February 18, 2010

Sitta: Nipo tayari kwa hukumu yoyote CCM

SPIKA wa Bunge Samuel Sitta amesema yupo tayari kwa hukumu yoyote itakayotolewa na chama chake CCM, iwapo msimamo wake wa kupinga ufisadi, rushwa na maovu ndani ya chama hicho, utaonekana ni tatizo.

Sitta alitoa msimamo huo jana katika mahojiano maalumu na gazeti hili ambapo pia alibainisha kuwa hatua zilizochukuliwa na CCM kupitia kamati maalumu ya Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi kwenye kikao cha Nec, itasaidia kupunguza uhasama ndani ya chama hicho.

"Nasema uhasama ni suala la moyo wa mtu na la kibinadamu kabisa na mifano ni mingi tu. Lakini, watu wanapokuwa na uhasama, imani inabaki vile vile. Mimi nitaendelea kukemea ufisadi, rushwa na kama hilo ndilo litakuwa ni tatizo kwa CCM, basi nitakuwa tayari kwa hukumu yoyote ya Chama Cha Mapinduzi," alisema Spika Sitta na kuongeza:

"Kama nikikemea ufisadi au nikisema kwamba lazima tuwe wakali zaidi ni tatizo kwa CCM, basi nipo tayari kwa hukumu yoyote, eeh".

Source: Mwananchi

No comments:

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...