June 18, 2008
Karibu Bongo Kelly Rowland
Bila shaka utakuwa bado unalikumbuka kundi maarufu la muziki lililokuwa linajulikana kama Destiny’s Child kutoka nchini Marekani. Miongoni mwa mabinti waliokuwa wanaunda kundi hilo ni Kelly Rowland(pichani).Wenzake walikuwa ni Beyonce Knowles(mke wa Jay Z hivi sasa) na Michelle Williams. Kundi hilo lilivunjika rasmi mwaka 2005 ingawa mara moja moja bado huwa inatokea wakafanya maonyesho pamoja.
Baada ya kuvunjika kwa kundi lao na kila mmoja kuendelea kivyake na shughuli za kimuziki,uigizaji nk, Kelly Rowland amekuwa akijitolea sana kwa huduma za kijamii.Hali hiyo ndio imemfanya achaguliwe hivi karibuni kuwa Balozi wa Taasisi ya MTV Staying Alive ambayo imejikita katika kupigana vita na maradhi ya ukimwi pamoja na matokeo yake kama vile kuwanyanyapaa walioathirika nk.
Ni katika wadhifa huo wa “ubalozi” ambapo Kelly Rowland anatarajiwa kutua nchini Tanzania hivi leo ikiwa ni katika ziara yake katika nchi kadhaa za Afrika ikiwa na nia ya kueneza ujumbe na kuendeleza kazi za taasisi hiyo.
Kwa mujibu wa Meneja Uhusiano wa Kampuni ya MultiChoice Tanzania ambao ndio wenyeji wake,Kelly Rowland anatarajia kutembelea vituo kadhaa vinavyojishughulisha na mapambano dhidi ya ukimwi na pia kuzungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ziara yake. Akimaliza ziara yake nchini Tanzania,Kelly Rowland anatarajiwa kuelekea Kenya na kisha Ghana,Msumbiji na Angola.
Halafu bonyeza hapa uone jinsi mwanamuziki huyu na nduguze walivyopewa heka heka na nyani katika mojawapo ya nchi za kiafrika anazozitembelea.
By BC.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
At least 32 people have been killed in multiple explosions after an accident at a munitions dump in Tanzania's commercial capital, Dar e...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni-Kinondoni leo imeamua mazishi ya mwili wa Marehemu Paulo Goliama aliyefariki wiki iliyopita yafany...
-
Skandali ya BOT yazidi kuchemka.... NITOKE VIPI?????? BOT SAGA, MEGHJI AJIVUA.......... Meghji: I was duped by governor Ballali -Minist...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Edmark International founder, Chief Executive Officer and Chairman. Edmark Tanzania welcomes all entrepreneurs, business people a...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...


No comments:
Post a Comment