September 19, 2011

JK awasili New York.


JK akisalimiana na Maura Mwingira, mmoja ya maafisa ubalozini. 




JK akisalimiana na Dkt Rachel Mhaville ambaye ni daktari bingwa wa meno ya watoto, kwa mbaali anaonekana Mkumbwa Ali, Kaimu Mhariri Mtendaji wa Tanzania Standard Newspapers ltd, wachapishaji wa magazeti ya serikali, Daily News na Habari leo. 





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Jumapili amewasili New York, Marekani kuhudhuria Kikao cha 66 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) na kushiriki katika mikutano mingine ya viongozi wa nchi na Serikali yenye maslahi kwa Tanzania na Afrika.



Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, Mheshimiwa Rais Kikwete asubuhi ya leo,  Jumatatu, Septemba 19, 2011, atashiriki mkutano wa ufunguzi wa UNGA wa viongozi wa nchi na Serikali utakaojadili “Jinsi ya Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa Yasiyokuwa ya Kuambukiza (Prevention and Control of Non-Communicable Disease) ambayo ndiyo mada kuu ya majadiliano ya Baraza Kuu la UN mwaka huu.



 Rais Kikwete leo  pia atakuwa Mwenyekiti wa mkutano wa waandishi wa habari kuhusu Maendeleo ya Umoja wa Viongozi wa Afrika Kupambana na Malaria (African Leaders Malaria Alliance - ALMA) ambao yeye ni mwenyekiti.



Pamoja naye katika mkutano huo, miongoni mwa waalikwa wengine, watakuwa marais Paul Kagame wa Rwanda na Goodluck Jonathan wa Nigeria, na Rais wa zamani wa Marekani Mheshimiwa Bill Clinton.



 Rais Kikwete pia leo atashiriki katika Mkutano wa Mwaka wa Taasisi ya Rais Clinton ya Clinton Global Initiative, na atahudhuria mkutano maalum wenye mada ya Putting Teeth into Non-Communicable Disease unaondaliwa kwa pamoja na Tanzania, Australia na Sweden.



Baadaye jioni atakuwa msemaji mkuu katika hafla ya viongozi ya nchi na Serikali kusheherekea mafanikio ya muongo uliopita ya kupambana na ugonjwa wa malaria ulioandaliwa na taasisi ya Roll Back Malaria. Miongoni mwa watakaohudhuria halfa hiyo ni Naibu Katibu Mkuu wa UN, Mheshimiwa Asha Rose Migiro.



 Jumanne, Septemba 20, 2011, Rais Kikwete atashiriki katika mkutano wa viongozi wa nchi na Serikali kuhusu Lishe na baadaye mchana atajiunga na Katibu Mkuu wa UN, Mheshimiwa Ban Ki Moon kushiriki katika hafla ya viongozi iitwayo “Every Woman, Every Child Leaders Event”. Mchana, Mheshimiwa Rais Kikwete atashiriki katika tukio maalum la kujadili mikakati ya kimataifa kuhusu afya ya akinamama na watoto ya Global Strategy for Women’s and Children’s Health.



Asubuhi ya Jumatano, Septemba 21, 2011, Rais Kikwete atashiriki katika ufunguzi wa majadiliano ya mada kuu ya UNGA mwaka huu, pia atashiriki katika mjadala kuhusu hali ya chakula wa Beyond Food Security, na vile vile atashiriki katika mkutano wa viongozi wa Social Good Summit ambako atapewa tuzo maalum kutoka Umoja wa Mataifa kwa mchango wake mkubwa wa kuimarisha afya ya akinamama na watoto.



Baadaye mchana, Rais Kikwete atashiriki katika chakula cha mchana kilichoandaliwa na Mheshimiwa Ban Ki Moon kwa ajili ya viongozi wote wanaoshiriki katika mkutano wa 66 wa UNGA, na pia atashiriki katika tukio jingine kuhusu afya ya akinamama lililoandaliwa na Soko la Mitaji la NASDAQ.



Baadaye jioni ya siku hiyo atahudhuria hafla iliyoandaliwa na Rais Barack Obama wa Marekani kwa ajili ya viongozi wanaoshiriki mkutano wa mwaka huu wa Baraza Kuu la UN.



Asubuhi ya Alhamisi, Septemba 22, 2011, Rais Kikwete atahutububia UNGA akiwa msemaji wa pili wa siku hiyo baada ya nchi ya Cyprus, shughuli ambayo itafuatiwa na shughuli nyingine nyingi za mikutano na viongozi ukiwamo ule wa kuadhimisha miaka 10 ya Azimio la Durban kuhusu ubaguzi wa rangi. Ijumaa, Septemba 23, 2022, Rais Kikwete atashiriki katika mkutano wa viongozi wa nchi na Serikali juu ya usalama wa nguvu za nyuklia wa Nuclear Safety and Security.

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...