October 27, 2011

Zitto Kabwe - Hali mbaya,



HALI ya Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ambaye alilazwa katika Hospitali ya Aga Khan, ilibadilika ghafla jana jioni kuhamishiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.Zitto alilazwa Aga Khan juzi jioni baada ya kusumbuliwa na maumivu ya kichwa kabla ya kuruhusiwa na kisha kurudishwa baada ya maumivu hayo kuendelea.

Kaka wa mbunge huyo, Salum Mohamed alisema jana jioni kwamba hali ya mdogo wake ilikuwa ikiendelea vyema lakini ilibadilika ghafla na kuanza kutetemeka.

“Hali yake ya Zitto imegeuka kuwa mbaya, anatetemeka mwili mzima na sasa tunampeleka Muhimbili kwa uangalizi zaidi,” alisema Mohamed.

Jana jioni, mwandishi wa gazeti hili alimtembelea Zitto Aga Khan jana majira ya saa kumi jioni na kumkuta akiwa anaendelea vyema. Zitto, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), alisema maeneo mengine katika mwili wake yalikuwa yamepona isipokuwa maumivu ya kichwa.

Awali, Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Chadema, Erasto Tumbo alisema Zitto anasumbuliwa na ugonjwa wa kipanda uso.

Aliwataka wanachama wake chama hicho, kumuombea kiongozi huyo ili apate nafuu na kushiriki kikamilifu kwenye vikao vya Bunge vinavyotarajiwa kuanza Oktoba 8, mwaka huu.

Source: Mwananchi.

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...