April 21, 2010

Pamoja na nyongeza 100% Mgomo uko palepale - TUCTA

SERIKALI imepandisha kima cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi kwa asilimia 100, huku wafanyakazi wa Serikali na sekta ya umma, wakitakiwa kuvuta subira hadi Jumapili ijayo wadau watakapokaa kujadili.
Hata hivyo, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (Tucta), limesema tamko hilo la Serikali ni siasa na msimamo wao hautarudisha nyuma nia ya wafanyakazi kugoma Mei tano mwaka huu, endapo madai yao makuu matatu hayatatekelezwa kabla ya Mei Mosi.
Katika madai hayo makubwa, Tucta wanaitaka Serikali iongeze kima cha chini cha mshahara, ipunguze kodi inayokatwa katika mishahara (PAYE) na kuongeza malipo yanayotolewa na mifuko ya pensheni.
Hata hivyo, msimamo huo wa Serikali na wa Tucta umetolewa wakati taarifa za Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), zikionesha kuwa kiwango cha chini cha mshahara wa Tanzania ni kikubwa kuliko Kenya na Uganda.
SOURCE: Habarileo

Bunge larekebisha Sheria Gharama za Uchaguzi- JE KWATOSHA

Bunge limepitisha kwa kauli moja marekebisho ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya Mwaka 2010, baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, kuwasilisha bungeni muswada wa sheria unaopendekeza marekebisho ya sheria 16, ikiwamo sheria hiyo.

Hatua hiyo ilifikiwa jana na Bunge, zikiwa zimepita wiki chache tangu Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, kukaririwa na vyombo vya habari akilalamikia kitendo cha serikali kuingiza vifungu ndani ya sheria hiyo kinyemela.

Vifungu vilivyolalamikiwa na Dk. Slaa kwamba, viliingizwa katika sheria hiyo nje ya utaratibu wa Bunge, ni pamoja na vifungu vidogo vya 1, 2 na 3.

Dk. Slaa, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chadema, alisema vifungu hivyo viliingizwa katika Kifungu cha 7 baada ya sheria hiyo kujadiliwa na kupitishwa na Bunge, kitu ambacho ni kinyume na utaratibu.

Kutokana na hilo, Dk Slaa, alitaka sheria hiyo irudishwe bungeni ili vifungu hivyo viondolewe mara moja.

swali!!

Wadau je kuingiza vifungu kinyemela na baadaye kushtukiwa lakini pamoja na kushtukiwa huko wakana na sasa waamua kuondoa vifungu ama kurekebisha tu kwatosha? hakuna makosa mahali fulani hapo? Je Mkuu wa Nchi hakudanganywa ama kuuziwa mbuzi kwenye gunia?

source:Nipashe

"they shall never perish"

Siku inakuwa njema sana uhamkapo na kupata ujumbe mzuri kama huu. ASANTE YESU.

“I give them eternal life, and they shall never perish; no one can snatch them out of my hand. My Father, who has given them to me, is greater than all; no one can snatch them out of my Father's hand. I and the Father are one.- John 10:28-30

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...