"Jua lilee literemke mamaaa, mwezi naoo utelemkee mamaaa haiyahiyaa hiyaa hiyaaa mamaaaa.............."
Je wakumbuka nyimbo gani za mchakamchaka za enzi zile? au ni nini wakumbuka katika miaka ya sabini na themanini shule za msingi na sekondari? Wakti ule tulikuwa ukifika shule tu mwakimbia mchakamchaka na kuimba nyimbo kibao hivi bado yafanyika hayo?? Nakumbuka wakti tuko Sekondari Jite Best kulikuwa na mwalimu mmoja anaitwa GB alikuwa anakuja saa kumi na nusu na kugonga kengere na kiboko mkononi, ole wako ubakie bwenini ujifanye ujasikia, hizo bakora zake ni balaa, hivi vingalipo hivi??
Mazingaombwe mwayakumbuka??? wale wakongo walikuwa wanajifanya wanatengeneza pesa, vitambaa, kalamu, NK na ilikuwa unalipa kiingilio na mwatangaziwa shule nzima siku hiyo HAKUNA MASOMA, hivi waliishiaga wapi wale??
Mdau ni kitu gani wakumbuka???
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
At least 32 people have been killed in multiple explosions after an accident at a munitions dump in Tanzania's commercial capital, Dar e...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
KASHFA YA RICHMOND YAPELEKEA Lowassa kujiuzuru, hii ina maana gani wapendwa? je na baraza zima limepigwa chini au niaje? Pichani juu ak...
-
Hivi Daktari Bingwa ndo wale wanaoitwa SPESHALISTI? je waweza bashiri hii ni wapi ambapo walipa buku tu kumwona mtaalamu?
-
Bila shaka wapo ambao kwa kuona picha tu udenda wawadondoka hapo walipo, msihofu tembeleeni sabasaba kule karibu na banda la Heineken kwa w...
4 comments:
Imebidi nicheke maana umenikumbusha mbali,yaani huwa nikifikiria heka heka hizo za mchakamchaka na kadhalika najiuliza hivi tuliwezaje kusoma hizo shule na kuzimaliza?! Kweli jitahada na uvumilivu ni vitu muhimu!
Hata mimi nimecheka sana kwa kufurahi kuona bado kuna watu wanakumbuka nyimbo hizi. Ngoja nami nimekumbuka hii Iddi amin akifa mimi siwezi kulia nitamtupa Kagera awe chakula cha mamba
Sio siri umenikumbusha mbali saaaana yaani hakuna kitu nilikuwa sipendi ka mchakamchaka saa kumi na moja na kiwinta cha Moshi, yaani we acha tu.
Panda mlima panda, panda.... Si mchezo ilikuwa safi lakini. Ndhani shele za mijini mchaka mchaka hakunaga tangu siku hizo
Post a Comment