February 17, 2011

"Goms" si salama tena!

Wakati Makamu wa Rais Dr Ghalibu Bilali akioneshwa sehemu mabaki ya mabomu yaliyolipuka jana usiku, wakazi wa maeneo hayo wako kwenye pilika pilika za kuondoka maeneo hayo wakitafuta hifadhi popote watakapo pata, wengi wanaamini kuwa mabomu hayo uenda yakalipuka tena kama ilivyokuwa Mbagala hivyo ni heri nusu shari kuliko shari kamili.
Taarifa zimekuwa zikitolewa kuwa kuna watoto wengi wamepotea, wengi wako vituo vya polisi, uwanja wa Uhuru na Sabasaba, wito umetolewa waliopotelewa kwenda kuangalia ndugu na jamaa zao sehemu hizo.
Mpaka sasa idadi rasmi ya waliopoteza maisha kutokana na milipuko hiyo ya jana haijatolewa, inakisiwa kuwa wanaweza kufika mia moja, Waziri Mkuu amenukuliwa akisema ni zaidi ya ishirini na Mnadhimu Mkuu wa jeshi alinukuliwa na bbc kuwa ni 32, hakuna idadi rasmi mpaka sasa.
Tunawapa pole wale woote waliofikwa na majanga haya, waliojeruhiwa, waliofiwa na ndugu na jamaa zao pia, na zaidi tunawaombea heri marehemu wote, Mungu alaze roho za marehemu hao pema peponi. Amen.
Picha kwa hisani ya John Bukuku.

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...