Bongo tuna tatizo kubwa la bidhaa zisizo na ubora na "feki" nadhani ni tatizo kubwa sana au twaweza kuwa twaongoza africa *(sina hakika), kwa kweli hili ni tatizo kubwa ambalo lina madhala makubwa sana kwa walaji, ipo mamlaka ilopewa jukumu la kuteketeza bidhaa hizo iitwayo Fair Competition Commision, tatizo ni kuwa wana eneo dogo sana la kufanyia kazi, sheria inawarusu ktk maeneo ya uingizaji tu yaani kama Bandarini au Viwanja vya ndege tu, zikishaingia sokoni au madukani hawana tena meno huko.
Hizo bulb, TV na KIWI zote ni feki, ni vigumu sana kwa mlaji kutambua tofauti kati ya bidhaa halisi na FEKI, ukweli ni mtihani sana unapokwenda nunua kitu hasa kama watafuta halisi...
TATIZO HILI LITAKWISHA VIPI? TUSAIDIENI MAWAZO MLO UGHAIBUNI NAMNA GANI TUFANYE HAPA BONGO?
No comments:
Post a Comment