kupokea taarifa ya maendeleo ya Wilaya ya Ngara iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Salumu Nyakonji.
”Hali walionayo wanafunzi hawa ni mbaya sana kwani inaonekana kuchangiwa na umaskini unaowakabili wazazi wao.
“Ili kuondokana na hali hii lazima sasa viongozi wa wilaya muwe wabunifu, mbuni fursa mbalimbali zitakazowaongezea wananchi wastani wa kipato chao.
“Viongozi lazima mhakikishe wananchi wanaboresha kilimo ili kiwe na tija kwani kwa kufanya hivyo wataweza kukabiliana na umaskini wa kipato unaowakabili,” Alisema Pinda
Ili kuimarisha Kilimo Kwanza, aliwataka viongozi wilayani hapa wawahamasishe wananachi juu na manufaa ya kilimo cha kisasa kwa kufuata kanuni za kilimo.
March 10, 2011
Pinda ashangaa wanafunzi kukosa viatu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Invitation Photography Areas/Maeneo Thursday 17 th June/7 pm/Goethe-Institut Goethe-Institut presents Areas/Maeneo a platform for friend...
-
Mineral occurrence in Tanzania by TMAA UONGEZAJI WA PATO LA MTANZANIA Mheshimiwa Spika, 46. Lengo la Dir...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni-Kinondoni leo imeamua mazishi ya mwili wa Marehemu Paulo Goliama aliyefariki wiki iliyopita yafany...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...

No comments:
Post a Comment