February 28, 2009

Hasheem aendelea kutesa USA.

Kijana Hasheem Thabit anaendelea kufanya vyema huko majuu, fuatilia mahojiano yake zaidi hapa>>>>

Birth Day yangu hi wapi???

Mdau anasema kazaliwa tarehe 29 mwezi wa pili sasa arihadiwa zawadi nono na mpenzi wake sasa hajui hafanyeje maana anaona yapita dry. Je aisherehekee lini siku yake hii muhimu?????

Kikwete awaonya viongozi wastaafu

Rais Jakaya Kikwete amewaonya viongozi wa serikali wastaafu kuacha kuingilia serikali ya sasa, kwa kutoa kauli ‘vijiweni’ zinazoashiria kuwa serikali yake imeshindwa kiutendaji. Bila kutaja moja kwa moja wahusika, Rais Kikwete alisema viongozi hao wanasahau kuwa wanayoyasema hawakuyafanyia kazi wakati wa uongozi wao. Ifate hapa

February 27, 2009

Niingie kichwakichwa???????????????????

Jamaa kantumia hii leo toka kwa Putin eti ana mahela hayana kazi, nilitaka kuingia kichwakichwa lakini hako kamstari kekundu ndo kamenishutua na hizo link zote usanii tu

Good day,

I am Nikolay Sintsov,personal assistant to Mikhail Khodorkovsky,once rated as the richest man in Russia and owner of YUKOS OIL (Russian largest oil company),chairman CEO: Menatep SBP Bank (a well reputable financial institution with its branches all over the world).

SOURCE OF FUNDS:

I have a profiling amount in an excess of US$40.5M, which I seek you to accommodate for me. You will be rewarded with 40% of the total sum for your partnership. Can you handle this? As his personal assistant, I was authorized to transfer money of an American oil merchant for his last oil deal with my boss Mikhail Khodorkovsky.The funds have since left the shores of America to a European private financial institution where the final crediting is to be carried out.

While I was on the process, my boss got arrested for his involvement in politics by financing the leading and opposing political parties (the Union of Right Forces, led by Boris Nemtsov, and (Yabloko, a liberal/social democratic party led by Gregor Yavlinsky), which posed as a threat to President Vladimir Putin's second Tenure as Russian president.

Since then, I have placed on hold all transactions concerning this amount.

You can catch more of the story on this website: http://www.yukos.com http://news.ft.com/cms/4bb9612a-d254-11d8-b661-00000e2511c8.html http://www.hoovers.com/yukos/--ID__53700--/free-co-factsheet.xhtml http://newsfromrussia.com/main/2003/11/13/51215.html

YOUR ROLE: All I need from you is to stand as the beneficiary of the above mentioned sum and I will re-profile the funds with your data, which will enable the financial firm transfer the sum to you.

I have decided to use this sum to relocate to the American continent and never to be connected to any of Mikhail Khodorkovsky conglomerates, presently I am in Burkina faso, West Africa,for a hide out,as it's a remote country. The transaction has to be concluded as soon and as I confirm your readiness to proceed with me, I will provide you with details. Thank you very much.

Regards, Mr.Nikolay Sintsov

Mchungaji Balozi

Mchungaji Balozi Charles Stith akizindua report ya utendaji ya viongozi wa Africa leo hii jijini.

February 26, 2009

Ban Ki Moon

JK na Ban Ki Moon.
Mdau Bakari Machumuktk Lecture ya Boss wa UN.
Mkurugenzi wa TBC Tido Mhando akifuatilia kwa makini.
Boss wa UN Ban Ki Moon amekutana na Rais Kikwete na kutoa lecture ya nguvu jijini Dar.

Tigo yapiga jeki shule,

Ofisa Mauzo wa Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo Kanda ya Kusini, LadislausKarlo (kushoto), akimkabidhi Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa,Pindi Chana (kulia) sehemu ya mabati 113 yenye thamani ya shs milioni3 yaliyotolewa na kampuni hiyo kuchangia ujenzi wa Shule ya Sekondari ChiefKidulile iliyopo Wilayani Ludewa Mkoani Iringa. Wa pili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Wilayaya Ludewa, John Mahali.

Boss wa UN atua Bongo

Katibu Mkuu wa UN Ban Ki Moon ametua mchana huu Bongo kuanza ziara ya siku mbili na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje Bw Bernard Membe, anatarajiwa pia kwenda Zanzibar na Arusha hapo kesho. Karibu sana BONGO Bw Ban, hapa ndipo anapotoka msaidizi wako wa karibu Mama yetu Dr Asha Rose Migiro

February 25, 2009

Lipumba kungoka CUF leo?

Uhakiki ulikuwa wa nguvu hili kuakikisha wanaoingia ni wajumbe halali tu.
Coplo Mstaafu Stephen Masanja anagombea uenyekiti pia.
Prof Abdalah Safari
Uhakiki kabla ya kuingia mkutanoni kwa ajili ya kupiga kula.
Chama cha CUF kinafanya uchaguzi wake mkuu leo hapa Diamond Jubilee ambapo nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu zinatarajiwa kujazwa,
Hata hivyo ni nafasi ya Mwenyekiti tu ndo yenye upinzania ambapo wanachama wawili wameomba kugombea na Prof Lipumba ambaya anatetea nafasi yake, Katibu Mkuu Maalimu Seif na Makame Machano Khamis wamekosa wapinzani.
Wanaogombea Uenyekiti pamoja na Lipumba ni Prof Abdalah Safari na Mstaafu wa JWTZ Cpl Spephen Masanja.

THE 1st and GREATEST COMMANDMENT

“Jesus replied: " 'Love the Lord your God with all your heart and with all your soul and with all your mind.' This is the first and greatest commandment. And the second is like it: 'Love your neighbor as yourself.”- Matthew 22:37-39

February 24, 2009

Pana nnkono wa nntu au???????

Gari lililokuwa likitumiwa na CCM ktk kampeni za uchaguzi huko Mbeya Vijijini likiteketea kwa moto. Ifate mwenyewe hapa.

Ki Moon akija Afrika, Dr Asha Rose YUKO ULAYA

Deputy Secretary-General Asha-Rose Migiro (centre) meets with Ingeborg Grässle (left), Member of the Budget Control Committee of the European Parliament; and Herbert Bösch, Chairman of the Budget Control Committee of the European Parliament. Wakti tunatarajia ugeni mkubwa wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Ban Ki Moon wiki hii, Mama yetu na mpendwa wetu mwakilishi ktk chombo hiki kikubwa zaidi Ulimwenguni naye amekuwa bize uko Ulaya ktk kuweka mambo sawa ya kidunia. Tanzania inajivunia sana mama yetu huyu.

MMEFURAHI?????????- Liyumba

Mtuhumiwa namba moja wa kesi ya BOT Amatus Liyumba ameibuka leo mahakamani Kisutu kinyume na taarifa kuwa alikuwa ametoweka.

Makali ya mtikisiko wa Uchimu....

VODAFONE YAPUNGUZA WAFANYAKAZI

Vodafone (VOD.L), the world's largest mobile phone group by revenue, is to cut hundreds of jobs in Britain, according to a report on Sky News. The move to cut jobs could be made as early as Tuesday, said the report.

The mobile phone operator, which employs 10,000 people, has previously said it will boost free cash flow by cutting 1 billion pounds of costs. Vodafone declined to comment on specific job cuts. Shares in Vodafone climbed 1.59 percent at 127.5 at 2:46 p.m., in line with a 1.7 percent rise in the European sector .SXKP.

Loud Silence....by Upendo H.

Not all old is wise…

I am very tired of shallow minded people who like to put tags on everything. Do they not know that everything does not always come with a price tag?

For example, if you do not have a degree you are considered “unfit,” but I can mention numerous people who do not have a degree and have still made it.

Bill Gates being the richest man in the world I imagine does not go around preaching how well and better a person he is. I can also mention a couple of people who have degrees up to P.H.Ds who are just disconnected from this world.

For instance I remember having a teacher in O`level who had a P.H.D in the subject she was teaching, and God knows she was the most boring, slow and uninspiring teacher I ever had to listen too.

But this is not a name calling article, what I truly want to express out there to the world is that this world that is full of judgment a prejudice is a sad and suffocating one, and if it shall continue like this I will loose my mind before they send me to the grave!

I have a friend who makes me feel like I am crazy every time I want to watch a programme on television on fashion; he thinks that I should always watch the news.

I agree on the watching news part, but do not agree on the fact that it has to be all the time. I love watching the news and knowing what happens on a daily basis not on an hourly basis! What really drives me to the curb is the whole idea that I automatically become stupid, simply because I do not watch the news the whole time.

So let’s say not everyone has experienced this, but I have another example on why I am so irritated.

There was a time I managed to secure a job at a much respected place. Of course I found people who had been there for a long time, people who knew the ins and outs of the company, people who knew everyone and the sort.

So here I was young and full of new ideas that were ready to burst out, I was ready to change the world, or so I thought.

With my bright ideas I was unstoppable… for like a minute when they were all suddenly shuttered by a simple statement “we do not do things that way”. I have to admit that it hurt me, but I was composed and no one could tell I was crushed.

But it did get me thinking, a company like that full of old people still operating in the seventies, and here I was trying to make some constructive criticism, and for what? To be told I was too young and inexperienced to know what I was talking about. I must say, I do not like people who tend to feel superior just because they are twenty years older than someone… some even say that height has something to do with it.

They say ( men especially) people who are short and small tend to have an inferiority complex, and would do things just to get attention.

Imagine having a boss who has this complexity? Exactly you would not. I do not know the extent of this theory, but in my young “stupid” years I have observed quite a number, one I even work with.

Somehow these kinds of people who are rigid at all times tend to be sad and hypocritical. Because if they are old and wise, surely they must know that change is inevitable.

I guess God made people to be different for this very reason, to challenge, to make us think and to drive us mad, and eventually to love one another, because eventually we do love one another.

February 23, 2009

Karibu tene Rais wa Uturuki.

"Cheeers" JK na mgeni wake Rais Abdullah Gul wa Uturuki wakigonga glasi wakati wa dhifa ya kitaifa iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salam jana usiku
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimpa zawadi mke wa Rais wa Uturuki Bi.Hayrunnisa Gul wakati mgenu huyo alipomtembelea Mama Kikwete katika ofisi za WAMA leo hii.

CUF Chama mbadala

CHAMA CHA WANACHI CUF KIMEANZA MKUTANO WAKE MKUU WA KITAIFA WA SIKU TATU AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MEMGINE KITACHAGUA VIONGOZOZI WAPYA AMA KUWAREJESHA WAZAMANI MADARAKANI.

MKUTANO HUO MKUU ULIUDHURIWA NA MABALOZI MBALIMBALI NA VIONGOZI KADHAA WA VYAMA IKIWEPO CHAMA TAWALA CCM KILICHOWAKILISHWA NA MWENYEKITI WA MKOA DSM KWA NIABA YA MAKAMU WAKE PIUS MSEKWA.

KILA LA KHERI CUF.

February 21, 2009

Pengo aazimisha silver Jubilee.

Askofu Mkuu wa Jimbo kuu Katoliki la Dar Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo leo ameazimisha miaka 25 ya uaskofu kwa ibada iliyoudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Rais mstaafu Ben Mkapa.
Pia ametumia shereh hizo kuzindua rasmi TV Tumaini.

Kuchka dawa jamani ooh!!!

Nimeifuma barua hii mahali fulani, yaani nimecheka mpaka basi.....

February 19, 2009

Jukwaa lakubali yaishe..

JUKWAA la Wahariri Co Limited limetangaza kumfungulia Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni George Mkuchika baada ya kugoma kuandika habari zake kwa takribani miezi minne sasa.

“Tayari gazeti liko mitaani, tunatangaza kumfungulia Mkuchuka. Lakini pia tunalaani kitendo cha kutumia sheria mbovu kuvifungia vyombo vya habari,” alisema mwenyekiti wa jukwaa hilo Sakina Datoo. Hata hivyo jukwaa hilo lilikishambulia kituo cha televisheni cha ITV kuwa kilifikia hatua ya kurusha habari za waziri huyo hasa baada ya Mkuchika mwenyewe kuzungumzia habari zinamlinda mmiliki wa kituo hicho Reginald Mengi.

Liyumba atoweka????????

Wadhamini wa mshitakiwa Amatus Liyumba, Benjamin Nguluguni (kushoto) na Otto Agaton, wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam leo baada ya kukamatwa kwa kukosekana mshtakiwa Liyumba.
DHAMANA aliyopewa Amatus Liyumba imeingia dosari baada ya mahakama kutoa amri ya kukamatwa pamoja na wadhamini wake, lakini juzi na jana alisakwa na maafisa wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) lakini hakuonekana.

Alitakiwa apandishwe mahakamani jana, lakini badala yake maafisa wa takukuru waliambulia kuwakamata wadhamini na wakakiri mahakamani hapo kuwa Liyumba haonekani. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu juzi ilitoa hati ya kukamatwa kwa Liyumba ikiwa ni siku moja tu baada ya kupewa dhamana na mahakama hiyo katika mazingira ambayo hayakuwaridhisha upande wa mashitaka. Hakimu Hadija Msongo jana alikiri kuwa mahakama hiyo ilitoa hati ya kukamtwa kwa mshitakiwa huyo pamoja na wadhamini wake. Hata hivyo hakueleza sababu ya mahakama kutoa hati hiyo kwa kile alichodai kuwa jalada la kesi hiyo tayari limepelekwa mahakama kuu. Ifate hapa baadaye.

Dk Kitine: AZOZA.

Dk Kitine: Nchi iko hatarini

MKURUGENZI Mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Makete na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), katika serikali ya awamu ya tatu, Dk Hassy Kitine ameonya kwamba, uchafu na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa, mustakabali mbaya wa kisiasa na hali ngumu ya uchumi vinavyoikabili nchi, vinahatarisha usalama wa taifa.

Kauli ya Dk Kitine ambaye alishika wadhifa huo wa Ukurugenzi katikaIdara ya Usalama wa Taifa, wakati serikali ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, imetolewa wakati nchi ikiwa imegubikwa na matatizo mbalimbali yakiwemo ya ufisadi na vita ya chini kwa chini ya kugombea madaraka.

Akizungumza katika mkutano maalumu na baadhi ya vyombo vya habari katika mgahawa wa Viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Salaam jana, Dk Kitine alionya kwamba, uchumi na maliasili za taifa zimeshikwa na wageni, huku Watanzania walio wengi wakifanya kazi za udereva, ufagiaji barabarani, kazi za ndani na mashambani. "Nimewaiteni kuzungumzia mustakabali wa nchi yetu, kama mnavyofahamu mimi nimeshika nafasi mbalimbali nyeti kuanzia wakati wa Mwalimu," alifahamisha. ICHEKI HAPA.

KP NA WENYE NACHO

Hakika WENYE NACHO ndipo walipoifikisha taaluma ya uandishi wa habari hapa nchini.

Je kwa stahili hii tutafika kweli????????????????????

Asante KP, Ujumbe umefika

.

Liyumba atoweka??????

Kuna taarifa kuwa Mtuhumiwa wa KESI YA Ujenzi tata wa minara miwili ya BOT A. Liyumba ametoroka na ajulikani alipo na kuwa wadhamini wake 2 wanashikiliwa na polisi kuhusiana na hilo.
Jana mawakili wanaomtetea Liyumba toka Amacus Attorneys Hudson Ndusyepo na Onesmo Kyauke (R) walithibitishia waandishi kuwa mteja wao alipewa dhamana licha ya kutotimiza masharti pamoja na kuwasilisha mahakamani hati ya kusafilia iliyopitwa muda wake(PASSPORT EXPIRED 2007).
Habari ndo hiyo wadau.

TUNGALI TUNAFUATILIA MAHAKAMANI KISUTU TUTAWAJULISHA TAARIFA KAMILI ZAIDI SI MUDA.

DEMOKRASIA

Uenyekiti wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania emekabidhiwa rasmi kwa CCM kutoka kwa UDP leo hii, Kiti hiki kitakuwa kinakaliwa kwa kupokezana kila baada ya mwaka mmoja kwa vyama vyote vyenye wabunge kwa kufuata mpangilio wa erufi.
John Cheyo alikabidhi rasmi kwa Pius Msekwa makamu wa CCM Bara.

February 17, 2009

WHY I LOVE BONGO!!!!

Bongo ndo pahala pekee duniani humu waweza fanya mambo yako kienyeji, kuanzisha mradi wowote na hata kujipendelea kwa kupoka huduma ya jamii nzima na kujimilikisha na kisha ukapanga ni kiasi gani uwalipe wahusika na asikuoji wala kukusumbua awaye yote yule na bado mambo yakakuendea bomba tu, ka ka-shamba haka ka-matanki ya maji huko Mbezi Africana na Mwekezaji huyu ambaye amejitahidi kuwekeza hapa baada ya kujinyima kweli au kulala njaa kwa jina la save bajeti.
Anasema anaweza kujipatia tulita laki na nusu tu kwa siku na kugawa kwa tujibiashara twake uto tudogo tu na kila mwisho wa mwezi ulazimika kujikamua kwelikweli kuwalipa DAWASCO libili la kumkomoa la TSHS 122,000/- , analalamika kuwa anaonewa sana na hawa jamaa kwani HILO LIBILI NI KUBWA SANA kulinga na tujimaji atumiatwo, yaani tulita laki moja na nusu tu kwa siku, zaidi soma hapa.
Hayo ndo ya huku kwetu BONGO, Ndo maana naipenda sana Bongo!!!!

February 16, 2009

Huyu ndo ...........................!!!!!!

JK akimtambulisha Prof Lipumba kwa Hu Jintao wakti wa Difha ya kitaifa.

"SIMU POCHI" NA ZAIN au ZAP

CEO wa CITIBANK Omar Hafeez mmoja wa wadhamini akiwa na Irene Madeje wa Zain
ZAIN LEO WAMEZINDUA HUDUMA MPYA AMBAPO SIMU YAKO YA MKONONI SASA NDIO BANK YAKO, KWANI WAWEZA SI KUTUMA TU BALI PIA KUWEKA, KULIPIA HUDUMA N.K HAYO NDO MAMBO YA ZAIN ZAIDI TEMBELEA TOVUTI YAO

LILIYEYUKAJE HILI DUBWANA??????????

Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa yapata wiki mbili zilizopita.
Hii ndo aina ya mashine zilizoibwa yapata wiki mbili zilizopita pale ORCI zaitwa Control Console, zimenunuliwa tena mpya kwa gharama ya Dola za US 22,000/- na hivyo wagonjwa wameanza tena leo kupata huduma baada ya kusimama kwa muda wote huo.

Tutafakali. Wadau niliposikia kuibwa/kutoweka au kuyeyuka kama barafu au mafuta kikaangoni isia zangu zilinituma kuwa hako kajifaa katakuwa ni kadogo tu pengine ukubwa wa simu ya kiganjani labda, haikunijia akili kuwa ni lidubwana likubwa kiasi hicho (yaani hiyo hizo kama screen mbili za kompyuta nyeupe na nyeusi mara mbili) ukweli sikuamini macho yangu nilivyonyeshwa na wahusika kuwa zilizoibwa ni kama hizi hapa!!!!!!!!!!

Cha kushangaza zaidi ni kuwa aina hii ya mashine kwa Afrika Mashariki na kati ni Tanzania tu ndo tunayo na huu ulikuwa ni msaaada wa shirika la nguvu za atomic la dunia na ilizinduliwa na JK Mwaka jana Mei tu, yaani hata mwaka mmoja bado toka tusaidiwe mashine hii.

Sitaki kutia chumvi wala kumnyooshea mtu kidole kwani polisi inaendelea na uchunguzi wake na sijui lini watamaliza, lakini nna maswali machache wadau ambayo naomba tushauriane kwa wema tu,

1. Mijidubwana mikubwa kama hii inawezawezaje kuyeyuka ka barafu hapo mezani pasi kuonekana na awaye yeyote????

2. Ikiwa ni Tz tu tunayo na tena hapo tu ORCI katika EAC and C, je yu wapi mteja au mseti ilikopelekwa hiyo mimashine? au inamatumizi gani mengine mbali na kutibu saratani??????

3. Hivi awaye yote alokuja chukua na kutoweka na mashine za namna hiyo au ukubwa huo alizibebabebaje? kwa lambo?? au katia mfukoni tu??????

4. Utaifa uko wapi kwa Watanzania wa leo jamani????? unapoiba kifaa kinachookoa maisha ya nduguzo, rafikizo, kaka na dadazo au mama na baba yako je uitwe nani????????? muuaji????? sijui ila yupo ajuaye.

February 13, 2009

February 12, 2009

Huu ni ulevi wa madaraka au????????????

DC AAMURU WALIMU WACHARAZWE VIBOKO MKUU wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali, ameacha maswali miongoni mwa walimu baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika shule tatu za msingi za kata ya Katerero na kuamuru walimu 16 kucharazwa viboko kwa kile alichodai ni utoro na uchelewaji wao.

“Nikamwita askari wangu nikamwambia Mwalimu Mkuu atoke, tukafunga mlango nikawaambia walimu kama watoto wanaochelewa mnawapa adhabu na mimi nawapa adhabu,” alisema Mnali kuthibitisha kucharazwa viboko vinne kila mmoja.

Walimu waliocharazwa ni Generosa Lwakatare, Ernestina Anatory, Jonesta Grenos, Hawa Ayubu, Rehema Baisi, Frieda Laurian, Avitus Leonald na Asirath Ndyamukama wa Katerero.

Wengine ni Amos Kamugisha, J.K. Zale, Bruno Francis, M. Mwesiga, Pulleti Rugemalila, Winfrida Kakurwa, Editha Bigilwa, Ester Mutashaba, Ludovic Bushongole, Gosbert William, Venance Philipo na Vedasto Munabi wa Kansenene.

Walimu wengine waliochapwa ni Imelda Lwegalulira, Coretha Ernest, Devotha Bushobe, Augustina Bampenja, Josephina Ndyamukama, Julius Katemana, Videlieth Yesse, Generoza Mulokozi, Sylvester Petro, Josiah Kamuhabwa na Concessa Rweyemamu wa Kanazi.

“Ni kweli tukio hilo limetokea … ni vyema DC na huyo Polisi wakapimwa afya kwa sababu hii si hali ya kawaida, kwani zipo taratibu za kinidhamu za kuchukua kwa watumishi,” alisema Naibu Waziri wa Elimu MWANTUMU Mahiza ambaye kitaaluma ni mwalimu.

WAASIA "WAUAJI" WAPANDA KIZIMBANI.

Watuhumiwa wa mauaji ya kutisha yaliyotekea jijini hivi karibuni Vinoth Praveen (23) na na mkewe Komal Bupendra (23) wamefikishwa mahakamani leo hii. Wanatuhumiwa kumuua Abdul Basit Abdallah kumkatakata na mwili kuuweka katika begi na kuutelekeza ndani ya gari katika jengo la J.M Mall, alikuwa akiwadai pesa kiasi cha dola za USA 20,000.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...