May 27, 2008
CHEE NKAPA AZOZA
RAIS Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa amevunja ukimya kuhusu tetesi na tuhuma kwamba alikiuka misingi na kujikita katika biashara wakati akiwa madarakani kwa kusema madai hayo si ya kweli na kwamba wanaomtuhumu wana chuki dhidi yake.
Akihutubia mwishoni mwa wiki katika Kijiji alichozaliwa cha Lupaso, Wilaya ya Masasi, Mkapa alisema wanaomtuhumu wanamchukia kwa kutowapendelea wakati wa utawala wake. Katika hotuba yake hiyo aliyoitoa wakati wa kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya tiba kwa Kituo cha Afya kinachomilikiwa na Kanisa la Katoliki kijijini hapo, alisema; “Msisikilize uongo huo kwa sababu hauna msingi wowote isipokuwa ni chuki …hasa inayotokana na watu ambao walifikiri nitawapendelea … sikuwapendelea,” alisema Mkapa huku akishangiliwa na wanakijiji wenzake waliohudhuria makabidhiano hayo.
Alisema kuwa yeye si tajiri na kwamba tuhuma hizo ni za uongo na hivyo kuwataka wananchi kuzipuuza kwa kuwa hazina msingi wowote wala chembe ya ukweli. “Sina uwezo wa fedha ingawa najua mnasikia na kusoma mengi …naishi kwa pensheni yangu kutoka serikalini kutokana na kuwa kiongozi kwa miaka 10 ambayo hata Mzee Mwinyi anaishi hivyo maana sisi sote ni wastaafu. Huo (uvumi) ni uongo …uongo ….uongo ….uongo …uongo….uongo….uongo,” alisema Mkapa na kuongeza; “Mimi si tajiri, nimeomba msaada nimepewa…nimejinyima mimi na mke wangu ndiyo tukaweza kugharimia kusafirisha vifaa hivi kutoka Canada hadi Dar es Salaam, kutoka hapo hadi hapa vimesafirishwa na Serikali…..sikuwa na uwezo wa kununua vifaa kama hivi. Nitapata wapi fedha za kununua vifaa kama hivi,” alisema Mkapa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
There has been resurgence in the number of registered divorces in the country in the past two years after declining between 2005 and 2006. ...
-
Tarime — FELISTA Laurent (15) had not been admitted to hospital in her life, until November 4, this year, when she was attacked by his fath...
-
TRA YA NCHI JIRANI YAPONDA PONDA MAGARI YALOSHINDWA KUKOMBOLEWA BANDARINI, MAGARI YAPATAYO 200 KUPONDWA DESEMBA HII, JE HUKU NI KUWA NA AK...
-
Shirika la habari la Uholanzi Radio Netherlands Worldwide limeipa shavu picha hii na kushika nafasi ya tano katika shindano lake la hivi kar...
-
Habari wadau, Mnaweza shangaa leo kuja na uzi huu wa Saratani ya Utumbo mpana, kifupi mi si tatbibu na wala sina fani yoyote ya namna hi...
-
Kwa mujibu wa ripoti za Shirika la Afya Duniani vifo vitokanavyo na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, kitaalumu Noncommunicable Dise...
-
Jessica is recognized internationally as an inspirational keynote speaker. Born without arms, Jessica now flies airplanes, drives c...
-
Hii ni repoti ya shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo na Viwanda inayoonyesha jinsi wataalamu wetu wanavyokimbia nchi yao na kwenda kuta...

1 comment:
Ebwana unatudanganya katika hiyo picha yako ya hapo pembeni. hivi unaweza kweli kupiga picha hapo ilhali jicho la kushoto lipo wazi?
Nipe jibu.
Post a Comment