MKURUGENZI Mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Makete na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), katika serikali ya awamu ya tatu, Dk Hassy Kitine ameonya kwamba, uchafu na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa, mustakabali mbaya wa kisiasa na hali ngumu ya uchumi vinavyoikabili nchi, vinahatarisha usalama wa taifa.
Kauli ya Dk Kitine ambaye alishika wadhifa huo wa Ukurugenzi katikaIdara ya Usalama wa Taifa, wakati serikali ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, imetolewa wakati nchi ikiwa imegubikwa na matatizo mbalimbali yakiwemo ya ufisadi na vita ya chini kwa chini ya kugombea madaraka.
Akizungumza katika mkutano maalumu na baadhi ya vyombo vya habari katika mgahawa wa Viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Salaam jana, Dk Kitine alionya kwamba, uchumi na maliasili za taifa zimeshikwa na wageni, huku Watanzania walio wengi wakifanya kazi za udereva, ufagiaji barabarani, kazi za ndani na mashambani. "Nimewaiteni kuzungumzia mustakabali wa nchi yetu, kama mnavyofahamu mimi nimeshika nafasi mbalimbali nyeti kuanzia wakati wa Mwalimu," alifahamisha. ICHEKI HAPA.
February 19, 2009
Dk Kitine: AZOZA.
Dk Kitine: Nchi iko hatarini
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
It has been a while now that my life had taken on a sense of expectation. It has been almost 3 months since I met Russell Simmons at a char...
-
It’s not important to hold all the good cards in life. It`s important how well you play the cards which you hold. Often, when we lose...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
Gadhafi na Obama With reported pockets of fighting remaining in Tripoli on Wednesday, the whereabouts of Lib...
-
President Obama's Responses to Yoani Sanchez's Questions Thank you for this opportunity to exchange views with you and your re...
-
MALUIMBANO kuhusu waraka wa Kanisa Katoliki (RC) yanaendelea kuwa makali, baada ya waumini wa kanisa hilo kumuelezea mwanasiasa mkongwe nchi...
-
Thank you. Thank you. Thank you so much. (Sustained cheers, applause.) Tonight, more than 200 years after a former colony w...
1 comment:
Amezungumza ya maana kuliko nilivyowahi kusikia la maana lolote katika siasa za Tanzania baada ya Nyerere J. Kambarage. Tatizo ni kuwa hao wanaozungumziwa hawataona ukweli huu bali watajitahidi sana kupinga na kupuuzia maonyo haya kama vile hayawahusu, na hapo ndipo chanzo cha kutokufika kokote katika hatua za kimaendeleo. Sijui tuna viongozi wenye ubongo wa aina gani.
Post a Comment