November 12, 2008
NATAMANI NIJUI WANACHOFURAHIA!!
MWENZENU NATAMANI NIJUE KILE WALICHOKUWA WAKITETA WAHESHIMIWA HAWA HATA KUMWAGA BATASAMU LA NGUVU MSIBANI KWA NYAULAWA..............
Nyaulawa aagwa Dar
RAIS Jakaya Kikwete pamoja na mkewe Mama Salma leo wameongoza mamia ya waombolezaji wakiwamo viongozi wa serikali, wabunge na wananchi kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa (57) aliyefariki dunia Jumapili nyumbani kwake, Kawe Beach, Dar es Salaam. Mwili wa marehemu Nyaulawa umeagwa kwa Ibada ya Misa iliyoongozwa na Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Martha, Mikocheni, Padri Paul Haule na kisha heshima hizo za mwisho.
MLIMANI WATIMULIWA
BAADA ya wanafunzi kugoma kuingia madarasani Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani umewasimamisha masomo wanafunzi wote wa shahada ya kwanza kwa mudu usiojulikana. Hatua hiyo imechuliwa baada ya wanafunzi hao kukaidi agizo la Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Jumanne Maghembe la kuwataka warejee madarasani jana ifikapo saa moja asubuhi. Hata hivyo wanafunzi hao waliendelea na mgomo huo hali iliyolazimu uongozi wa chuo hicho kuchukua hatua za kuwasimamisha kwa lengo la kurejesha amani chuoni hapo. Wanafunzi hao wapatao 16,000 waliamuriwa kuondoka maeneo ya mlimani ifikapo saa 12 jioni. Polisi walitumika kuhakikisha wanafunzi hao wanaondoka maeneo hayo bila kufanya uharibifu wowote. Uamuzi huo umechukuliwa baada ya wanafunzi hao kukiuka sheria za chuo hicho kwa kutoingia darasani kwa siku tatu mfululizo kwa madai ya kupinga sera ya uchangiaji na kutaka Serikali iwapatie mkopo kwa asilimia 100.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...
-
Dr H Mwakyembe akishushwa toka ktk ndege ya kukodi na kupelekwa moja kwa moja MOI kwa Matibabu zaidi, Dr Mwakyembe alipata ajali ya gari m...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...