January 21, 2011
Kisa cha Ngombe, Mzee na mtoto mwenye hekima
Niliwai kusoma hadithi hii mahali fulani, kwa bahati isiyo njema sikumbuki ni kitabu gani, anyway hadithi yenyewe iko hivi:-
Mzee mmoja mfugaji akiwa na mwanae mdogo alikwenda kuchunga mifugo yake wakiwamo Ng'ombe kadhaa, katika kundi lile ng'ombe mmoja alizaa kandama hukohuko polini, ilipofika jioni ilibidi kuwarudisha mifugo yake zizini, wote waliongoza njia isipokuwa yule ngombe na ndama wake, ndama yule baada ya miguu yake kupata nguvu alikuwa anarukaruka tu kule polini.
Mzee yule alikuwa akiangaika kumchapa ngombe mzazi ili aongoze njia ya zizini lakini ngombe yule hakuwa tayari kwani ndama alikuwa bado akivinjali polini kule, Mzee aliangaika kwa kitambo bila mafanikio huku mwanae akimwangalia tu.
Mwishoe mtoto akamshauri babaye, akamwambia- "Baba kwanini usimbebe yule ndama? kwani mamaye atakufuta tu"
Mzee akumwelewa kwanza mtoto wake aliendelea kidogo kumlazimisha ngombe wake, mwishoni akaamua kujaribu kufuata ushauri ule lakini kwa namna ya kujifanya yeye ndo kaamua, akambeba ndama na hatimaye ng'ombe naye akamfata mpaka zizini.
Jambo lile la kushauriwa na mtoto wake tena wa miaka kumi tu lilimkwaza sana mzee yule alifikiri saaana mwishowe akafanya kitendo cha kijinga, akaamua kujinyonga, kisa, kushauriwa na mtoto mdogo.
Sitarajii baba zetu nao watafanya kitendo cha kijinga kama cha mzee mfugaji yule, sitarajii, nina hakika baba zetu leo hii wanabusara sana, wataona ushauri wa mtoto ni changamoto ya kujitafakari na kuamua kwa busara zaidi sasa na wakati ujao pi.
Hongereni sana VIJANA kwa kukataa kukaa kimya.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Dr H Mwakyembe akishushwa toka ktk ndege ya kukodi na kupelekwa moja kwa moja MOI kwa Matibabu zaidi, Dr Mwakyembe alipata ajali ya gari m...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
Mineral occurrence in Tanzania by TMAA UONGEZAJI WA PATO LA MTANZANIA Mheshimiwa Spika, 46. Lengo la Dir...